Aliyekamatwa akilima bangi ekari tatu asema ilimuingizia fedha zilizomuwezesha kununua mifugo

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
Nkire Chacha, mmiliki wa ekari tatu za shamba la bangi amesema alikuwa akipata fedha zilizomwezesha kununua mifugo anayoitumia kwenye kilimo.

Mtuhumiwa huyo mwenyeji wa Kijiji cha Sogoti wilayani Serengeti alikamatwa jana.

Hata hivyo kutokana na mazingira ya eneo imebainika kuwa kilimo hicho kimefanyika kwa muda mrefu na watu mbalimbali lakini hata viongozi wa eneo hilo hawakutoa taarifa.

Mbele ya kamati ya ulinzi na usalama inayoongozwa na mkuu wa wilaya, Nurdin Babu alisema soko lake lilikuwa hapohapo kijijini na limemsaidia kupata fedha za kukidhi mahitaji mbalimbali.

“Kwa kweli mbegu za bangi hii zilikuwa ndani ya nyumba yangu nilizitoa na kuzimwaga shambani maana hata mimi mwenyewe ninatumia, mimi sijawahi kusafirisha kwenda popote kwa kuwa wateja wanakuja nyumbani wenyewe na nimenunua ng’ombe wa kulimia,” alisema.

Babu akimkabidhi mtuhumiwa huyo kwa polisi baada ya kukamilisha ukaguzi ulioongozwa na hakimu mkazi, Felix Ginene.

“Kila siku tunahamasisha kilimo cha mazao kama pamba, mahindi na mengine lakini wananchi kwa kushirikiana na viongozi mnakwenda kinyume, lazima tuwafikishe mahakamani,” alisema Babu.

Alisema maeneo hatari kwa kilimo cha zao hilo haramu ni kata za Kebanchabancha na Machochwe lakini wataendelea kuwakamata.

“Huyu amehusika kuwavuruga wananchi kwa kuwauzia dawa za kulevya, atakuwa fundisho maana tulishawataka walime mazao yanayokubali,” alisema.

Mkuu wa polisi wilaya, Methew Mgema alisema watu watatu akiwemo mwenyekiti wa kitongoji wanashikiliwa.

“Huyu alikuwa anajua maana ndiyo wanaogawa mashamba na anaishi hapahapa. Tutawakamata viongozi kila tutakapokuta bangi kwenye maeneo yao na wao hawatoi taarifa,” alisema.

Mwenyekiti wa kitongoji, Magabe Chacha alisema hakuwa na taarifa ya kilimo hicho.
 
Nadhani Shida sio kuruhusu bangi iwe kilimo cha biashara ya madawa au matumizi binafsi

Shida inakuja sisi watu wa taifa hili bado sana kuhandle consequences za mabangi

Ni Sawa umpangie chumba mtaani mtoto wako wa kike wa form one useme amekua, Utampoteza tuu
 
Hapo kamati ya roho mbaya ishafanya yake imeona jamaa anafaidii
Ukizingatia 'ujinga' na 'umaskini' ndio sera ya chama pendwa, yeyote anayejaribu kujikwamua ni mhujumu uchumi, angalia wanavyojilipa wenye nchi, unabaki unajiuliza nani mhujumu uchumi hapa?
 
Serikali iangalie namna ya kuitoa bangi miongoni mwa mdawa ya kulevya.

Sijaona ubaya wa bangi
Ni nani ameshindwa kuhandle ulevi wa bangi!?
Ni yupi anaeweza kuhandle ulevi wa pombe!?

Ujue hakuna mtu anevuta bangi anaeshindwa kuvuta kwa sbb eti serekali imekataza" bangi ipo mitaani nyingi tu na watu wanatumia kisirisiri miaka na dahari.

Hata serekali ikiruhusu hakuna mtu ataevuta eti kwa sababu imeruhusiwa"!

Kama zilivo sigara kuna wanovuta na wengine hawatumii japo ni halali.

Hapo kenya miraa ni halali na serekali yao inapata pesa kupitia miraa, huku kwetu watu wanatumia lakini serekali haipati kitu na inazidi kuwatia watu umasikini kwa kuzuia biashara zinazoweza kumwingizia mnyonge kipato halali"
 
Gunia moja la bangi milioni moja
Huwa zinasafirishwa usiku kwa baiskeli .
Kwenda town wengine huwa wanadakwa usiku.
Kitu chochote haramu kina bei kubwa sana sawa sawa na dawa la kulevya mengine
 
Ujinga mtupu, huku kitaa raia kama wote wanapuliza alafu mnavunga hamuwaoni.
 
Nadhani Shida sio kuruhusu bangi iwe kilimo cha biashara ya madawa au matumizi binafsi

Shida inakuja sisi watu wa taifa hili bado sana kuhandle consequences za mabangi

Ni Sawa umpangie chumba mtaani mtoto wako wa kike wa form one useme amekua, Utampoteza tuu
Kwahiyo hao ambao wanatumia nani anawasaidia kuhandle hizo consequences??
 
