TANMO
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 11,513
- 11,276
MSEMO wa mapenzi yaua nusura utimie kwa mrembo Sophia Amir, baada ya kuamua kubwia sumu, kisa kulikosa penzi la mtoto wa mkuu wa mkoa (jina kapuni), chanzo kinaarifu. Mwishoni mwa wiki iliyopita, Sophia ambaye ni mkazi wa Kawe jijini Dar es Salaam, alidaiwa kumeza idadi kubwa ya vidonge aina ya Flagyl kwa lengo la kujiua.
Chanzo cha habari kinaeleza kwamba, msichana huyo alipatwa na wazimu wa mahaba baada ya mtoto huyo wa mkuu wa mkoa kwa jina moja anaitwa Thomas kumtamkia wazi kuwa hamtaki tena kimapenzi.Walikuwa wapenzi wa siku nyingi, lakini yule kaka akamwambia Sophia kuwa amemwacha, kwa uchungu ndiyo akaamua kunywa hivyo vidonge, watu wakamuwahi, kalazwa Mwananyamala hospitali, chanzo kilifunguka.
Baada ya taarifa hiyo, mwandishi wetu alikwenda hospitalini ambako alimkuta mrembo huyo akipatiwa matibabu na bila ajizi alikiri kutaka kujitoa roho.Nampenda sana, aliniahidi mambo mengi, leo nikimpigia simu hapokei wakati mwingine ananitukana, nikaona ni bora nijiue, alisema Sophia huku akibubujikwa machozi.Kama ilivyo ada habari lazima itende haki, mwandishi wetu alimpompigia simu Thomas alijibu kwa kifupi: Usinifuatefuate, kisha akakata.
My take: Duh..!
Chanzo cha habari kinaeleza kwamba, msichana huyo alipatwa na wazimu wa mahaba baada ya mtoto huyo wa mkuu wa mkoa kwa jina moja anaitwa Thomas kumtamkia wazi kuwa hamtaki tena kimapenzi.Walikuwa wapenzi wa siku nyingi, lakini yule kaka akamwambia Sophia kuwa amemwacha, kwa uchungu ndiyo akaamua kunywa hivyo vidonge, watu wakamuwahi, kalazwa Mwananyamala hospitali, chanzo kilifunguka.
Baada ya taarifa hiyo, mwandishi wetu alikwenda hospitalini ambako alimkuta mrembo huyo akipatiwa matibabu na bila ajizi alikiri kutaka kujitoa roho.Nampenda sana, aliniahidi mambo mengi, leo nikimpigia simu hapokei wakati mwingine ananitukana, nikaona ni bora nijiue, alisema Sophia huku akibubujikwa machozi.Kama ilivyo ada habari lazima itende haki, mwandishi wetu alimpompigia simu Thomas alijibu kwa kifupi: Usinifuatefuate, kisha akakata.
My take: Duh..!