do u mean online interview? hahaah bado sana kwa nchi hii ya Tanganyika...labda baada ya miaka mingine 50 ya uhuruLazma tanzani tufanye interview kwa kutumia software. Itasaidia kuundoa usumbufu huu.
Inawezekana kabisa.kongamano la Udom kujitangaza na kujisafisha kisiasa,kuwa hakuna ajira za kufahamiana
nashangaa kwani walipotuma maombi hawakutuma na cv zao? Kwanini chuo hakiuanza kufanya mchujo kwa cv na kuwabakisha wachache kwa interview.
Sijui hii inaashiria nin kwa sisi ambao bado tuko mashulen!
Wangepokea maombi kisha wakachuja kutokana na CVs jinsi zilivyokaa baadae wakatangaza majina machache ambayo ndiyo yatafanyiwa interview.
Mkuu hapa kuna mambo mawiliKama hari ndio hii basi somo la Entrepreneurship linatakiwa kutiliwa mkazo mashuleni inasikitisha kuona watu zaidi ya 1000 wakigombania nafasi kumi this is very shame kwa wasomi wetu wakati kuna opportunity kibao bongo.
Kila siku nazidi kujionea dalili kwamba Watanzania namnagani vipi. See this:
- Inakuwaje interview watu waitwe weekend? Ijumaa, interview ifanyike J'pili
- Uharaka wa nini hapa? kwa manufaa ya nani?
- Inakuaje watu waitwe kijumla jumla? hii inaendana na uharaka uliooneshwa kwa kuita watu weekend?
- Gharama za kutahini kundi lote hilo la watu ni busara? zimelipwa na nani? kwa manufaa ya nani?
Ni wazi kabisa kwamba lengo lilikuwa kuwanufaisha (1) wenye biashara ya usafiri, (2) wenye biashara za chakula na nyumba za kulala wageni (2) wenye biashara ya photocopy, etc.
Nachukua fursa hii kuwashukuru (au kuwapa pole) nyote mliotumia kidogo mlichonacho kuchangia kwa kushiriki kwenye interview hiyo YA AJABU AJABU FASTA FASTA. Hii ndo Tanzania, upende usipende.