Pole kwa yaliyokusibu. Bahati mbaya wazazi wako ni wabinafsi. Ulichotakiwa ni kuongea ukweli tu, na hata kama matokeo yangemuathiri mmoja wa wazazi wako, huo ndio ukweli na asingeweza kukushutumu juu ya wewe kuongea ukweli wa kilichotokea. Ni kama alivyofanya mdogo wako kutokana na udogo wake na hivyo hakuchukulia atamdhuru au kumpendelea nani. Ukijaaliwa kupata watoto, wafunze kusema ukweli, na pia hakikisha huwakwazi kwa kuendekeza ubinafsi.
Kwa sasa jaribu kufuatilia maisha yako, inaelekea magomvi ya wazazi yanakuathiri, yaliyotokea yametokea, tengeneza maisha yako usije haribikiwa kwa kujaribu kuwaridhisha wao, wala usijihisi kuwa uliwakosea, wao ndio walikukosea wewe na wadogo zako kwa kutokuwa na maamuzi ya busara katika maisha.