Angalizo kwa wanunuzi wa Colgate

Angalizo kwa wanunuzi wa Colgate

Naenda kutupa ile faster huenda ni feki ndo maana fizi zimechubuka
 
Hii ni colgate triple action nimeichukua leo dakika chache zilizopita baada ya kuiona ina features chache za boksi ya colgate original......

Ninaitumia na muda mfupi ujao nitawapa mrejesho......

Ukitazama hiyo boksi utaona ina mlango wa kufungua na kufunga. Hata kama ukienda dukani ukaikuta ni rahisi hata kuibinya na kuitaste ladha yake na kubaini kama inawalakini ama ipo sawa.

Pia utaweza kuona alama ya Barcode katika hiyo boksi ingawa katika hii tube ya dawa sijaona barcode yoyote ndio najaribu kucheki hapa niitumie kisha nibaini kama ipo vema ama la.
 
nami ni mpenzi wa colgate na sasa nitakuwa makini wakati wa manunuzi
Jaribu kununua katika maduka ya kishua sehemu ambazo wazungu na wahindi wanakwenda kufanya manunuzi ya dawa zao za miswaki utakuta original huku uswazi watu wanatumia feki sababu ya kupenda kuzembea kufuatilia usalama wa bidhaa wanazotumia.
 
Naenda kutupa ile faster huenda ni feki ndo maana fizi zimechubuka
Same thing mimi imenichubua fizi pia na sio kawaida ndio maana nimestuka.....

Yaani nimeitumia mara moja tu nimeitupilia mbali hiyo tube....
 
Bado natafuta....hauwezi amini hizi feki ndizo zimesambaa, nimepita maduka yote kila nikiulizia ile Colgate ya single action nyeupe.....naletewa hizi takataka feki.

Tbs mnakesi ya kujibu kwa kuzembea kuzibaini hizi dawa feki......


Bado natafuta kesho nitajihimu niende maeneo ya mjini kule nikacheki......

Sent from my Infinix HOT 4 using JamiiForums mobile app
Tatizo hata hao wenye madula wanachoangalia ni bidhaa yenye bei nafuu ili wapate wateja wengi. Asante kwa taarifa nami ni mhanga wa hii kitu maana yenyewe kwanza ni kali tofauti na hizi za sasa si kali sana kama ile original
 
Huwa nazinunua kwenye maduka makubwa ya dawa but kwamba ni og au sio og ndio kitu nilikuwa sijui jinsi ya kuangalia hivyo nakushukuru sana mleta mada next tym nitazingatia hizi points ulizotoa hapa,waTanzania wengi sana tunatumia bidhaa fake sema ni vile tu hatujui.
Usiamini hizi
 
Sisi tunaotumia miti kusafishia vinywa hayatuhusu......mi na hayo madude mbalimbali.
 
zamani tulikuwa tuna dawa nzuri sana ya meno ikiitwa bonamed ikitengenezwa Tanzania EMCO Ind. Colgate ilikuwa haiifikii ubora wa hiyo Bonamed
 
Kwisha habari yetu
Ila kwa jinsi waafrika tulivo wagumu tutakufa kwa malaria/kipindupindu sio matokeo ya ubora duni wa Colgate
Ajasema Colgate fake inaua, sasa hiyo ya waafrika kufa kwa malaria na kipindupindu na sio matokeo ya ubora duni wa Colgate, umeitowa wapi mjomba!!!?
 
Elimu nzuri sana ispokuwa mimi hapa nilipo nimezungukwa na ndugu zangu kama nane hivi na wote wanatumia Smartphone lkn cha hajabu hakuna hata mmoja mwenye account ya jf kitu ambacho kitawakosesha kupata elimu hii, ukiachilia mbali wale ambao hawana kabisa hizi smartphone na walioko vijijini pia. Mungu tuepushie mbali na maradhi yatokanayo na matumizi ya Colgate fake.
 
Hii colgate si ata Nairobi inatengenezwa?
Box inasema South Africa, sijawahi sikia Colgate ya Nairobi......nadhani fake zinatokea huko.......

Watu wanaroho mbaya kwakweli......ni heri watutengenezee viatu feki lakini sio madawa na vyakula.....pumbavu hawa
 
Tatizo hata hao wenye madula wanachoangalia ni bidhaa yenye bei nafuu ili wapate wateja wengi. Asante kwa taarifa nami ni mhanga wa hii kitu maana yenyewe kwanza ni kali tofauti na hizi za sasa si kali sana kama ile original
Yes mojawapo ya sifa ya colgate ni ukali hadi inawaka moto mdomoni.....na ukipiga hapo mswaki unakuja kuusikia mdomo mwepesi balaa.
 
Back
Top Bottom