gambakhuffu
JF-Expert Member
- Jul 2, 2010
- 509
- 547
Habari zenu wana bodi,
Kuna binti nilikuwa na date naye lakini hapa katikati ikatokea kutoelewana na isitoshe tupo ofisi moja, yote ni kwa sababu ya maneno yaliyoibuka ndipo akasema kuwa hataki mahusiàno na Mimi, lakini cha kushangaza haishi kunitumia jumbe mbali mbali kwenye mitandao ya kijamii hata kwenye simu. Na text zake zote zinafanana kama ilivyokuwa awali wkt bado uhusiano upo on peak.
Hapo mwanzo nimejaribu kumbembeleza arudishe roho nyuma ili tuendelee lakini amebaki kuwa na msimamo uleule na cha kushangaza text anazotuma ni hadi usiku wa manane.
Nashindwa kuelewa msimamo wa huyu binti na mara zote hapo nyuma alikuwa analazimisha nimvishe pete lakini sikuwa nimejipanga na amekuwa mdadisi kwa watu kwa kila hatua ninayopiga mbaya zaidi nikimchomekea turudiane anakuwa mbogo na ameanza hata kuniamkia kitu ambacho hakikuwa kawaida hapo kabla.
Hii hali imeniumiza sana kwani binti amebaki kuwa na msimamo tata na ukweli ni kwamba tulishibana sana hadi coworkers wakawa wanaona wivu na kwa hivi sasa imekuwa kama vile wanashangilia kuona love birds tumetengana.
Naomba ushauri wenu wana jamvi nifanye nini kuepukana na hii hali na labda nimweleze nini ili tuendelee kama zamani.
Nawasilisha!!
Kuna binti nilikuwa na date naye lakini hapa katikati ikatokea kutoelewana na isitoshe tupo ofisi moja, yote ni kwa sababu ya maneno yaliyoibuka ndipo akasema kuwa hataki mahusiàno na Mimi, lakini cha kushangaza haishi kunitumia jumbe mbali mbali kwenye mitandao ya kijamii hata kwenye simu. Na text zake zote zinafanana kama ilivyokuwa awali wkt bado uhusiano upo on peak.
Hapo mwanzo nimejaribu kumbembeleza arudishe roho nyuma ili tuendelee lakini amebaki kuwa na msimamo uleule na cha kushangaza text anazotuma ni hadi usiku wa manane.
Nashindwa kuelewa msimamo wa huyu binti na mara zote hapo nyuma alikuwa analazimisha nimvishe pete lakini sikuwa nimejipanga na amekuwa mdadisi kwa watu kwa kila hatua ninayopiga mbaya zaidi nikimchomekea turudiane anakuwa mbogo na ameanza hata kuniamkia kitu ambacho hakikuwa kawaida hapo kabla.
Hii hali imeniumiza sana kwani binti amebaki kuwa na msimamo tata na ukweli ni kwamba tulishibana sana hadi coworkers wakawa wanaona wivu na kwa hivi sasa imekuwa kama vile wanashangilia kuona love birds tumetengana.
Naomba ushauri wenu wana jamvi nifanye nini kuepukana na hii hali na labda nimweleze nini ili tuendelee kama zamani.
Nawasilisha!!
