Anayekutawala amekuzidi Akili

Anayekutawala amekuzidi Akili

Kama mabavu yangekuwa yanatawala basi wanyama kama tembo na faru wangetawala hii dunia.

Alafu mtu anaweza kuwa na panga akaja kwako lakini wewe ukawa na Bastola ambayo ukivuta tuu kidole mtu anapasuka kichwa.

Hao wanaotumia mapanga ndio haohao wanaotumikishwa miaka nenda rudi.

Elewa kuwa mabavu bila akili ni kama punda tuu.
Kwenye comment yangu ya mwanzo nimekuonesha namna jamii mbalimbali zote duniani zilitumia mabavu kutawaliana.

Kitu ambacho kinapingana na dhana yako kuwa jamii fulani ina akili nyingi kwa sababu ya kuitawala jamii nyengine kitu ambacho sicho.

Kwa faida zaidi nikuongezee kuwa wachina ndio jamii ya mwanzo kufika Afrika mashariki kabla hata wazungu hawana mpango huo lakini hawakuitawala east Africa zaidi ya kufanya biashara na kuondoka ila wazungu walitumia mabavu kutawala east Africa.
 
Kwenye comment yangu ya mwanzo nimekuonesha namna jamii mbalimbali zoye duniani zilitumia mabavu kutawaliana.

Kitu ambacho kinapingana na dhana yako kuwa jamii fulani ina akili nyingi kwa sababu ya kuitawala jamii nyengine kitu ambacho sicho.

Kwa faida zaidi nikuongezee kuwa wachina nduo jamii ya mwanzo kufika Afrika mashariki kabla hata wazungu hawana mpango huo lakini hawakuitawala east Africa zaidi ya kufanya biashara na kuondoka ila wazungu walitumia mabavu kutawala east Africa.

Huwezi tumia mabavu kwa Watu wenye Akili utapigwa.
Mabavu hutumika kwa Watu uliowazidi Akili na nguvu.

Hizo jamii zote zilizotumia mabavu zilikuwa na Akili.
Kumbuka jeshini kuna vifaa ambavyo ili uvitengeneze lazima uwe na Akili.
Sasa niambie ni utawala gani uliotawala pasipo kuwa na silaha.
Na ili uwe na silaha lazima akili ihusike.

Hao wachina unaowataja wanaweza kuwa na akili kwako au kwa jamii za chini yao lakini kidunia bado hawapo namba Moja mpaka tatu.

Utawala unahusisha Akili
 
Kwhyo brother ndio umeamua kutukandia kbs eeh! Bnafs ninaamini ulichoandka ingawa kuna mengne hapo nahtaj niyang'amue kwanza.
 
Huwezi tumia mabavu kwa Watu wenye Akili utapigwa.
Mabavu hutumika kwa Watu uliowazidi Akili na nguvu.

Hizo jamii zote zilizotumia mabavu zilikuwa na Akili.
Kumbuka jeshini kuna vifaa ambavyo ili uvitengeneze lazima uwe na Akili.
Sasa niambie ni utawala gani uliotawala pasipo kuwa na silaha.
Na ili uwe na silaha lazima akili ihusike.

Hao wachina unaowataja wanaweza kuwa na akili kwako au kwa jamii za chini yao lakini kidunia bado hawapo namba Moja mpaka tatu.

Utawala unahusisha Akili
Kwanza unapaswa ufahamu kila nchi,taifa, jamii ina taratibu zake za kiulinzi wengine sera zao za kiulinzi ni kijilinda tu sio kushambulia au kupora.

Turudi kwa wachina hiyo ya kusema hawana uwezo mkubwa wa akili ni kwa mujibu wako binafsi au kwa mujibu wa taifiti gani ?

Mimi nacho fahamu tafiti za kimataifa zimewataja watu wa Asia mashariki kama watu wenye akili nyingi kushinda jamii zote na hao ni wachina, wajapan na wakorea.

Unafahamu Chinese Civilization ? imeanza lini na ina miaka mingapi mpaka sasa ?
 
Kwanza unapaswa ufahamu kila nchi,taifa, jamii ina taratibu zake za kiulinzi wengine sera zao za kiulinzi ni kijilinda tu sio kushambulia au kupora.

Turudi kwa wachina hiyo ya kusema hawana uwezo mkubwa wa akili ni kwa mujibu wako binafsi au kwa mujibu wa taifiti gani ?

Mimi nacho fahamu tafiti za kimataifa zimewataja watu wa Asia mashariki kama watu wenye akili nyingi kushinda jamii zote na hao ni wachina, wajapan na wakorea.

Unafahamu Chinese Civilization ? imeanza lini na ina miaka mingapi mpaka sasa ?

Hata wewe unawezakuwa na akili kwa level ya familia yenu. Halikadhalika na Mimi.
Huyo China anaweza kuwa na akili kwa level ya jamii zao(Wachina, Wajapan, Wakorea) na ukanda wa Mashariki ya mbali . Lakini tukizungumzia Ulimwenguni hapo tunazungumzia habari nyingine kabisa.

