Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,504
- 911,249
Adai kweli sijamtamkia, lakini ajua ninamtaka!
Adai macho yangu yanamchokoza, siju kivipi!
Adai nayo yanambipu, lakini yeye bado ni nguli!
Akiri sijamkonyeza, lakini macho yambembeleza!
Rafikize kawatonya, mimi ninamchemkia yeye!
Sijui ninachemka vipi, kwani sijalonga mie!
Kama kaandikiwa, mie kwake sina ujanja!
Itabidi nijisalimishe, hivyo awe na subira!
Kigori hasikii bali naye kunizulia majambo!
Rafikize kawatonya, mimi ninamchemkia yeye!
Ni kweli mtoto wa watu kaumbika lakini, Mmh!
Aaache domo kaya, kwani ananiaibisha mie!
Jicho halina pazia na nionacho nilete raha!
Lakini jicho kusisim'ka haimaanishi ni moyo!
Rafikize kawatonya, mimi ninamchemkia yeye!
N.B........................yatosha kwa leo!
Adai macho yangu yanamchokoza, siju kivipi!
Adai nayo yanambipu, lakini yeye bado ni nguli!
Akiri sijamkonyeza, lakini macho yambembeleza!
Rafikize kawatonya, mimi ninamchemkia yeye!
Sijui ninachemka vipi, kwani sijalonga mie!
Kama kaandikiwa, mie kwake sina ujanja!
Itabidi nijisalimishe, hivyo awe na subira!
Kigori hasikii bali naye kunizulia majambo!
Rafikize kawatonya, mimi ninamchemkia yeye!
Ni kweli mtoto wa watu kaumbika lakini, Mmh!
Aaache domo kaya, kwani ananiaibisha mie!
Jicho halina pazia na nionacho nilete raha!
Lakini jicho kusisim'ka haimaanishi ni moyo!
Rafikize kawatonya, mimi ninamchemkia yeye!
N.B........................yatosha kwa leo!