Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao huumba!

Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao huumba!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
57,103
Reaction score
128,722
Wanabodi,

Huu ni wito wangu kwa wana jf wenzangu, Tuwaepuke "Manabii wa Majanga", Prophets of the doom" ambao kazi yao ni kuwanyooshea vidole wenzao na kuwahukumu pasipo uthibitisho, kila kunapotokea tukio baya, na kuwaombea wenzao majanga ikiwemo kuwaombea vifo, au kuwatabiria kifo.

Unapomuombea janga mwenzako, wewe bila kujua, kumbe ndio unajichumia janga kwako au kwa uwapendao as a karma reaction kwa mabaya uliomuombea au kumtabiria kifo mwenzako kwa kutumia kanuni ya tatu ya Newton law of motion isemayo "for every force, there is an equal and opposite reaction, pulling towards that force", yaani kila jema unalowaza, unalopanga, unalosema na unalotenda kwa wengine, litatengeneza karma nzuri ya mema (positive good karma power) ambayo mema hayo uliowaza, uliopanga, uliosema na uliotenda, yatakurudia wewe na kizazi chako, na kila janga,unalowaza, unalopanga, unalosema, unalotenda kwa wengine, linategeneza a bad karma (karma mbaya) ya majanga (negative bad karma power) hivyo majanga hayo yatakurudia wewe na uzao wako!. Tusiwaombee wenzetu majanga, ili tusijichumie majanga!.

Wito huu ni kufuatia kuongezeka kwa threads ambazo haziliombei mema taifa letu na viongozi wake na nyingine kuwaombea hadi vifo wale tunaowahisi ni wabaya wetu. Kwa dini zote, amri kuu kuliko zote ni upendo, kwa jinsi ile Mungu alivyotupenda sisi hadi.... vivyo hivyo nasi tupendane, hata adui mpende, kama ni adhabu, adui yako ataadhibiwa na Mungu kupitia karma ya matendo yake!.

Kauli huumba, hivyo tusishabikie sana kauli zenye negativity na kujikuta kumbe ni sisi tuna sababisha hizo negatives kwa kuziumba kwa kauli zetu. Badala yake tuwe positive kwenye kila jambo, hata tukihisi jambo fulani sio jema, tutumie kitu kinachoitwa affirmatives kubadili negatives kuwa positives.

Miongoni mwa kauli hizi za hawa Prophets of the doom wa humu jf, ni pamoja na kuwatabiria vifo vya ajabu ajabu wenzao, wakiwemo viongozi wetu!. Tusishangilie majanga yoyote kwa binadamu wenzetu, hata hawa viongozi wetu sio miungu watu hawa ni binadamu tuu kama sisi hivyo hata wakiwa ni watu wabaya kiasi gani, hata wakiwa na mioyo ya kishetani kiasi gani, hata watutendee maovu kiasi gani, sisi tuwaombee tuu mema, tuwaombee mafanikio na kuwaombea afya njema na waishi maisha marefu hapa duniani na sio kuwaombea kifo, halafu kama kuna maovu wameyatenda, sisi tusiwahukumu, tusije tukahukumiwa, kazi ya kuwahukumu kwa matendo yao, tumwachie Mungu mwenyewe ambaye ndiye Hakimu Mkuu, na hukumu yake ni kupitia kitu kinachoitwa karma, ambapo kila mmoja wetu atahukumiwa kwa matendo yake, ukitenda mema, utalipwa mema, ukitenda uovu au ubaya, utalipwa uovu au ubaya!.

Ila maisha yameumbwa na kifo pia kumeumbwa, kila mtu ni lazima atakufa siku yake ikifika tena atakufa kifo kile kile alichopangiwa na Mungu ile siku anazaliwa, hivyo tusimtabirie yoyote kifo, tusimuombee yoyote kifo, uhai na kifo ni chini ya mamlaka ya Mungu pekee na sio sisi binadamu.

Haijalishi mtu atakufaje, ila malaika mtoa roho Israel humpitia kila kiumbe humu duniani mara 7x 70 ( saba mara sabini) kila siku ili kuhakikisha saa yake ikifika, hazidishi hata nukta moja ya sekunde, kifo ni kazi ya Mungu hatuna haja kutabiriana vifo humu na wengine hadi kuombea vifo wengine, kwa kufanya hivyo wengine bila kujijua kuwa kumtabiria mwenzako kifo au mabaya ni kujiombea wewe mwenyewe kifo au mabaya hayo kwa kanuni ya karma ya what goes around, comes around kwa kufuata kanuni ya Newton ya every action, there is equal and opposite reaction.

