PostGE2025 Aliyekosoa mchakato wa uteuzi wa Samia ndani ya CCM, Mzee Godfrey Malisa ashtakiwa kwa UHAINI

PostGE2025 Aliyekosoa mchakato wa uteuzi wa Samia ndani ya CCM, Mzee Godfrey Malisa ashtakiwa kwa UHAINI

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Mchungaji Godfrey Malisa, aliyekuwa mwanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi mkoani Kilimanjaro akikabiliwa na kosa la uhaini. Kesi hiyo (Namba 000028333 ya 2025) inatarajiwa kutajwa kesho, Ijumaa, Januari 2, 2026, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Ally Mkama.

Mchungaji Malisa anashitakiwa chini ya Kifungu 39(2)(d) cha Kanuni ya Adhabu (Sura ya 16) kama kilivyofanyiwa marejeo mwaka 2023. Anatuhumiwa kutenda kosa hilo mnamo Novemba 16, 2025, katika eneo la Miembeni, Wilaya ya Moshi.

Hati ya mashitaka inadai kuwa mshitakiwa alinuia kuhamasisha umma kushiriki katika mikusanyiko isiyo halali kwa lengo la kumtishia mtendaji mkuu wa Serikali. Inadaiwa kuwa alitoa matamko ya kumtaka Rais Samia kujiuzulu kabla ya Desemba 9, 2025, na kutishia kuanzisha maandamano makubwa nchini iwapo matakwa yake hayatatekelezwa.

Katika taarifa iliyosambaa Novemba 21, 2025, ilidaiwa kuwa Mzee Malisa alitekwa majira ya usiku nyumbani kwake maeneo ya Msamaria Majengo au Malenga, siku chache baada ya kutoa maazimio ya Kamati ya Kitaifa ya Kurejesha Haki na Amani katika Tanzania.

Unaweza kusoma zaidi hapa: Tetesi: - Inadaiwa Dkt. Godfrey Malisa ametekwa jana usiku akiwa nyumbani kwake

Zingatia: Kosa la uhaini chini ya kifungu hicho haliruhusu mshitakiwa kujibu chochote katika mahakama ya chini, na adhabu yake kisheria ni kifo iwapo mshitakiwa atapatikana na hatia.

Kesi hii inakuja wakati kukiwa na mfululizo wa mashitaka dhidi ya watu mbalimbali kufuatia maandamano ya Oktoba 29, 2025, ambayo Serikali iliyatangaza kuwa ni haramu.
  • Msamaha wa Rais: Rais Samia Suluhu Hassan alitoa maelekezo kwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kuwafutia mashitaka vijana walioingia kwenye maandamano hayo kwa mkumbo, akibainisha kuwa wengi hawakujua madhara ya vitendo vyao.
  • Kifungu cha 91(1): Baadhi ya washitakiwa tayari wamenufaika na kifungu hiki cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) na kuachiwa huru.
Kabla ya kufikishwa mahakamani, Malisa alikuwa akionyesha misimamo mikali dhidi ya uongozi uliopo, ikiwemo:
  1. Kufungua kesi mahakamani kupinga uteuzi wa mgombea urais ndani ya CCM.
  2. Tishio la kufungua kesi ICC: Alitangaza nia ya kuwafungulia mashitaka Rais Samia na IGP Camillus Wambura katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kwa madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu.
Hadi kufikia kesho, Mchungaji Malisa atakuwa ametimiza siku 30 tangu alipowekwa kizuizini kufuatia kukamatwa kwake nyumbani kwake mwezi Novemba 2025.

Wasifu wa Mchungaji Godfrey Malisa

Mchungaji Malisa (PhD) ana historia ndefu ya ushiriki katika siasa za upinzani na CCM:
  • 2010: Aligombea Ubunge Moshi Mjini (TLP).
  • 2015: Aligombea Urais (CCK) na baadaye Uspika.
  • 2018-2020: Aligombea Ubunge kupitia TLP na NCCR-Mageuzi kabla ya kuhamia CCM.
  • 2025: Alifukuzwa uanachama wa CCM mkoani Kilimanjaro kwa madai ya kupinga maamuzi ya Mkutano Mkuu wa Taifa wa kuteua mgombea urais, jambo lililotajwa na chama kama utovu wa nidhamu na kudhoofisha umoja.
Pia Soma:
Dkt. Malisa awafungulia Kesi Rais Samia na IGP Wambura Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) The Hague

Katika taarifa iliyosambaa Novemba 21, 2025, ilidaiwa kuwepo kwa taarifa mzee huyo (Mchungaji Malisa) alitekwa majira ya usiku nyumbani kwake maeneo ya Msamaria Majengo au Malenga, siku chache baada ya kutoa maazimio ya Kamati ya Kitaifa ya Kurejesha Haki na Amani katika Tanzania.