Ni nani ameshindwa kuhandle ulevi wa bangi!?
Ni yupi anaeweza kuhandle ulevi wa pombe!?

Ujue hakuna mtu anevuta bangi anaeshindwa kuvuta kwa sbb eti serekali imekataza" bangi ipo mitaani nyingi tu na watu wanatumia kisirisiri miaka na dahari.

Hata serekali ikiruhusu hakuna mtu ataevuta eti kwa sababu imeruhusiwa"!

Kama zilivo sigara kuna wanovuta na wengine hawatumii japo ni halali.

Hapo kenya miraa ni halali na serekali yao inapata pesa kupitia miraa, huku kwetu watu wanatumia lakini serekali haipati kitu na inazidi kuwatia watu umasikini kwa kuzuia biashara zinazoweza kumwingizia mnyonge kipato halali"
Point yangu ni kwa wale wanaofungwa kwa kulima, kuuza au kuvuta.

Wewe fikiria umefungwa kwa kosa la kuvuta kiburudisho chako
 
Nkire Chacha, mmiliki wa ekari tatu za shamba la bangi amesema alikuwa akipata fedha zilizomwezesha kununua mifugo anayoitumia kwenye kilimo.

Mtuhumiwa huyo mwenyeji wa Kijiji cha Sogoti wilayani Serengeti alikamatwa jana.

Hata hivyo kutokana na mazingira ya eneo imebainika kuwa kilimo hicho kimefanyika kwa muda mrefu na watu mbalimbali lakini hata viongozi wa eneo hilo hawakutoa taarifa.

Mbele ya kamati ya ulinzi na usalama inayoongozwa na mkuu wa wilaya, Nurdin Babu alisema soko lake lilikuwa hapohapo kijijini na limemsaidia kupata fedha za kukidhi mahitaji mbalimbali.

“Kwa kweli mbegu za bangi hii zilikuwa ndani ya nyumba yangu nilizitoa na kuzimwaga shambani maana hata mimi mwenyewe ninatumia, mimi sijawahi kusafirisha kwenda popote kwa kuwa wateja wanakuja nyumbani wenyewe na nimenunua ng’ombe wa kulimia,” alisema.

Babu akimkabidhi mtuhumiwa huyo kwa polisi baada ya kukamilisha ukaguzi ulioongozwa na hakimu mkazi, Felix Ginene.

“Kila siku tunahamasisha kilimo cha mazao kama pamba, mahindi na mengine lakini wananchi kwa kushirikiana na viongozi mnakwenda kinyume, lazima tuwafikishe mahakamani,” alisema Babu.

Alisema maeneo hatari kwa kilimo cha zao hilo haramu ni kata za Kebanchabancha na Machochwe lakini wataendelea kuwakamata.

“Huyu amehusika kuwavuruga wananchi kwa kuwauzia dawa za kulevya, atakuwa fundisho maana tulishawataka walime mazao yanayokubali,” alisema.

Mkuu wa polisi wilaya, Methew Mgema alisema watu watatu akiwemo mwenyekiti wa kitongoji wanashikiliwa.

“Huyu alikuwa anajua maana ndiyo wanaogawa mashamba na anaishi hapahapa. Tutawakamata viongozi kila tutakapokuta bangi kwenye maeneo yao na wao hawatoi taarifa,” alisema.

Mwenyekiti wa kitongoji, Magabe Chacha alisema hakuwa na taarifa ya kilimo hicho.
Mi nawaza tu hao Ngombe alionunua kwa kutumia hela za madawa ya kulevya.Zenyewe ziko slama au nazo watazitaifisha? sababu ni utakatishaji wa fedha, au
nasema uongo ndugu zangu?
 
Gunia moja la bangi milioni moja
Huwa zinasafirishwa usiku kwa baiskeli .
Kwenda town wengine huwa wanadakwa usiku.
Kitu chochote haramu kina bei kubwa sana sawa sawa na dawa la kulevya mengine
Hadi milioni tatu gunia moja
 
Gunia moja la bangi milioni moja
Huwa zinasafirishwa usiku kwa baiskeli .
Kwenda town wengine huwa wanadakwa usiku.
Kitu chochote haramu kina bei kubwa sana sawa sawa na dawa la kulevya mengine
Niko zaidi ya million moja,debe tu linaweza fika laki tatu
 
Mkulima huyu awezeshwe, maana hata Ndugayi anatumia huu mmea japo kwa siri

Kujaza magereza na walimaji na wavuta bangi ni hasara kwa taifa!!! Mkulima huyu amekosea wapi; mmea huu unatumiwa kama dawa na watu wengi tu kwa maelekezo ya madaktari bingwa!!! Ufike wakati tutumie akili tunapotekeleza hizi sheria tulizorithi toka enzi ya ukoloni!!!
 
Back
Top Bottom