King Kong III
Platinum Member
- Oct 15, 2010
- 62,920
- 95,281
Aliyekuwa Mr.ofisa wa BOT Amatus Liyumba yupo katika timbwili zito na mkewe kwa kugombania hekalu,Liyumba anataka kuiuza lakini mkewe hataki kwhyo sakata limetimba mahakamani.
=======
Source:NIPASHE
=======
Source:NIPASHE
Kama picha fulani vilenamkumbuka mh huyu sikuwahi kumjua kwa sura mpaka kesi ya epa lakini nikkiwa form two alivuma sana sana na magari mekundu kwa mabinti huku kadi za gari akibaki nazo mkononi....na si hili tu kuna baadhi waliumia sana kwa kulazimishwa kushuka kwenye gari na kuliachia walipofika kwenye mataa kisa kutokuelewana na mh huyu.
Sasa hili ni lingine linahusu familia pengine wengi wamepitia kwenye shida hii ya kuuza mali za familia; familia ya Amatus Liyumba imefungua kesi ikiongozwa na mkewe Liyumba kusimamisha uuzwaji wa mali za familia...kesi hiyo imefunguliwa wilaya ya Ilala na mkewe aliefunga nae ndoa 1978 mkoani Kilimanjaro.
Kesi hiyo ilitajwa mahakamani hapo jana na ilihairishwa mpaka kesho ambapo mahakama itatoa uamuzi kulingana na kipingamizi kilichowasilishwa na bw Amatus Liyumba.
Mlalamikaji anaitaka mahakama itoe amri ya kumzuia bwn. Liyumba kuuza mali za familia na yeye aendelee kuishi na watoto wake kwenye moja ya nyumba za familia ambazo mh liyumba alileta madalali wa kuiuza huku mama na watoto wakiwa ndani ya nyumba awajui kinachoendelea.
Kesi hiyo iko mbele ya hakimu Jackline Rugemalila mlalamikaji anatetewa na Margareth Ringo.
Hata hivyo mlalamikaji aliwasilisha kiapo mahakamani cha ndoa yao 1978 na kufanikiwa kupata watoto wa nne Lyinda,Jennifer,Priscus na Yulia na wanaishi kwenye nyumba Africa sana Mbezi Beach.
Kiapo kinasema bwn. Liyumba baada ya kutoka mahakamani alirudi nyumbani na kuanza kuuza rangerover 2, landcruiser 2,trekta moja na benzi mbili pamoja na hekari 50, hakuishia hapo akataka kuuanza kuza na mali ya nyumba wanamoisihi.
Mlalamikaji ameomba mahakama kusimamisha swala hili la uuzwaji wa mali za familia.