Ni sawa useme Chadema inanguvu kisa umeenda Moshi au Arusha. Kitaifa Watu watakushangaa.

Hao Wachina hawana Rekodi yoyote ya maana katika mambo ya Akili na utawala ulimwenguni.
Labda kama unazungumzia habari za Future ambazo kwa sasa hazina maana yoyote.
 
Hata ule uwezo wa kutawala na kudhibiti hisia zako binafsi, unategemea kwa kiasi kikubwa, uwezo wako wa kusimamia , na kuelewa akili yako.

Watu wenye uwezo Bora, wa kudhibiti na kusimamia ( kutawala) hisia zao , mara nyingi wana uwezo wakufanya maamuzi bora, na kushughulikia changamoto katika njia bora zaidi.

Mtoa mada upo sahihi sana.
 
ANAYEKUTAWALA AMEKUZIDI AKILI

Anaandika, Robert Heriel.
Mtibeli.

Ukiona mtu amekuzidi na kukutawala kisiasa, kiuchumi, kijamii au kiteknolojia basi fahamu kabisa mtu au jamii hiyo imekuzidi Akili.

Akili ndio inayotawala mambo yote duniani. Ili upewe Mamlaka na nguvu basi lazima uwe na akili kuwashinda wengine hasa hao unaowatawala.

Kijinsia, Mwanaume anaakili kuliko Mwanamke ndio maana anamtawala. Ingawaje zipo siasa na porojo za kuwafariji wanawake kuwa wanaakili kuwashinda wanaume lakini kiuhalisia Mwanaume anaakili zaidi kuliko Mwanamke. Ndio maana Mwanaume anamtawala Mwanamke.

Kijamii, Wazungu na jamii zao wanaakili kushinda Waafrika, na Waarabu na wachina na jamii zingine. Ndio maana wazungu miaka nenda rudi wanatawala huu ulimwengu.

Kuna ile kujidanganya kuwa utawala ni majaliwa lakini hata hiyo akili yenyewe ni Majaliwa. Kila kitu kwenye maisha ni Majaliwa.

Wanyama wa porini tunawatawala kwa sababu ya sisi kuwashinda kiakili.
Huwezi tawala kitu ambacho kimekuzidi Akili hiyo haiwezekani na haitakuja kutokea.

Elewa kuwa wewe unaakili nyembamba au ndogo ndio maana unatawaliwa, na ndio maana wewe sio mtawala. Ingawaje unaweza na unaruhusiwa kujifariji kuwa umewazidi waliokutawala akili hiyo haibadilishi chochote kuwa wewe kiakili upo Chini.

Kama nitaulizwa ni kwa nini CCM mpaka leo inatawala mpaka leo basi moja kwa moja nitakuambia kuwa CCM inaakili kuliko vyama vingine. Yaani Watu wa ccm(inawezakuwa isiwe wote) wanaakili kuliko vyama vingine.
Haiwezekani kila mpambano na kila uchaguzi CCM ishinde tuu. Hiyo ni kuonyesha kuwa wanaakili kuwashinda wapinzani wao.

Watu wajinga hupenda kutoa visingizio katika kushindwa au pale wanaposhindwa na wenye Akili.
Sijui polisi, sijui wanatumia vyombo vya Dola, sasa kwa nini ninyi msitafute akili ya kupata ushawishi kwenye hivyo vyombo vya Dola kama mnajua kuwa kuna wakati ili mpate ushindi basi vyombo vya dola vinaweza kuwasaidia. AKILI.

Unakuta mtu anajiona anaakili kuliko Boss wake. Mpaka unamshangaa. Hiyo ni dalili ya kuchanganyikiwa. Huwezi kuwa na akili zaidi ya mtu ambaye amekuzidi na amekutawala katika uchumi alafu useme unamzidi akili za uchumi.

Kwenye Vita baina ya Israel na Palestina, watu wajinga na wenye upeo mdogo wanakataa kuwa Israel haina Akili na utawala wake unatokana na Kusaidiwa na Marekani. Yaani kama sio Marekani basi Israel haiiwezi Palestina na Waarabu. Unakuja kugundua kuwa wanaosema hivyo upeo wao upo chini katika kuyachambua mambo.

Hawajiulizi mbona Ukraine inasaidiwa na Marekani, na nchi za Nato lakini Inashindwa mbele ya Urusi. Hawajiulizi hivyo kwa sababu hawajui kuwa Akili ndogo haiwezi kuishinda akili kubwa.
Urusi ni akili kubwa hivyo inapokutana na Ukraine hapo ni lazima Ukraine ashindwe tuu bila kujali huyo Ukraine atasaidiwa na Marekani au Nato.

Wewe kama unajua ili ushinde unatakiwa ufanye moja mbili tatu. Kwa nini usifanye hizo moja mbili tatu.
Mshindani wako akikushinda unaleta visingizio.
Ooooh! Fulani kaenda kwa waganga wa kienyeji, sijui anauza madawa ya kulevya, ndio maana anapesa, pesa za wizi zile.
Hivi kwa ujinga wako unafikiri hata huo Wizi au kuuza madawa ya kulevya hakuhitaji AKILI?

