Almanusura mtoto atolewe kafara

Almanusura mtoto atolewe kafara

Aiseeee huyu mwehu kweli akapimwe akili
Mnamo tarehe 19/12/2019 majira ya SAA 18:30hrs A/Insp Mganga nikiwa na askari wenzake doria nyuki tulipata taarifa kuwa maeneo ya nguzo camp site kwenye maporomoko ambako yanakingwa maji ya Railway kuna mtu anakata mabomba ya miundo mbinu ya maji na anaoneka akiwa na mtoto anayekadiriwa kuwa na umri 5_7 akiwa amemshikilia ndani ya maporomoko ya maji,huku akiwa na panga na msumeno kitendo kinachoashiria kuwa na nia ovu dhidi yake na mtoto. Askari wametumia ujasili was hali ya juu kuokoa maisha yake na mtoto Mara baada ya mtu huyo kujitosa kwenye kina cha maporomoko marefu ya maji na kufanikiwa kuwaokoa maisha yao.
View attachment 1298392

Jr

Update
Hili tukio si Mbweni ya Dsm kama inavyotangazwa kwa sababu zifuatazo:
1. DSM hakuna mto wenye maji meupe vile mito hii yenye maji meupe hupatikana sehemu yenye milima kama vile, Moro, Mbeya, Kilimanjaro Tanga na Arusha.
2. Dar hakuna mto unaokuwa na Maporoko ya maji (water falls) kama inavyoonekana.
3. DSM hususani Mbweni iliyojirani na bahari hakuna mawe (miamba) ya namna ile kama yanayoonekana miamba ya pwani (coastal rocks) ina julikana kwa kuiona.
Ni kweli tukio hili limetokea Tanzania kutokana na lugha inayozungumzwa pale lakini si Mbweni ya Dsm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao Askari kweli?

Yaaani kama kwenye hii clip Askari wetu ndio wana mafunzo kama haya.
Maana yake askari wetu ni

Taka taka kabisa
Aisee! Yaani kuna watu mmejaa kejeli kwa kila kitu.
Mtu alikuwa na kisu na msumeno na ukiangalia hali ya mazingira ilivyo lakn mtoto kaokolewa akiwa salama lakn bado unalaumu..

Hayo ndio matatzo ya kukalilishwa matukio ya kwenye movie ya kuandaliwa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom