Angalia maamuzi magumu

Angalia maamuzi magumu

shabaan Dogo

Senior Member
Joined
Apr 27, 2014
Posts
196
Reaction score
82
Watanzania na maamuzi magumu;

(1) Huna uhakika wa kula na elfu1 pekee uliyo nayo unaamua kuinywa KIROBA-ni maamuzi magumu.

(2) Huna kitanda wala godoro unaamua KUOA-ni maamuzi magumu.

(3) Huna uwezo wa kumlisha mkeo kazi na kumjaza MIMBA-ni maamuzi magumu.

(4) Shule haina WAALIMU una mpeleka mwanao-ni maamuzi magumu.

(5) Dala dala imejaa hadi mlangoni unaamua KUPANDA- ni maamuzi magumu.

(6) Unalipwa laki 2 una muhonga HAWARA laki1- nimaamuzi magumu.

(7) Mdada unaweka Brazillian ya laki 7 MSHAHARA laki 2- nimaamuzi magumu.

(8) Kufanya mtihani wakati unajua UTAFELI- nimaamuzi magum.

(9) Unaowa/ kuolewa bila kupima VVU -nimaamuzi magum.

(10) Unakubali uvivu wa kufanya kazi uendeleze maisha yako. Unazunguuka huvyo ukitegemea kwamba ipo siku UTAOKOTA fuko la hela-nimaamuzi magumu.

(11) Kama utasoma hapa na kushindwa kuweka maamuzi magumu unayo yajua utakua na mamuuzi magumu mnoo!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
maamuzi magumu ni kumkaribisha stranger nyumbani kwako zen ukamfanya faza house bila kuwa na uhakika kama atailinda familia
 
kuangalia Taarifa ya habari ya saa mbili usiku TBC na kuacha ITV na Star ni maamuzi magumu.
 
Kudiriki kuipigia kura CCM ni Maamuzi magumu zaidi!
 
kutafta pesa wakati wewe ni tajiri pia ni maamuzi magumu
 
Kufungua iyi post yako pia ni maamuzi magumu
 
Magumu zaidi ni pale kijana wa kiume anakaa kijiweni hajibidiishi zaidi ya kusubilia nyumba ya urithi baba yake akifa
 
kusikiliza ushauri wa mwanamke hadi kustaafu siasa wakati ungeliweza kuja kuwa waziri mkuu, ni maamuzi magumu.
 
Kumkaribisha obama ukiamini atakupa msaada kumbe anasaka mafta na gas kwa ajili ya nchi yake na unalijua hilo ni maamuzi magumu.
 
Kuhama chama dola mchana kweupe kama alivyofanya mzee wa maamuzi magumu,nimemuaminia kwa kweli!
 
Kumiliki mke mzuri wakati huna kazi ya kueleweka ni maamuzi magumu!
 
Kuoa mke anaekuzidi kipato nayo pia ni maamuzi magumu
 
-kusikia Haja Na Usiende Chooni Ni Maamuzi Magumu.

-kuendelea Kutenda Dhambi Na Unajua Siku Ya Mwisho Ni Moto (Fire) Ni Maamuzi Magumu.

-kubeba Mimba Shuleni Ni Maamuzi Magumu.

-kukopa Pesa Vodacom Na Kuweka Vocha Kwa Mwingine Ili Usikatwe Na Kununuliwa Muda Wa Maongezi Kupitia Sim Ya Mwingine, Ili Uchati Nayo Ni Maamuzi Magumu.

-kulala Na Kusinzia Umefumbua Macho Ni Maamuzi Magumu,.

-kuandika Meseji Kwa Vifupi Vilivyokithiri Wakati Unajua Unaemtumia Hataielewa Nayo Pia Ni Maamuzi Magumu,

-kuishi Dar, Na Maisha Ya Msongamano Wakati Huna Kazi Ya Kukulazimu Uishi Dar Ni Maamuzi Magumu,.

-sisiemu Kukubali Kushindwa Uchaguzi Hata Kama Kura Zimewatupa Ni Maamuzi Magumu.

-masuper Staa Wa Bongo Kuishi Mikoani Tofauti Na Dar Ni Maamuzi Magumu,.

-kumuacha Mkeo Kwa Sababu Ya Mchepuko Ni Maamuzi Magumu.

-kutumia Mda Kuandika Haya Maneno Mengi Nayo Pia Ni Maamuzi Magumu.........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom