ichumu lya
JF-Expert Member
- Aug 11, 2016
- 2,649
- 2,795
CHANZO CHA UMASIKINI KAGERA KWA MAWAZO YANGU NI TOFAUTI NA WATAWALA WANAOWAZA KISIASA.
Kinachonisikitisha ni kwamba kila anayepanda jukwaa kuelezea kinachoitwa umaskini wa Mkoa wa Kagera anakuja na ngonjera za wingi wa maprofesa na Ma-PhD holders kutoka mkoani mwetu.
Lawama zote zinarundikwa kwa watu hao na Wanakagera kwa jumla. Huo ndio utawala wetu ambao tumezoea kwa miaka mingi sasa. Watawala wanajifanya kama hawajui chanzo halisi cha kile wanachokiita umasikini uliokithiri mkoani humo.
Bila tafakuri yoyote ya "tafiti" zinazodaiwa kufanywa na Serikali, wanakuja tu na porojo za jumlajumla kuhusu "umasikini" huo. Tafiti hizo za kimangumashi hazielezei chanzo cha tatizo la Mkoa wa Kagera. Haziangalii matokeo ya Vita vya Kagera na uharibifu wa usalama na miundombinu uliosababishwa na ugomvi wa Serikali na Iddi Amin.
Kwamba shughuli za uzalishaji na kiuchumi zilikufa kabisa kutokana na vita hiyo. Hawaoni kwamba Serikali ilikosea (kwa makusudi) kutotangazwa kwa hali ya hatari mkoani humo, kwa maana ya kujenga miundombinu upya na kuwasaidia Wanakagera kurudia maisha yao ya kabla ya vita. Hawasemi Serikali ilifunga mpaka na Uganda, hivyo kusitisha shughuli zote za kiuchumi, ambapo soko kuu la mkoa wa Kagera lilikuwa Uganda.
Baada ya vita Ukimwi uliotokea Uganda ulimaliza nguvukazi kubwa ya mkoa huo kwa kupuputisha maisha ya maelfu ya nguvukazi wa Kagera. Wanajifanya hawajui kwamba MV.
Bukoba ilizama na kuua mamia ya watu, wengi wao wakiwa Wanakagera. Hapohapo, MV. Victoria "iliharibika" na kufanya Wanakagera kukosa kabisa usafiri wa kuwaunganisha na nchi yao, huku mazao yao ya kiuchumi yakishindwa kusafirishwa kwenda kwenye masoko makubwa ya kibiashara ya hapa nchini kama Mwanza na Dar es Salaam.
Serikali haikuona umuhimu wa kuwapa Wanakagera vyombo vingine vya usafiri ili wajimudu kiuchumi. Ndipo pia ulipoingia "Ugonjwa wa Mnyauko" wa migomba uliopigilia msumari wa mateso na umasikini wa Wanakagera. Yapata sasa zaidi ya miaka 15. Je, Serikali ilichukua hatua gani kuwasaidia wakulima wa kilimo cha migomba mkoani Kagera? HAKUNA.
Wakati huohuo Wanakagera walikatazwa kuuza kahawa yao nchini Uganda ambako walikuwa wanapata bei nzuri kulingana na gharama za uzalishaji.
Waliopatikana na uvushaji wa zao hilo waliadhibiwa, ikiwemo vifungo au kufilisiwa, huko kahawa ikilimbikiziwa "TOZO" lukuki bila kutilia maanani gharama za wakulima za uzalishaji.
Wanasahau tetemeko la ardhi ambapo serikali haikusaidia chochote badala yake serikali ilisema nyumba wamezisukuma wenyewe wafe maana majanga makubwa yote uanzia Kagera kama UKIMWI na majanga mwngine makubwa hakuana msaada uliotolewa mbali na kunyang'anywa kidogo kilichopatika na kuzuia waliokuwa tayari kusaidia ndugu zao kuzuiwa kwa kile serikali ilichosema kuwa vitu vyote vikusanywe kwenye mfuko wa mkoa pale Boari lakini vile vitu viliyeyuka na wananchi kuambulia biskuti mpaka sasa watu wengi wanaishi kwenye turubai.
Kwa kagera kama ambavyo imekuwa ikifanya kwa baadhi ya mikoa ambayo iliwahi kupata majanga kama mafuriko, njaa nk.
Leo hii tunashuhudia jitihada za serikali kuhamisha watu kutoka kwenye hifadhi nakupelekwa kwenye kijiji ambacho imewaadalia wanakuta kila kitu sembuse wanakagera ambao walipata janga la tetemeko na serikali haikujali wala haikujiusisha kabisa na jambo hilo bali ilikuwa ni kuwazuia hata waliokuwa tayari kusaidia.
