Kwanza huyo hakuwa mkeo kabisa ila mtu mliyezaa naye tu, hakuona future yake kwako tangu mwanzo inawezekana umezidi kusingizia maisha sana hivyo ameona kuwa wewe huna muelekeo wowote ule zaidi ya jusubiria kisichoonekana.
Kama ungekuwa mwamaume wa nguvu ungeshamuoa kitambo hata kabla hujaenda sijui wapi huko kusoma. Mnapenda kupotezea muda watoto wa watu kwa kisingizio cha maisha, kama unajijua huwezi kuoa mpaka uunge unge maisha acheni kuwazalisha watoto wa watu halafu mnataka kuwalazimisha kuvumilia eti sijui maisha magumu.
Wanaume tumekuwa chanzo cha haya matatizo wenyewe, yaani mnataka wanawake wafanye mazoezi ya kuzoea shida tena wale ambao hata ndoa nao hamna, unafikiri wao hawana akili? Anajiuliza kama tangu tumezaa tumeshindwa kufunga ndoa halali ikitokea kesho kanigeuka itakuwaje wakati sina ndoa yoyote ? Lazima ajiongeze aisee, kama maisha magumu ishi mwenyewe ukijiweza oa na sio kutia mimba halafu baadae usingizie maisha ndio kikwazo eti uvumiliwe tena kwa muda usiojulikana.
Wanawake wamekuwa victims kwa visingizio hivi, mtu unakuta umeenda kusoma unarudi umemsahau binti wa watu kisa yeye mama wa nyumbani, hasa vijana wa kisasa wasiotaka majukumu kabisa, yaani wao wanataka wanawake wa kuwasaidia kimaisha tu na si vinginevyo sasa huyo kakuwahi kwa mbele kabla hujamuwahi. Kama kweli wewe una nia ya dhati nenda msikitini/kanisani kafunge ndoa acha makuu sijui kualika kijiji kizima uone kama atakimbia, lakini kama kila siku visingizio tu vya maisha aisee huyo binti ana akili sana kwani uvumilivu nao una kikomo chake, mwache aende akapumue na wewe utapata mwingine wa kula shida naye.