Haijalishi mtu atakufaje, ila kwa yoyote na vyovyote atakavyokufa, kifo hicho ndicho alichoandikiwa na ndicho kilichopangwa ile siku anazaliwa, kwa sababu kuzaliwa na kifo ni mipango ya Mungu pekee. Hata shetani akipanga mipango miovu vipi, kama Mungu hajaridhia, hata wapange vipi, kamwe hawatafanikiwa, kila binadamu atakufa saa ile tuu aliyoandikiwa na kifo kile tuu alichopangiwa kwa mipango ya Mwenyezi Mungu pekee.

Tupendane, tuombeane mema hata maadui zetu, tuwaombee mema hivyo kutengeneza positive karma effects.
"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa ...

Wasalaam.
Paskali
 
Umeanza kuogopa kifo mkuu? Nlikuona jana, naona kaumri kamesogea sogea!!

Anyway, muda na wakati wa sisi kurudi mavumbini ni Siri ya Mungu na watendaji wake. Kinachotokea hadi kuombeana mabaya ni chuki tu za kibinadamu. Uzuri mmoja, Mungu hashawishi au kuendeshwa na hisia za mwanadamu
 
Pasco kama wewe ni mfuatiliaji wa maandiko, imeandikwa ni kufuru kubwa kujifananisha na Mwenyezi Mungu na ufanyapo hivyo hakika utakufa hata kama Mungu alikupangia miaka 50 mbele. Na kukumbushana ndio wajibu wetu wanadamu na kufanya hivyo sio kukuombea mabaya bali mema.
Ila la kujiuliza jee kujifananisha na Mungu ni kufanyaje? Kujiita Mungu?, au kutenda mambo bila kuheshimu haki na mawazo ya binadamu wengine? Kusababisha maisha ya wengine yawe magumu na hata kifo bila kujali? Na au, au, au?
Hapo ndio pagumu kujua. Ila akukumbushaye ni mtu Mpatanishi kati yako na Mungu.
Kheri Wapatanishi maana wataitwa wana wa Mungu.

Good morning!
 
Umenena vyema mkuu lakini unabii si maombi ni ufunuo na katika imani zetu ukifunuliwa lazima utoke nje na ushuhudie.
Faida ya kushuhudia pia ni kuleta maonyo na ufumbuzi wa swala husika sawia alivofanya Mnabii kwa kumuonya bwana yule asijifananishe na Mungu,nadhani anania njema sana ya kumrekebisha pale alipoteleza.
 
Kwa hii hali ngumu ya maisha hizo Negativity hazikosekani.

Hatuwezi tukawaombea mema wakati wanatutendea mabaya.

Tenda jema ulipwe jema.

Najua ile thread ya Godbless Lema ndio imezaa hii thread.
Na wamesahau walivokuwa wanamwombea Lowasa,

huwezi lazimisha hisia za watu,

uko sahihi sana Lema ndo sababu ya Uzi huu
 
Kuna mmoja akifa nahisi watu watafurahi sana

Mbaya zaidi ni kama anatabiriwa/anaombewa kifo....maneno huumba hivyo kadamnasi ikishaomba uondolewe duniani ni hatari sana.
 
Mshua aliupenda sana huu wimbo R.I.P

Dunia msomgamano

Mawazo yamenijia Leo mzee wangu alikuwa akisema. Dunia msomgamano wa watu wenye akili tofauti. Ukitaka kuishi vyema fikiri kabla ya kujibu jifunze Kwa walimwengu, walimwengu wajifunze kwako dunia nikuona mambo halafu kuyasahau.

Mateso nimeshayapata matatizo mengi yamenikuta furaha nyingi nimeshaona Maisha nusu nimeshafanya naelekea usemi sasa lazima niwe na utulivu sababu kuishi kwingi nikuona mengi kuelimisha waliobaki waishi Kwa heshima.

Huyo chunusi huyooo

Dunia msomgamano asema baba nimeona Leo nakubali mie. WENGINE UPENDELEA KUFURAHIA WANAPOSIKIA FULANI KAAFAA OHH. KUFA KWA BINADAMU UPANGWA NA MUNGU NAMUOMBA MWENYEZI ANIPE MAISHA.

Ndala Kasheba

 
Back
Top Bottom