Anaweza kuwa Mtoto wako

Anaweza kuwa Mtoto wako

platozoom

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2012
Posts
9,548
Reaction score
11,517
Ni jioni ya leo nimekaa kwenye kibaraza na Laptop yangu. Mara anatokea mtoto wa kike umri miaka kama
nane hivi mtoto wa jirani yangu, anasoma darasa la tatu.

Akaniita "Uncle plato shikamoo, naomba laptop niangalie akaunti yangu ya facebook"! Kwanza sikuwa nafahamu kama ana facebook account lakini pia Sikuwa na kazi yeyote zaidi ya kuperuzi e-mail za kale....Nikamruhusu (kwa udadisi).

Akachakua na kufungua. Halafu baada ya kitambo nikamuuliza ana marafiki wangapi, akajibu 30! Halafu akaniambia unaona hili jina (kwenye akaunti yake), ni m-boy rafiki yangu. Huwa ananisumbua na last week nimemdanganya nimesafiri na baba kwenda Nairobi but he is so sturbon!. Nikamuuliza anakusumbua kivipi? akasema "nothing than charting"!

Sasa sijui kwa sababu ya utoto akanionyesha inbox yake:

Boy: Mambo
Mtoto: Shwari
Boy: Mbona umeadimika sana
Mtoto: Am around niko na dady tunaenda Coco beach
Boy: Umerudi lini kutoka nair
Mtoto: Wikend, badae nitakutafuta tuchati..bye mwaa
Boy: Poa, keep in touch!

Mtoto hakuwahi kufika Nairobi wala muda huo anasema alikuwa home ila anamdanganya tu. Inavyoonekana jamaa ana
umri mkubwa pengine wa Sekondari na naamini hawakuwahi kuonana. Nimepigwa na butwaa sikuwa na ushauri wa haraka.

Haya wananchi kizazi cha Mummy Daddy hicho!
 
Wazazi tuna michango mikubwa sana kwa yanayotokea kwa watoto wetu tuko bize kusaka shekeli na kulea kisasa.:tape2:
 
Wazazi tuna michango mikubwa sana kwa yanayotokea kwa watoto wetu tuko bize kusaka shekeli na kulea kisasa.:tape2:

Kuna jambo jingine nililiona kwa harakaharaka. Kwenye notification alikuwa na message kama 5, maana yake ni mwanachama active. Isitoshe kibaya zaidi alipoanza kunionyesha anachokifanya alikuwa ana requests za friendship
kama watu 5 na kwa haraka haraka akawa ana-accept (bila hata kuangalia profile ya huyo mtu), hilo kweli nilimkataza kwa kumwambia si sawa ku-accept kila mtu.

Na ana confidance kweli, hata password yake alikuwa anaweka kwa kujipinda nisiione!
usiyemjua
 
Idadi ya watoto kwenye FB ni kubwa, na kwa wenye watoto ninashauri wawe wanalimit watoto wao kwenye huo mtandao. coz kule hakuna mipaka, watoto wasio jua kuchambua jema na baya wanaharibikiwa, huyo akifika 15 itakuwaje?
 
Teknolojia ni kitu kizuri sana, lakini inapotokea watoto wakaamua kutumia teknolojia hizi bila uangalizi na angalizo mapema, matokeo yake ndiyo hayo unayoyaona sasa!
Kuna kila sababu ya wazazi kupata muda wa kukaa na watoto na kuwaeleza kinagaubaga lipi jema na lipi si jema kwenye ulimwengu huu tunaoishi sasa na hususan teknolojia, faida zake na hasara zake.
 
miaka nane? U cant be serious kwa kweli...

Unashangaa! Kwamba hawezi kutumia Internet au kuzungumza maneno kama hayo!
Chunguza watoto mtaani kwako utanipa jibu. They know a lot
 
Mkuu wangu platozoom,
Napata taabu kuamini hii habari....yaani katoto kana ka-boy kake ambako anakapiga fix zilizoenda skonga?! Tell me you're kidding!
 
Mkuu wangu platozoom,
Napata taabu kuamini hii habari....yaani katoto kana ka-boy kake ambako anakapiga fix zilizoenda skonga?! Tell me you're kidding!

NazDas na mimi nilishangaa sana. Kwanza anajua ile mikato yako yao ya kike. Halafu unashangaa hilo, Hiyo ni inbox moja
tu nyingine hakunifungulia. Na kulikuwa na marafiki zake watatu online hali inayoonyesha si wote watoto labda kama
siku hizi Wazazi wanawapa Computer watoto kama sehemu ya homework!

Ni hatari sana kwa sababu hata hao anawasiliana nao kuna wengine hawajaweka picha zao real, wanaweka za Superstars
na huwezi kujua huyo ni mtoto, mdada au fataki fulani tu. Kitu nachoweza kufanya labda kumshauri next time akitaka net, lakini kumkataza moja kwa moja wakati wazazi wanamruhusu kuperuzi haisaidii.
 
Nakuambia kama hali yenyewe ndiyo hii, tusubiri failures nyingi zaidi kwenye shule zetu!!!
 
Juzi nilikuwa kwenye internet cafe pembeni yangu kulikuwa na watoto wa wawili wa kiume miaka kama 10 au 11 wamefungua page mbili moja FB nyingine ponograph wakiona mtu anasogea wanaweka Fb kiukweli nilishindwa kusema kitu ila nina wafahamu na wazazi wao nitajaribu kusema nao maana tupo mtaa mmoja, sasa najiuliza walijuaje mitandao ya picha za ngono huu utandawazi. Utatumaliza

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Unafikir nimenyamaza mtani!
mamake ni mmojawa hao130 na comment zake saaasa!

Kudadeeki mzazi naye kumbeee....!
Kwa hiyo ukitaka kushauri unaanza na mzazi, ila jitayarishe, si mnasema mwanamke kusutwa suna!
 
Back
Top Bottom