Amekosa ada, anataka kuishia certificate

Amekosa ada, anataka kuishia certificate

Promethazine

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2017
Posts
262
Reaction score
260
Wakuu za asubuhi, niende moja kwa kwenye mada.

Kuna rafiki yangu anayesoma Diploma in nursing mwaka wa pili sasa kanielezea hali ifuatayo.

Aliamua kusoma Diploma hiyo baada ya wazazi wake kuweka uhakika wa kumsomesha, kweli walimsomesha mwaka wa kwanza ukaisha, changamoto imekuja kwenye ada mwaka wa pili, yaani wazazi wamekosa ada kabisa hapo alipo kaniambia anawaza kuishia certificate kwa sababu anahisi akizidi kuendelea deni litakuwa kubwa na atazuiliwa kufanya mtihani

Chuo huwa kina utaratibu wa kuzuia wanafunzi wenye madeni makubwa kutokufanya mitihani ya mwisho, hivyo kaona bora aishie certificate isije kumtokea hiyo akiwa mwaka wa tatu.

Je yupo sawa? Maoni yenu
 
Promethazine Komaa adi mwisho mdaiwa afungwe

atu tunadaiwa mamilioni na bodi ya mikopo (HESLB)

Itakuwa wewe ada ya mwaka mmoja

Wapige porojo mpaka unamaliza watashikilia cheti chako ukipata pesa utakuja kuchukua,
Diploma ni 3 yes yaani uishie 2 yes uache mmoja

Komaa boss
Hizo case za ada hauko peke yako wapige siasa

Cha msingi ela ya mitihani uko separate ndo ulipie
 
Komaa adi mwisho mdaiwa afungwe
Watu tunadaiwa mamilioni na bodi ya mikopo (HESLB)
Itakuwa wewe ada ya mwaka mmoja
Wapige porojo mpaka unamaliza watashikilia cheti chako ukipata pesa utakuja kuchukua,
Diploma ni 3 yes yaani uishie 2 yes uache mmoja
Komaa boss
Hizo case za ada hauko peke yako wapige siasa
Cha msingi ela ya mitihani uko separate ndo ulipie
Sasa ugumu ni pale wanapokuja kuzuia kufanya mtihani
 
wazazi wapambeane hata ikibidi kuuza mali walizonazo hamna jinsi
 
Wakuu za mida hii

Kuna mtu mmoja anasoma nursing diploma ila kakosa ada ana mpango wa kuishia certificate, je hii itafaa? Ataweza kuajiriwa?

Chuo kina utaratibu wa kuzuia watu ambao hawajamaliza ada kutofanya mitihani ya mwisho, sasa anahofia atazuiliwa kufanya mitihani siku ya mwisho awe amepoteza miaka mitatu yote

Je madhara yake ni yapi na kipi unaweza kumshauri?
 
Back
Top Bottom