DERICK2000
JF-Expert Member
- Apr 8, 2012
- 203
- 35
Ananipenda sana,ila anawivu mno mpaka ananiudhi..Dawa yake ni nini wana mmu?.nataka anipende kiasi..
Hujasomeka bado....Ananipenda sana,ila anawivu mno mpaka ananiudhi..Dawa yake ni nini wana mmu?.nataka anipende kiasi..
Loh asaraa yako! Umepewa nyama ukanyimwa meno......Ananipenda sana,ila anawivu mno mpaka ananiudhi..Dawa yake ni nini wana mmu?.nataka anipende kiasi..
Mwache .ataacha kukupenda sana na atakusahau then utakua huru.
Dah umemjibu vizuri sana, ninachoamini wivu ni ngao ya mapenzi, mara nyingi watu wenye vidumu huwa hawapendi waonewe wivu, Wivu ni kipimo cha mapenzi... Wanaume wengine bwana, eti anawivu mpaka ananikera, khaaaaaa.. !!! Kweli anakukera mtoto wa watu? Ulitaka awe anakaa kimya ili uhisi kuwa hupendwi? Mapenzi hayako hivyo, "ukiamua kuolewa usiogope kulala uchi".. Na wewe ukimpenda kikweli YEYE PEKEYAKE na wewe utakua ktk viatu vyake tu, ukimshindwa sana nikaPM namba zake..
Ananipenda sana,ila anawivu mno mpaka ananiudhi..Dawa yake ni nini wana mmu?.nataka anipende kiasi..
Wivu ukizidi ni KERO na laweza kuwa tatizo la kisaikolojia kwahiyo usitake watu wavumilie kero eti kuwa ndio mapenzi. Hata wasio na mapenzi ya kutosha wanaweza kuonyesha wivu kwasababu ya kupenda KUMILIKI wenzao iwe wanawapenda au hawawapendi.
Wivu ukizidi ni KERO na laweza kuwa tatizo la kisaikolojia kwahiyo usitake watu wavumilie kero eti kuwa ndio mapenzi. Hata wasio na mapenzi ya kutosha wanaweza kuonyesha wivu kwasababu ya kupenda KUMILIKI wenzao iwe wanawapenda au hawawapendi.
Dawa ya mtu mwenye wivu ni kufanya vile anavyotaka ili umridhishe,tatizo linakuwa kama wewe haujampenda kihivyo lazima akunyime raha na kama hapo ndio umefika we yatimize tu na utaona sio kero bali raha ya ajabu.Ila umeniboa hapo unaposema unataka akupende kiasi ina maana wewe hauko serious na kitu kinachoitwa mapenzi bali ni wale onjaonja.Ananipenda sana,ila anawivu mno mpaka ananiudhi..Dawa yake ni nini wana mmu?.nataka anipende kiasi..