Aliyenizidi umri anapokataa salamu ya shikamoo nimpe salamu gani?

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Katika Mila na desturi za Tanzania shikamoo ni salamu unayompa mtu aliyekuzidi umri. Nimekutana na watu wazima waliokwepa salamu hii. Mfano mtu mzima uliyemuajiri, anaitikia vizuri shikamoo za wengine lakini shikamoo kutoka kwa boss inamsumbua.

Pamoja na kuwa kijana au binti unaeweza kumzaa akawa boss wako lakini haibadili ukweli kuwa uliiona dunia kabla yake na hii ni heshima unayostahili. Hizi ni Mila na desturi zetu.

Maoni yenu tafadhali mtu mzima asiyetaka salamu ya shikamoo nimpe salamu gani?
 
Kama wa kiume na kike jua huyo mkubwa anataka mapenzi!
Labda mpe tamu ndiyo ataanza kukubali shikamoo zako


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
U hali gani, baba, /mama? Njema hali yako, mjomba/shangazi? Asante, achana na salaam za mwalimu na wanafunzi wake(shikamoo- marahaba!).
 
Sky, wewe endelea kumpa heshima yake kwa kumuamkia shikamoo kwa sababu umehiari na haikupunguzii kitu, ukiona haitikii, muite umpe warning kwamba ni lazima aitikie salaam yako, ni mila zetu hizo.
 
Woooiiiiii yanini kuzeeshana...shikamoo uiache ndani ukitoka kwenu...mujini ni habari ya saizi full stop....
 
Wazazi wako nyumbani uwaambie hi or hello dady/mum....ukija huku kazini tuanze mishikamoo nani anataka huo ujinga...
 
Hapo jamaa anakwepa kunyimwa! By the way shikamoo ilitumika zamani kwa watumwa kuwaambia watwana kwamba tuko chini ya miguu yako,hivyo si salamu ya kiungwana kwa jamii ambazo zimeshakuwa huru kifikra
 
Sky Eclat,
Goodmorning/ afternoon au evening zitamfaa huyo. Au Kiswahili chake habari za asubuhi, mchana, na jioni. Kama bado hajielewi basi mpe hujambo.

Ila kama za wengine anapokea ya kwako hataki, basi yawezekana upo 'hot hot' kiasi kwamba anafikiri sio muda mrefu ataona ndani. Punguza uchangamfu kwake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom