Amechoka kunivumilia anataka kuniacha!

Amechoka kunivumilia anataka kuniacha!

huyo mwanamke hakukupenda kaka, tusikudanganye tu hapa. Mapenzi ni kuvumiliana kwenye shida na raha. Kama huna ajira hakutaki siku ukikatika miguu itakuaje? kikubwa kama alivyokwambia huyo mzazi mwenzio weka juhudi zako kwenye kutafuta pesa utampata tu mwenza mwenye mapenzi ya kweli na utalisahau kabisa hilo tapeli la mapenzi.....ni hayo tu
 
Wakuu habari za muda huu?

Naomba niwashirikishe hii changamoto tunayoipitia kati yangu mimi na mzazi mwenzangu!

Ni muda wa miaka sita tangu tulipofahamiana na mama wa mtoto wangu, maisha yetu yamekuwa ya furaha na amani.

Mwaka 2014 nilipata nafasi ya kujiunga shahada ya kwanza katika mojawapo ya vyuo mkoani mbeya, na hapo tatizo ndipo lilipoanzia.

Niliamua kwenda kujiendeleza kitaaluma ili kuongeza maarifa na ujuzi kwa lengo la kuandaa mazingira murua ya baadae. Niliamua kuomba ruhusa kwa mwajiri wangu katika mojawapo wa halmashauri katika mkoa wa Simiyu.

Mwajiri hakuridhia kunipa ruhusa japo nilikua na sifa na vigezo vinavyohitajika ili kupata kibari hicho.

Kwa kuwa nina malengo yangu nikaamua kwenda masomoni na kumuacha mama na mtoto sehemu tuliyokuwa tukiishi. Baada ya mabadiliko ya uongozi hapa kwetu nchini niliondolewa kwenye pay roll kwani taarifa zangu zilionesha sipo kazini. Hali hiyo ilisababisha kuyumba kiuchumi tangu April 2016 na kupelekea maisha yetu kuwa magumu.

Mzazi mwenzagu amevumilia kwa kipindi chote hicho na sasa anasema anataka kunipunguzia matatizo na mawazo kwa kuniacha niendelee na harakati zangu za kusaka maisha na yeye aendelee na shughuli zake huku akimlea mtoto. Nitakapokaa sawa atanipatia mwanangu.

Sasa wakuu naomba ushauri wenu nifanyaje kwani nampenda sana mama wa mwanangu si mpango wangu mwanangu kuja kulelewa na mama mwingine au baba mwingine.

N. B nimetoa mahari ila ndoa bado hatujafanikiwa kufunga.
Mkuu pole upo Arusha?!
 
Wakuu habari za muda huu?

Naomba niwashirikishe hii changamoto tunayoipitia kati yangu mimi na mzazi mwenzangu!

Ni muda wa miaka sita tangu tulipofahamiana na mama wa mtoto wangu, maisha yetu yamekuwa ya furaha na amani.

Mwaka 2014 nilipata nafasi ya kujiunga shahada ya kwanza katika mojawapo ya vyuo mkoani mbeya, na hapo tatizo ndipo lilipoanzia.

Niliamua kwenda kujiendeleza kitaaluma ili kuongeza maarifa na ujuzi kwa lengo la kuandaa mazingira murua ya baadae. Niliamua kuomba ruhusa kwa mwajiri wangu katika mojawapo wa halmashauri katika mkoa wa Simiyu.

Mwajiri hakuridhia kunipa ruhusa japo nilikua na sifa na vigezo vinavyohitajika ili kupata kibari hicho.

Kwa kuwa nina malengo yangu nikaamua kwenda masomoni na kumuacha mama na mtoto sehemu tuliyokuwa tukiishi. Baada ya mabadiliko ya uongozi hapa kwetu nchini niliondolewa kwenye pay roll kwani taarifa zangu zilionesha sipo kazini. Hali hiyo ilisababisha kuyumba kiuchumi tangu April 2016 na kupelekea maisha yetu kuwa magumu.

Mzazi mwenzagu amevumilia kwa kipindi chote hicho na sasa anasema anataka kunipunguzia matatizo na mawazo kwa kuniacha niendelee na harakati zangu za kusaka maisha na yeye aendelee na shughuli zake huku akimlea mtoto. Nitakapokaa sawa atanipatia mwanangu.

Sasa wakuu naomba ushauri wenu nifanyaje kwani nampenda sana mama wa mwanangu si mpango wangu mwanangu kuja kulelewa na mama mwingine au baba mwingine.

N. B nimetoa mahari ila ndoa bado hatujafanikiwa kufunga.
mambo mengine bana sasa unatuhadithia ?unaomba ushauri
? ama nini kaongee na mkeo haaaa????
 
Back
Top Bottom