Unaweza kusoma zaidi hapa: Tetesi: - Inadaiwa Dkt. Godfrey Malisa ametekwa jana usiku akiwa nyumbani kwake
 
Mchungaji Godfrey Malisa aliyekuwa mwanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kabla ya kufukuzwa uanachama mwaka jana, ameshitakiwa kwa kosa la uhaini katıka Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi.

Kesi hiyo iliyopangwa kutajwa kesho, Januari 02, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Ally Mkama.

Malisa, ambaye hapo awali alifukuzwa uanachama wa CCM baada ya kupinga uteuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan kama mgombea urais wa chama hicho, amekabiliwa na mashtaka hayo makubwa.

===

Hivi maridhiano yatapatikana kweli?

Mzee huyu alikamatwa lini na mchakato wa kumfikisha Mahakamani ulikuwaje?
 
Huyu mzee Malissa naonaga anaongea ongea tu kupinga uhalali wa Rais nk nk

Ila maneno tu hayatoshi kumtia hatiani kama maneno yale hayako kwenye njama au mipango ya kutaka kumtoa raisi madarakan kwa nguvu.

Hii ndio mfano halisi wa
"Kumkomoa nyani Kundule".
 
Kwa hali hii hata mimi basi ni Mhaini! Kwa sababu mpaka sasa ninaamini muungano tuliokuwa nao wa changu changu, chako changu ni wa muungano wa kipuuzi, hivyo ni bora ukavunjwa tu ili kila nchi ijitegemee yenyewe!! Pili ninaipenda Tanganyika zaidi kuliko Tanganyika!
Tatu ninaamini Tundu Lissu ndiye anayestahili kuwa Rais wa Tanganyika huru! Na hata huko gerezani anashikiliwa kwa uonevu! Nne ninaamini tarehe 29 Oktoba hakukufanyika uchaguzi! Tano ninaamini kuna mtu yuko madarakani kwa ushawishi wa kikundi cha watu wachache wenye nia ovu na nchi!

Kwa hali hii Watanganyika walio wengi ni wahaini!
 
Huyu Godfrey Malisa alikuwa anatumika na watu fulani, ile siyo akili yake.

Muache amalize uzee wake kwa shida
Nyie kila mtu akikemea utekaji, ufisadi, wizi wa kura anatumika na mabeberu mara analipwa na NGOs

Hao wanaotumia watu hawana vitu vya kufanya hadi wawe wanatuma kila siku wao wazungumzie matatizo wanayokumbana nayo kwao.

Yaani mtu anaona kabisa mzee Kibao kashushwa kwenye gari kesho kapatikana maiti haina macho na mwili umeharibika kutokana na kumwagiwa tindikali anakemee nyie mnasema kalipwa.

Mtu anakemea Mdude kavamiwa na wahuni wa policcm wamempiga na nyundo kichwani damu zimechuruzika chini nyie mtasema analipwa kukemea uhuni huo.

Polepole kavamiwa kapigwa tunaona michirizi ya damu na haonekani leo mwezi wa tatu linakuja jinga lingine litasema anayesema na kukemea haya analipwa.

Dar es Salaam jiji kubwa halina maji watu wakisema ni ujinga nchi kutegemea mvua kama chanzo cha maji licha ya uwepo wa vyanzo lukuki vya maji atakuja mjinga mwingine kusema analipwa na NGO.

Yaani orodha ya matatizo ni mengi na yanawakumba wakazi wa Tanzania ila wanapopaza sauti kukemea wanaambiwa wanalipwa.

Hivi wewe ndugu yako akikwapuliwa usiku saa 8 kwake halafu unaambiwa watu hao waliomchukua hawajulikani utasubiri NGO ikulipe kukemea ushenzi huo.?
 
Back
Top Bottom