Alinitenda, aliniumiza, nataka kumuadhibu

Alinitenda, aliniumiza, nataka kumuadhibu

samehe saba mara sabini...usilipe kisasi we mwambie tuu huna mipango nae
 
Huna sababu ya kumpa adhabu. Desperate times kwake hizi..kula wikiendi na bi mdogo huyo, after all she's a free bird, anatua mti wowote, wikiendi hii kwako..ijayo kwa mwingine...mie ningelamba afu namwambia next weekend gf anakuja so atue mti mwingine.
Ushauri wako umeenda kidato
 
Story yako ni tofauti na topic kiukweli hakukutenda ila hamkushabiahana hapo mwanzo yy alikua anataka haraka2 so msingi mpotezee coz hiyo miaka minne haujui kaja na nn huko alikowepo so usimkaribie ww mpotezee tu ndo msingi
 
Before you embark on a Journey of Revenge dig two Graves..

Hio quotation ina maana kwamba mara nyingi kama sio zote ukilipiza kisasi mwisho wa siku unajiumiza wewe na muhusika pia
 
mle mini kabang
mamaa.jpg mamaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!
 
]jaman jaman jaman...! adhabu kwa kosa lipi sasa?
Kwa kosa la kuniumiza
Kosa ni yale maumivu aliyoniachia na kutokunisikiliza
kakuacha coz aliona kama hueleweki!
Kwahiyo baada ya miaka minne na kwa kuongea kwa simu tu wiki mbili ndio naeleweka?
kajisikia kukutafuta coz bado anakufeel, hutaki mwambie SITAKI over,
Yawezekana ni kweli lakini, Kuna maji aliyavulia nguo akashindwa kuyaoga sasa adhabu stahiki ni muhimu kwake ili asije kufanya ujinga huo tena kwangu na kwa mwingine na hapa ni funzo na kwa wengine pia.
isitoshe kutaka kumwadhibu kunaonyesha jinsi ambavyo bado unampenda ila hujui tu ufanyeje coz alionyesha misimamo yako, ngoja niulize kitu, kwa miaka hiyo minne we huna mtu kweli?
Siku zote adhabu haimaanishi kukomoa, Lengo ni kutoa funzo, Mimi kuwa na mtu ama lah, Si hoja hoja ni biashara yangu na yeye tu.
 
Umeisoma hii signature ya Heaven on Earth? hizi signature zina maana sana sana msizipuuze, ukimaliza kusoma hii ya Mpwa wangu soma na ya kwangu hapa chini

You may not be her LAST,her FIRST,or her ONLY,she loved before she may love again
IF she love you now what else matters!!!!!!!!!
Heaven on Earth Swadakta, UMENENA.
What matters ni kuwa kachezea shere hisia zangu, Na kwa hiyo kuna gharama ya kulipa.
As for[MENTION] Elli[/MENTION]
.but what MAN is entirely without Evil intent in the Silence of his Soul???
Guess, None.
 
Last edited by a moderator:
Sasa visasi vya nini mkuu? kwanza kwenye story yako umesema kwamba ''hukutaka wala kuhitaji sana malumbano na kwa roho safi uliachia behewa likatike'' Mpotezee tu, na sio ajabu yeye ndo anakuja kukumaliza sasa
 
Wewe ndio wa kumsaidia kwa sasa ili asiendelee kupotea.
Nakuelewa, Lakini wengi mnadhani nakurupuka tu kuamua kuwa anastahili adhabu.
Iko hivi; Haikutokea tu siku moja akaamua kunitosa, Alianza kwa vituko vidogodogo ambapo mara zote nimekuwa nikimuelewesha kuwa si sahihi, Nilipoona vimepitiliza nikaamua kuachia ngazi.
Hata mtoto haishauriwi kumuadhibu kwa adhabu kumbwa mwanzo tu wa makosa atakuwa hajifunzi,
Utaweka sheria zako, akikosea utamwambia amekosa, akiendelea utamuelekeza tena, akizidi utamsema, ikizidi zaidi utamkaripia, Utamgombeza na ikibidi utamchapa kabisa.
Sasa kwa huyu yote hayo yalishapita. Lengo ni kumfundisha maisha ya kimahusiano.
Na zinazokera zaidi ni kumbukumbu za vimaneno vyake vya nyodo.
Si kwa nia mbaya hii_muelewe.
 
Hastahili adhabu yeyote. Acheni uzinzi sio kila siku kulia lia wakati matatizo mnayatafuta wenyewe. Mimi hata nikizini nikiachana na mwanamke siwezi kuanza kulia lia eti sijui kanitenda, sijui nimpe adhabu. Kwanza kakukosea kitu gani hasa??!!!

Mjasiria nakubaliana na wewe sana Lakini pia Dalalitz kama unataka kumhukumu je, umejiuliza nikwakiasi gani UMEKUA UKIMKOSEA MINGU WAKO?kama ukijitathmini basi Mungu atakupa baraka na reheme zake kwakua hukumu anayo Mungu..
sikushauri urudiane au usirudiane nae lakini nakusihi usimhukumu bali Muombe Mungu akusaidie ushinde vishawishi.
 
Kikatae kikombe hicho cha kumuadhibu; Kumbuka Kiendacho hurudi; ni lazima yatamsibu makubwa huko mbeleni pasi na wewe kuhusika na kwa hiyo utakuwa umekwepa dhambi ya kulipiza kisasi. forgive but do not forget; hilo ni darasa kubwa sana kwako; pole sana
 
Alikuumiza unataka kumuadhibu?
Jibu haya maswali matatu
1. Ukishamwadhibu utafaidika na nini?
2. Bila kujali aina ya adhabu utayompa huoni kuwa unaweza kuingia matatani?
3. Miaka minne bado unahisi huyo ni mtu wa kumkaribisha katika maisha yako?
 
Back
Top Bottom