Katika hiyo Mihimili yote tunaomba utuoneshe na uanishe hayo Matusi..
Binafsi nimesha shuhudia walio mtukana Raisi wakipandishwa Mahakamani lkn katika Makosa yao sijawahi kuona kumtukana Raisi kukawa ni Uhaini.
Sheria ya Uhaini. Na.2 ya 1970 Jedwali
SURA YA SABA
UHAINI NA MAKOSA MENGINE DHIDI YA SERIKALI
39.-(1) Mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano
(a) akiwa ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, anamuua au anajaribu kumuua Rais; au
(b) akiwa ndani ya Jamhuri ya Muungano anaanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano,
atakuwa na hatia ya kosa la uhaini na atawajibika kwa adhabu ya kifo.
(2) Mtu yeyote ambaye, yumo katika ndani ya Jamhuri ya Muungano, akiwa ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, anajenga nia kusababisha au kuwezesha kusababishwa, au anajenga nia ya kuchochea, anashawishi, shauri au kuusia mtu yeyote au kikundi cha watu kusababisha au kuwezesha kusababishwa yoyote kati ya matendo au malengo
yafuatayo, yaani:-
(a) kifo, kumlemaza au kumjeruhi, au kufungwa au kumzuia,
Rais;
(b) kumwondoa Rais madarakani isivyo halali kutoka katika
wadhifa wake wa Urais au kumwondolea ufahari, heshima na jina la Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Jamhuri ya Muungano;
(c) kupindua kwa njia zisizo halali, Serikali ya Jamhuri ya Muungano; au
(d) kutishia Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Bunge na Mahakama ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano,
na kubainisha nia hiyo kwa kuchapisha maandishi or machapisho au kwa kitendo chochote cha siri kinachojionyesha cha hali yoyote, atakuwa na hatia ya kosa na atawajibika kwa adhabu ya kifo.
(3) Mtu yeyote ambaye, yumo katika utii wa Jamhuri ya Muungano–
(a) aliye na mshikamno na maadui wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au anawapa msaada au hifadhi ndani ya Jamhuri ya Muungano au kwingineko;
(b) anachochea, aidha ndani ya Jamhuri ya Muungano au kwingineko, mtu yeyote aivamie Jamhuri ya Muungano kwa kutumia jeshi; au
(c) anabeba silaha ndani ya Jamhuri ya Muungano kwa amri, kwa nia ya kutumia nguvu ya kuizuia, kuilazimisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano kubadilisha vigezo au ushawishi wake, au kwa nia ya kulazimisha au kuzuia au kutishia, Serikali ya Jamhuri ya Muungano,
atakuwa na hatia ya kosa la uhaini na atawajibika kwa adhabu ya kifo.