Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,701
- 9,779
Dah, inasikitisha sana ndugu zanguni. Mke aambulia kipigo kitakatifu kilichosheheni ngumi, banzi jiwe kama alilokumbana nalo yule mwombolezaji wa Mh. Lowasa pale Ngarenaro, mikanda ya rasha rasha na ngumi peresu peresu usiku wa kuamkia jana.
Hii ni baada ya mumewe kugundua kuwa mkewe pamoja na wanae watatu wa kike akiwemo binti wa miaka 12 wanachezeshwa mchezo wa kukusanya pesa kwa pamoja kisha mmoja wao hupokea maokoto ndani ya wiki
Pesa yenyewe ni Tsh. 500 kwa siku, hivyo wote wanne kwa pamoja (akiwemo mama) hutengeneza kitita cha Tsh.14,000 ndani ya wiki
Mwanaume huyo alisikika akilaumu eti mwanamke anawafundisha pesa watoto wake angali wadogo, hivyo kuwafanya wawe na tamaa. Anatafuta pesa ili wanae wakifika shuleni watumie kwa kujivinjari, badala yake watoto wanawasilisha pesa hizo kwa mama yao mzazi na kwenda shuleni na 300, 300. Aliendelea kwa kusema kuwa amewahi kumkataza tabia hii ya kucheza michezo mkewe miaka mitatu iliyopita.
Mke aliadhibiwa mbele ya watoto ili wao wajifunze kuwa michezo hiyo ya pesa ya kinamama ni hatari kwa maisha yao. Hivyo wasije jaribu katika maisha yao. Kwamba Samaki mkunje angali mbichi
Je, alichofanya ni sahihi, ama tumlambe bakora?
Hii ni baada ya mumewe kugundua kuwa mkewe pamoja na wanae watatu wa kike akiwemo binti wa miaka 12 wanachezeshwa mchezo wa kukusanya pesa kwa pamoja kisha mmoja wao hupokea maokoto ndani ya wiki
Pesa yenyewe ni Tsh. 500 kwa siku, hivyo wote wanne kwa pamoja (akiwemo mama) hutengeneza kitita cha Tsh.14,000 ndani ya wiki
Mwanaume huyo alisikika akilaumu eti mwanamke anawafundisha pesa watoto wake angali wadogo, hivyo kuwafanya wawe na tamaa. Anatafuta pesa ili wanae wakifika shuleni watumie kwa kujivinjari, badala yake watoto wanawasilisha pesa hizo kwa mama yao mzazi na kwenda shuleni na 300, 300. Aliendelea kwa kusema kuwa amewahi kumkataza tabia hii ya kucheza michezo mkewe miaka mitatu iliyopita.
Mke aliadhibiwa mbele ya watoto ili wao wajifunze kuwa michezo hiyo ya pesa ya kinamama ni hatari kwa maisha yao. Hivyo wasije jaribu katika maisha yao. Kwamba Samaki mkunje angali mbichi
Je, alichofanya ni sahihi, ama tumlambe bakora?