Homeofservices
Member
- Dec 31, 2017
- 88
- 77
Habarini za Jioni,
Mwaka 2008 nilikuja hapa Mjini Dar es Salaam, baada ya kumaliza Form four na nilibahatika nilikuwa na vi akili kidogo mjomba wangu alinitaka nije nikae nikiwa nasubiri matokeo yangu.
Kwa sababu mjomba alikuwa ananipenda sana, basi alipenda kuwa ananichukua tunaenda wote pale Ilala boma alipokuwa akifanyia kazi.
Enzi hizo Jiji lilikuwa la Kandoro, basi tulikuwa tukipata muda tunatembea kwa miguu kwenda Mjini Kariakoo.
Siku moja nikiwa home niliona na mimi niende Kariakoo, nikipanda magari pendwa yale ya msitari mwekundu.. Kimara-Kkoo.
Basi safari mdogo mdogo bila kujua nashukia wapi, maana sikuwahi kwenda kwa Daladala. Nikastuka tumefika pale Bigbon sheli watu wote wakashuka, nikaona ni vema na mimi nishuke itakuwa ni mwisho basi nilizunguka mule ndani ya Kariakoo kama unavyojua ukiwa umezoewa ground building za kule Mkoani yaani shingo na kichwa vinakuwa Juu juu kushangaa maghorofa.
Nilikuja kustuka imeshafika saa kumi na mbili basi nikasema nipatafute pale Bigbon.Nakumbuka nilitembea takribani lisaa limoja nikipatafuta bila mafanikio.
Wazo lilinijia hivi pale boma si karibu tu, ngoja nipatafute mpaka nipapate then nikaanzie hapo. Nikaitafuta ile round about ya kipindi kile pale Uhuru. Nakumbuka nilitumia nusu saa nikaiona.
Nilipoiona nikaanza mdogo mdogo mpaka Boma, nilipofika pale nikajiuliza nifanye nini ili nikipate hicho kituo likaniijia wazo nipige simu nyumbani basi nikapiga wakaniambia panda tu piki piki umwambie akulete Kimara vinane. Basi nikaitafuta pikipiki huku moyoni nikiwa nasema aisee hii ndiyo Dar.
Ila sasa hivi ukinikuta foleni napambana na foleni ukichomeka nakutukana mshamba nini wewe umekuja mjini lini hahaahahaa!
Kama kuna mwingine alishawahi kupatia kitu kama hiki kiweke tukumbushane.
Mwaka 2008 nilikuja hapa Mjini Dar es Salaam, baada ya kumaliza Form four na nilibahatika nilikuwa na vi akili kidogo mjomba wangu alinitaka nije nikae nikiwa nasubiri matokeo yangu.
Kwa sababu mjomba alikuwa ananipenda sana, basi alipenda kuwa ananichukua tunaenda wote pale Ilala boma alipokuwa akifanyia kazi.
Enzi hizo Jiji lilikuwa la Kandoro, basi tulikuwa tukipata muda tunatembea kwa miguu kwenda Mjini Kariakoo.
Siku moja nikiwa home niliona na mimi niende Kariakoo, nikipanda magari pendwa yale ya msitari mwekundu.. Kimara-Kkoo.
Basi safari mdogo mdogo bila kujua nashukia wapi, maana sikuwahi kwenda kwa Daladala. Nikastuka tumefika pale Bigbon sheli watu wote wakashuka, nikaona ni vema na mimi nishuke itakuwa ni mwisho basi nilizunguka mule ndani ya Kariakoo kama unavyojua ukiwa umezoewa ground building za kule Mkoani yaani shingo na kichwa vinakuwa Juu juu kushangaa maghorofa.
Nilikuja kustuka imeshafika saa kumi na mbili basi nikasema nipatafute pale Bigbon.Nakumbuka nilitembea takribani lisaa limoja nikipatafuta bila mafanikio.
Wazo lilinijia hivi pale boma si karibu tu, ngoja nipatafute mpaka nipapate then nikaanzie hapo. Nikaitafuta ile round about ya kipindi kile pale Uhuru. Nakumbuka nilitumia nusu saa nikaiona.
Nilipoiona nikaanza mdogo mdogo mpaka Boma, nilipofika pale nikajiuliza nifanye nini ili nikipate hicho kituo likaniijia wazo nipige simu nyumbani basi nikapiga wakaniambia panda tu piki piki umwambie akulete Kimara vinane. Basi nikaitafuta pikipiki huku moyoni nikiwa nasema aisee hii ndiyo Dar.
Ila sasa hivi ukinikuta foleni napambana na foleni ukichomeka nakutukana mshamba nini wewe umekuja mjini lini hahaahahaa!
Kama kuna mwingine alishawahi kupatia kitu kama hiki kiweke tukumbushane.