Nenda nawe ukauze au kaibe ili ujue huyo mwenzako amekuzidi Akili na atakutawala kwa ufinyu wa akili yako.

Elewa kuwa Akili ni akili tuu. Bila kujali ni Akili ya uadilifu au akili ya uhalifu. Kutawaliwa ni kutawaliwa tuu iwe unatawaliwa kwa Haki au kwa haramu.

Jambo moja nalotaka kusema ni kuwa, ukishindwa kubali umeshindwa, kukubali kushindwa ni mwanzo wa kujitambua na unaweza kujua wapi pakuanzia.
Lakini kujifanya unauwezo wakati uwezo huo huna na kama ungekuwa nao usingeshindwa ni dalili ya kutojitambua.

Mimi nimemaliza,

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hilo la wanawake kutokutawala na kutokuwa na akili, nakupinga 100%

Mwanamme kwa ujinga wako hata nyumbani unajiona unatawala wewe, hujielewi kuwa kuna Malkia anaekutawala.

Watawala wa kiasili, iwe kwa Binadam, wanyama na hata wadudu ni wanawake.

Sijawahi kusikia kuna mtawala "mfalme" kwenye himaya zote nje ya binadam.

Binadam, mwanamme anajidai tu kuwa anatawala, kwa ujinga wake, lakinimtawala haswa ni mwanamke.

Kama unabisha soma biblia kisa cha Tamari alivyomzidi akili hata baba mkwe wake.

Soma Malkia wa Sheba alivyotawala.

Soma kuhusu kina Nfertiti, malikia wa Kufarao.

Soma chuo kikuu cha kwanza duniani kimeanzishwa na nani, utakuta ni Mwanamke.


Soma historia ya Somalia, walipokuwa na Malikia Fatma (Faduma) hawajawahi kutawaliwa, mpaka walipokuja kurithi wanaume, Somalia imekuwa janga.


Tazama Uingereza, si unaona miaka aliyotawala Malkia nchi ilivyotawala ulimwengu? Sasa tazama akiingia mwanamme itavyokuwa. Itakosa hata heshima inayopewa duniani.


Hakuna Mwanamme anayeweza kumzidi akili Mwanamke hata siku moja.++Basi hujasoma hata Alfu lela ulela?
 
Hata ule uwezo wa kutawala na kudhibiti hisia zako binafsi, unategemea kwa kiasi kikubwa, uwezo wako wa kusimamia , na kuelewa akili yako.

Watu wenye uwezo Bora, wa kudhibiti na kusimamia ( kutawala) hisia zao , mara nyingi wana uwezo wakufanya maamuzi bora, na kushughulikia changamoto katika njia bora zaidi.

Mtoa mada upo sahihi sana.

Ndio.
Kujidhibiti na kudhibiti wengine na mazingira ndio akili yenyewe
 
Hilo la wanawake kutokutawala na kutokuwa na akili, nakupinga 100%

Mwanamme kwa ujinga wako hata nyumbani unajiona unatawala wewe, hujielewi kuwa kuna Malkia anaekutawala.

Watawala wa kiasili, iwe kwa Binadam, wanyama na hata wadudu ni wanawake.

Sijawahi kusikia kuna mtawala "mfalme" kwenye himaya zote nje ya binadam.

Binadam, mwanamme anajidai tu kuwa anatawala, kwa ujinga wake, lakinimtawala haswa ni mwanamke.

Kama unabisha soma biblia kisa cha Tamari alivyomzidi akili hata baba mkwe wake.

Soma Malkia wa Sheba alivyotawala.

Soma kuhusu kina Nfertiti, malikia wa Kufarao.

Soma chuo kikuu cha kwanza duniani kimeanzishwa na nani, utakuta ni Mwanamke.


Soma historia ya Somalia, walipokuwa na Malikia Fatma (Faduma) hawajawahi kutawaliwa, mpaka walipokuja kurithi wanaume, Somalia imekuwa janga.


Tazama Uingereza, si unaona miaka aliyotawala Malkia nchi ilivyotawala ulimwengu? Sasa tazama akiingia mwanamme itavyokuwa. Itakosa hata heshima inayopewa duniani.


Hakuna Mwanamme anayeweza kumzidi akili Mwanamke hata siku moja.++Basi hujasoma hata Alfu lela ulela?

Nikujibu kwa upande wa Historia, dini au kisayansi?
 
Kwhyo brother ndio umeamua kutukandia kbs eeh! Bnafs ninaamini ulichoandka ingawa kuna mengne hapo nahtaj niyang'amue kwanza.

Hiyo inanihusu hata mimi Mkuu.
Huo ndio ukweli.
Mimi nikiona umenizidi kipato na tunarika sawa moja kwa moja na- appreciate kuwa umenizidi Akili Kwa eneo hilo. Kuhusu kufanya changes kukufikia au kukupita hiyo ni ishu nyingine
 
Back
Top Bottom