Hiyo ni mifano michache tu ya hujuma ya Serikali dhidi ya Mkoa wa Kagera kwa miongo mingi sasa. Matokeo yake ni nini? Wananchi wa Mkoa wa wa Kagera waliona Serikali ilikuwa haiwataki, haiwapendi. Wakasema isiwe taabu, wakaamua kuhamia mikoa nyingine nchini na kuwekeza huko.
Je Serikali inajifanya haioni uwekezaji wao mkubwa na uliotukuka katika mikoa mingine nchini, ikiwemo Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na kwingineko?
Serikali imekuwa ikipiga kelele nyingi eti Wahaya wameshindwa kujenga soko na kituo cha mabasi mjini Bukoba, ikijifanya haijui kwamba jukumu hilo ni lake na vyombo vyake, ikiwemo TAMISEMI.
Kwani vituo vya mabasi na masoko ya Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam, Mwanza na kwingineko vimejengwa na nani kama sio Serikali?
Nimalizie kwa kuishauri Serikali kwamba iwekeze mkoani Kagera kama ambavyo imekuwa ikiwekeza sehemu nyingine nchini. Ikiwekeza Kagera, kama ambavyo Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imepanga kufanya kwa kujenga kitengo cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), mkoani humo, basi itarajie kwamba maprofesa na PhD holders kutoka mkoani Kagera watarudi nyumbani kufaidi fursa za uwekezaji wa Serikali.
Ni matumaini ya wengi mkoani Kagera kwamba Mkuu mpya wa Mkoa wa kagera, Mhe. Chalamila ataelewa chanzo cha "UMASIKINI WA MKOA WA KAGERA".
Kwani ni mnataka wanakagera tujenge stendi na soko?
Kwani WASOMI mnaosema ni watumishi wa serikali? Wanakusanya kodi gani? Maeneo mnakopeleka miradi ya maendeleo kama stendi, soko na vyuo vikuu hakuna wasomi? Kigezo icho nichakikatiba?
Mwanza imejengwa viwanda kwakuwa hakuna wasomi? Arusha, Dodoma, Mbeya, Dar Es Salaam nk. Hakuna wasomi?
Mwambie Mkuu wa mkoa awaeleze ukweli wanaKagera kuwa umasikini na utapia mlo wanaousema Kagera ni mradi wa CCM ili waendelee kutawala.
Najua hamna majibu inawezekana mkanifungulia kesi nyingine kwakuwa nimesema ukweli mimi ni Muhaya na mzalendo wa Kagera nachukia unafiki na Majungu
Serikali timiza wajibu wenu acha kurukaruka kama maharage sufuriani.
Kinachonisikitisha ni kwamba kila anayepanda jukwaa kuelezea kinachoitwa umaskini wa Mkoa wa Kagera anakuja na ngonjera za wingi wa maprofesa na Ma-PhD holders kutoka mkoani mwetu.
Lawama zote zinarundikwa kwa watu hao na Wanakagera kwa jumla. Huo ndio utawala wetu ambao tumezoea kwa miaka mingi sasa. Watawala wanajifanya kama hawajui chanzo halisi cha kile wanachokiita umasikini uliokithiri mkoani humo.
Bila tafakuri yoyote ya "tafiti" zinazodaiwa kufanywa na Serikali, wanakuja tu na porojo za jumlajumla kuhusu "umasikini" huo. Tafiti hizo za kimangumashi hazielezei chanzo cha tatizo la Mkoa wa Kagera. Haziangalii matokeo ya Vita vya Kagera na uharibifu wa usalama na miundombinu uliosababishwa na ugomvi wa Serikali na Iddi Amin.
Kwamba shughuli za uzalishaji na kiuchumi zilikufa kabisa kutokana na vita hiyo. Hawaoni kwamba Serikali ilikosea (kwa makusudi) kutotangazwa kwa hali ya hatari mkoani humo, kwa maana ya kujenga miundombinu upya na kuwasaidia Wanakagera kurudia maisha yao ya kabla ya vita. Hawasemi Serikali ilifunga mpaka na Uganda, hivyo kusitisha shughuli zote za kiuchumi, ambapo soko kuu la mkoa wa Kagera lilikuwa Uganda.
Baada ya vita Ukimwi uliotokea Uganda ulimaliza nguvukazi kubwa ya mkoa huo kwa kupuputisha maisha ya maelfu ya nguvukazi wa Kagera. Wanajifanya hawajui kwamba MV.
Bukoba ilizama na kuua mamia ya watu, wengi wao wakiwa Wanakagera. Hapohapo, MV. Victoria "iliharibika" na kufanya Wanakagera kukosa kabisa usafiri wa kuwaunganisha na nchi yao, huku mazao yao ya kiuchumi yakishindwa kusafirishwa kwenda kwenye masoko makubwa ya kibiashara ya hapa nchini kama Mwanza na Dar es Salaam.
