Amenibebea mimba bila ridhaa yangu

Amenibebea mimba bila ridhaa yangu

caxton

Senior Member
Joined
May 8, 2015
Posts
145
Reaction score
157
Wana Jf nawasalim,

Nina mpenzi wangu mpya ambae amehamia kwangu katika mazingira ambayo yanatatanisha hadi sasa na hatimae kubeba mimba bila ridhaa yangu.Huyu binti tumefahamiana miezi si mingi, ni business woman anakwenda Arabuni kufuata mizigo mbalimbali, mimi ni HR business partner.

Alianza mtindo wa kuja kwangu Friday na kuondoka Sunday aliendelea kuongeza siku hadi akahamia kwangu mazima..
Juzi jumamosi kaniambia hazioni siku zake, na wiki yote hii amekua kama mgonjwa.

Tulipoenda hospital tukaambiwa ni mjamzito, tuliporudi home nikamuuliza nani kakutuma ubebe mimba wakati bado tunachunguzana? Je matokeo ya kuchunguzana yakija negative? Utamlaumu nani?

Anadai hajui imekuaje hadi kabeba mimba ina maana mwanamke wa miaka 27 hajui mzunguko wake upoje?
Alipolazimisha kuja kuishi kwangu alidai sababu kuu ni kujuana tabia, then taratibu zingine zifuate.

Sasa mbona anaruka hatua kwa kunitegeshea mimba?Halafu anadai niende kujitambulidha kwao, kwa hiyo ni mbinu au?
Seriously mimi bado nahitaji kuendelea kumchunguza kuna vitu bado navifuatilia kumhusu yeye.

Mfano hizo safari za Arabuni na Hong Kong bado sijazielewa kwa kina naendelea kuzichunguza, sasa kwa hali hii mtu unafanyaje? Mawazo yenu please

Tatizo la pill ni hobby zetu kuwa tofauti kwa mfano yeye anapenda sana kwenda kwenye bendi za dansi kama twanga na Fm Academia wakati mimi miziki hiyo naiona ni makelele na tukienda wote huko mimi nakua bored ile mbaya.

Na kila weekend anataka twende, anajua ratiba za mabendi yote makubwa, mm kwa upande wangu napenda kwenda sehemu tulivu zenye mziki laini kwa mbali, hata kama ni bendi iwe ni karaoke na sio makelele ya akina FM academia ambapo huwezi hata kuongea na jirani yako.

Hivi karibuni, tulienda bendi, masikio yangu yaliziba wiki nzima huku nikisikia miluzi kama nimekunywa ile dawa ya zamani ya quinine je, kama tunaendelea kuishi pamoja je hili haliwezi kuwa kikwazo?

Yeye akibadilisha sana ni kwa kina mzee Yusuph ambako hata kwa kunifunga minyororo hujanipeleka, huwa namruhusu anaenda na ndugu na rafiki zake.

Your help please

Unaweza kujibu swali unalodhani unaliweza kati ya hayo mawili

Thanx
 
kumbe kuchunguzana mpaka mnajigijigi...safi sana we hapo oa tu.. ukimaliza uchunguzi wako mtarekebishana maisha yanaendelea
 
pole sana ndugu yangu ,lakini mimi nakulaumu wewe inakuwaje ukubali kuishi na mchumba wako NDANI KABLA HATA HAMJAFANYA TARATIBU ZOZTE ? swali la pili kwanini uliendelea kushiriki tendo la ndoa bila kinga yeyote ? je umeshaenda kufanya vipimo kujua afya zenu? nakushauri uende hospitali mkapate ushauri nasaha na kufanya vipimo, baadhi ya vipomo ni HIV VDRL,BLOOD GROUP & RHESUS FACTOR, SICKLE DISEASES,HEPATIS B
 
Hapo pa kuhamia ndani ndipo ulipokiuka kanuni za ''probation period'' ya mapenzi. Kuchunguzana kunafanyikaga kabla hamjaamua kukaa kinyumba,mzigo ukishaingia ndani maana yake ushakuwa certified kwa matumizi ya muda mrefu.Hiyo ni implied move haina haja ya kuambiana.Na wanawake wanajua hii mbinu vilivyo akiingia ndani kwako its a wrap.

Kwa hiyo cha msingi endelea na hatua stahiki kama kujitambulisha,kulipa faini ya kufungua mzigo kabla ya kupata ridhaa ya wazazi(if applicable) nk. Wanadamu huwa tunajifunza kutokana na makosa na makosa yenyewe ndio kama hili. Just be a man and face the music. Wish you a very prosperous life with your new partner.
 
Alianza mtindo wa kuja kwangu Friday na kuondoka Sunday aliendelea kuongeza siku hadi akahamia kwangu mazima..

Juzi jumamosi kaniambia hazioni siku zake, na wiki yote hii amekua kama mgonjwa tulipoenda hospital tukaambiwa ni mjamzito, tuliporudi home nikamuuliza nani kakutuma ubebe mimba wakati bado tunachunguzana? Je matokeo ya kuchunguzana yakija negative? Utamlaumu nani?
Anadai hajui imekuaje hadi kabeba mimba
Ina maana mwanamke wa miaka 27 hajui mzunguko wake upoje?


images


No disrespect, but that's got to be the dumbest question i ever heard.

​​
 
caxton

Una akili kweli? Kwa nini kumchunguza akiwa kwako na mkizini? Hicho unachochunguza ni nini. Yaani kwa nini uharibu mtoto wa watu halafu ndo uombe ushauri. Katibu na ufunge ndoa.
 
Last edited by a moderator:
You are a man....man up

kwanza we ndo mwnye makosa unakubali vp mtu mnayechunguzana naye aje aishi kwako?...anyway 2fanye ulikosea cha mcng kwa sasa ni vigumu kumtimua fanya kuendelea kumchunguza lkn pia usiwe na haraka ya kwnd kujitambulisha
 
Kwenye hobby hapo hapana maana yeyote.
Ukishaingia kwenye ndoa hobby zingine hupungua au kutoweka kabisa automatically!
 
Kwa muktadha huuina maana hata ngono zembe ulifanya bila ridhaa eti?
 
Back
Top Bottom