Amos Makalla: Wanafunzi wa Mbeya Day, wana nidhamu mbovu,Wanavuta bangi, Walimu karibuni Mbeya

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla, amesema nidhamu ya Wanafunzi MBEYA DAY ni mbovu, wakati mwingine wanatoka nje ya darasa Mwalimu akiingia'. Wanaenda kuvutia bangi kule shule ya Msingi Azimio na wakifika huko wanafanya vurugu.

"Sisi kama Serikali tumezama na tunauthibitishia Umma kwamba nidhamu ya wanafunzi wa Mbeya Day katika kidato cha tatu na cha nne ni ya hali ya chini sana. Katika darasa la wanafunzi 50 inaweza ikatokea Mwalimu akafundisha watoto kumi na wengine wanatoka wanapishana na Mwalimu na hawafanyi kitu chochote. Kuna vijana ambao wamekinga ngumi wanataka kupigana na walimu na Walimu wanaona isiwe tabu.

Sasa lazima tufike mahali mimi kama Mzazi na Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama lazima nione kwamba walimu wanatimiza wajibu wao lakini na watoto wetu wawe na malezi ya kuamini kwamba Mwalimu ni mtu ambaye ni kama mzazi wake anampa Elimu, lakini muda mwingi hatukai na hawa watoto kwa Malezi Mazuri.

Kwahiyo niwahakikishie tukio hili limetokea na halitatokea tena lakini pia niwatoe hofu kwamba wanafunzi walimu wanaokuja kwenye Mafunzo waje. Na miminitaendelea kuziangalia shule zote zenye watoto wakorofi kudeal nao kuwarejesha katika nidhamu nzuri wapate malezi na walimu wale watimize wajibu wao.

Hivi karibuni Walimu wa Mafunzo katika Shule ya Mbeya Day walifukuza kazi kazi kwa kile kilichodaiwa ni Video iliyosambaa ikionesha walimu hao wakiwapa adhabu wanafunzi bila kufuata utaratibu.


Habari hiyo ya Mwanafunzi kupigwa, ipo kwenye hii thread=>MBEYA: Walimu warekodiwa Video, wakimfanyia unyama Mwanafunzi
 
Mkuu wa mkoa Mbeya Mhe. Amos Makalla, anasema nidhamu ya Wanafunzi MBEYA DAY ni mbovu, wakati mwingine wanatoka nje ya darasa Mwalimu akiingia'.

"Sisi kama Serikali tumezama na tunauthibitishia Umma kwamba, nidhamu ya Wanafunzi wa Mbeya Day katika kidato cha tatu na cha nne ni ya hali ya chini sana. Katika darasa la wanafunzi Hamsini, inaweza ikatokea Mwalimu akafundisha watoto kumi tu"
huyu mkuu wa mkoa jembe sana mwanafunzi anazingua sometimes
 
Sawa lkn kipigo km kile syo
Hujawahi kukutana na mianafunzi hamnazo mkuu. Wengine tumeangalia matokeo badala ya chanzo. I believe, hadi kufikia hatua ile yule mwanafunzi atakuwa alionesha utovu wa nidhamu wa hali ya juu; siamini ilikuwa ni siku ile tu bali "ni kawaida yake". Wale walimu ni binadamu pia tena wasomi sio rahisi kuchukia kiasi kile bila kufanyiwa maudhi "ya kutosha". Mbona wanafunzi wengi tu walikuwa hawajafanya homework lakini adhabu yao ilikuwa ya kawaida?
 
Mkuu wa mkoa Mbeya Mhe. Amos Makalla, anasema nidhamu ya Wanafunzi MBEYA DAY ni mbovu, wakati mwingine wanatoka nje ya darasa Mwalimu akiingia'.

"Sisi kama Serikali tumezama na tunauthibitishia Umma kwamba, nidhamu ya Wanafunzi wa Mbeya Day katika kidato cha tatu na cha nne ni ya hali ya chini sana. Katika darasa la wanafunzi Hamsini, inaweza ikatokea Mwalimu akafundisha watoto kumi tu"

Kutokana na hiyo sentensi kuna maswali ya kujibu hapa

1. Je nidhamu ya wanafunzi kidato cha kwanza na pili ni nzuri?

2. Kama swali la kwanza jibu ni ndio, inamaana hawa watoto nidhamu yao inashuka wakiwa shule. Wao kama walimu ambao ni walezi mbadala wanafunzi wakiwa shule wamechukua hatua gani kudhibiti hilo?

3. Na kama jibu ni hapana, inamaana shule nzima ina wanafuzi wenye nidhamu mbovu, hivyo walimu watakuwa hawafanyi kazi zao, wanaweza sema malezi ya wazazi ni mabaya. Lakini pia wamewashirikisha vipi wazazi kwenye kuweka sawa swala hili?
 
Na tulihabarishwa yule aliyepata kipigo hakuwepo shule sijui kwa siku ngapi halafu anaulizwa badala ya kuwa mpole analeta jeuri. Tunajenga taifa la namna gani?
Nidham ifuate mkondo
 
MImi nilisema; HASALA ILIYO IPATA SERIKALI KWA KUWAFUKUZA WALE WALIMU, NI KUBWA KULIKO HATA YA KUMTETEA YULE MTOTO! simaanishi naunga mkono watoto wapigwe la hasha! Lakini pale palihitahi kuonyana tu kinidhamu! Gharama ya serikali iliyowekeza Kwa wale walimu ni kubwa kuriko huyo mtoto JEURi;
 
Back
Top Bottom