Serikali haikuona umuhimu wa kuwapa Wanakagera vyombo vingine vya usafiri ili wajimudu kiuchumi. Ndipo pia ulipoingia "Ugonjwa wa Mnyauko" wa migomba uliopigilia msumari wa mateso na umasikini wa Wanakagera. Yapata sasa zaidi ya miaka 15. Je, Serikali ilichukua hatua gani kuwasaidia wakulima wa kilimo cha migomba mkoani Kagera? HAKUNA.
Wakati huohuo Wanakagera walikatazwa kuuza kahawa yao nchini Uganda ambako walikuwa wanapata bei nzuri kulingana na gharama za uzalishaji.
Waliopatikana na uvushaji wa zao hilo waliadhibiwa, ikiwemo vifungo au kufilisiwa, huko kahawa ikilimbikiziwa "TOZO" lukuki bila kutilia maanani gharama za wakulima za uzalishaji.
Wanasahau tetemeko la ardhi ambapo serikali haikusaidia chochote badala yake serikali ilisema nyumba wamezisukuma wenyewe wafe maana majanga makubwa yote uanzia Kagera kama UKIMWI na majanga mwngine makubwa hakuana msaada uliotolewa mbali na kunyang'anywa kidogo kilichopatika na kuzuia waliokuwa tayari kusaidia ndugu zao kuzuiwa kwa kile serikali ilichosema kuwa vitu vyote vikusanywe kwenye mfuko wa mkoa pale Boari lakini vile vitu viliyeyuka na wananchi kuambulia biskuti mpaka sasa watu wengi wanaishi kwenye turubai.
Kwa kagera kama ambavyo imekuwa ikifanya kwa baadhi ya mikoa ambayo iliwahi kupata majanga kama mafuriko, njaa nk.
Leo hii tunashuhudia jitihada za serikali kuhamisha watu kutoka kwenye hifadhi nakupelekwa kwenye kijiji ambacho imewaadalia wanakuta kila kitu sembuse wanakagera ambao walipata janga la tetemeko na serikali haikujali wala haikujiusisha kabisa na jambo hilo bali ilikuwa ni kuwazuia hata waliokuwa tayari kusaidia.
Hiyo ni mifano michache tu ya hujuma ya Serikali dhidi ya Mkoa wa Kagera kwa miongo mingi sasa. Matokeo yake ni nini? Wananchi wa Mkoa wa wa Kagera waliona Serikali ilikuwa haiwataki, haiwapendi. Wakasema isiwe taabu, wakaamua kuhamia mikoa nyingine nchini na kuwekeza huko.
Je Serikali inajifanya haioni uwekezaji wao mkubwa na uliotukuka katika mikoa mingine nchini, ikiwemo Dar es Salaam, Mwanza, Arusha na kwingineko?
Serikali imekuwa ikipiga kelele nyingi eti Wahaya wameshindwa kujenga soko na kituo cha mabasi mjini Bukoba, ikijifanya haijui kwamba jukumu hilo ni lake na vyombo vyake, ikiwemo TAMISEMI.
Kwani vituo vya mabasi na masoko ya Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam, Mwanza na kwingineko vimejengwa na nani kama sio Serikali?
Nimalizie kwa kuishauri Serikali kwamba iwekeze mkoani Kagera kama ambavyo imekuwa ikiwekeza sehemu nyingine nchini. Ikiwekeza Kagera, kama ambavyo Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imepanga kufanya kwa kujenga kitengo cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), mkoani humo, basi itarajie kwamba maprofesa na PhD holders kutoka mkoani Kagera watarudi nyumbani kufaidi fursa za uwekezaji wa Serikali.
Ni matumaini ya wengi mkoani Kagera kwamba Mkuu mpya wa Mkoa wa kagera, Mhe. Chalamila ataelewa chanzo cha "UMASIKINI WA MKOA WA KAGERA".
Kwani ni mnataka wanakagera tujenge stendi na soko?
Kwani WASOMI mnaosema ni watumishi wa serikali? Wanakusanya kodi gani? Maeneo mnakopeleka miradi ya maendeleo kama stendi, soko na vyuo vikuu hakuna wasomi? Kigezo icho nichakikatiba?
Mwanza imejengwa viwanda kwakuwa hakuna wasomi? Arusha, Dodoma, Mbeya, Dar Es Salaam nk. Hakuna wasomi?
Mwambie Mkuu wa mkoa awaeleze ukweli wanaKagera kuwa umasikini na utapia mlo wanaousema Kagera ni mradi wa CCM ili waendelee kutawala.
Najua hamna majibu inawezekana mkanifungulia kesi nyingine kwakuwa nimesema ukweli mimi ni Muhaya na mzalendo wa Kagera nachukia unafiki na Majungu
Serikali timiza wajibu wenu acha kurukaruka kama maharage sufuriani.
Aliyesoma hiyo habari anifanyie summarization... All in all Kagera imejaa uchawi uvivu na ubaguzi vyote hivi husababisha Umasikini mkubwa ktk mkoa huo... Ndio maana huwez kukutana na Muhaya tajiri...
