Alinitenda, aliniumiza, nataka kumuadhibu

Alinitenda, aliniumiza, nataka kumuadhibu

jaman jaman jaman...! adhabu kwa kosa lipi sasa? au kuna kisa nyuma ya pazia? kakuacha coz aliona kama hueleweki! kajisikia kukutafuta coz bado anakufeel, hutaki mwambie SITAKI over,

isitoshe kutaka kumwadhibu kunaonyesha jinsi ambavyo bado unampenda ila hujui tu ufanyeje coz alionyesha misimamo yako, ngoja niulize kitu, kwa miaka hiyo minne we huna mtu kweli?
 
Huko alikoenda walimwahisha?kama jamaa alimchelewesha?

Mimi ningemtaftia wahuni wenye ugwadu wa kutosha wampige mtungo huku wanamrekodi. Hiyo ndio adhabu ndogo ningemchagulia.
angalia huo mtungo usijekukugeukia mwenyewe kesho ukajipeleka kwa muumba kabla hajakuita....
 
makubwa, sa hapo ulitendwa nini au una mengine umeyaficha
 
Wewe ndio wa kumsaidia kwa sasa ili asiendelee kupotea.
 
!
!
wadau humu ndani kuna shifti nini? duh hamlali ati teh teh teh teh. Anyway muite mkate bonge la banzi la uso akuyumba mpe bonge la tama na akuanguka kanyaga kabisa afu mwambie blad ful kenge manyoya.



Hahaaaaaaa mkuuu unaweza kuua aiseeee
 
hekima ni muhimu hapo..... kama ni miaka minne ishapita hakukutafuta na kwa sasa ghafla anakuambia she is ready to mingle.... wakati kipindi kile alikuwa anataka ndoa kwa haraka lakini kwa miaka minne kakosa ina maana kila aliyekuwa nae ameona makucha zaid ya wewe uliyoaona kwa muda wa miez sita yenu.... huyo anataka kukupotezea muda na maisha pia usipokuwa makini.... we pandisha kioo endelea na safari yako....
 
Angalia usije ukapiga punch ukutani, utaumia mkono wako!
 
Mkuu dalalitz pole sana ...

Napenda kukukumbusha jambo moja, sio kila kosa linaadhibiwa ndio maana duniani kukawa na msamaha. Pili sio lazima urudiane nae, mwambie ukweli kuwa alikuumiza na huwezi kuwa nae kama mlivyokua mwanzo. Hizi tabia za visasi ni hatari kwani vinakua na muendelezo katika maisha yako. Kama wewe hautafanyiwa atakuja kufanyiwa mwanao baadae kwa kosa ulilofanya wewe.

Alikosea au alidanganywa na mtu, ndio sababu akakuona wewe ni bora na kuamua kurudi kwako. Usiharibu ubora wako kwa kitu kisichokusaidia kwa lolote. Msamehe bure kwani mpaka hapo alipo ni adhabu tosha ashaipata.

Pole sana ila kurudiana nae sikushauri.
 
Last edited by a moderator:
Kwanza niseme tu kwamba huyo dada bado unampenda ndio maana roho inakuuma mpaka baada ya miaka minne.....
Umpe adhabu ya nini? Alipoondoka aliondoka na dushe yako?? It is a free country....kuwa na mpenzi haimaanishi kwamba unamiliki moyo wake. Ana haki ya kufanya maamuzi yanayohusu maisha yake binafsi....humtaki mwsmbie tu kwamba sikutaki.
 
Kama ambavyo viganja vyetu ni vikubwa lakini tuna mbamiza mbu ambae hata mikononi hajai ni sawa na Mungu wetu anaweza kutuadhibu the same lakini anahuruma wewe unaanzaje kujitutumua eti umpe adhabu adhabu ya nini kwani kuachana ni kosa.
Kama uliweza kumove on muda wote huo yanini uhangaike nae mpotezee na umuoneshe umhitaji
 
Alitokea kuwa
binti mzuri aliyenivutia machoni mwangu.
Tabia na busara zake vilistahili kusifika kwa mujibu wa nilivyomsoma na
kumfahamu
ingawa ni kwa muda mfupi (kadiri ya miezi 6 ya uhusiano wetu)

Kifupi alikidhi vigezo vyangu binafsi,
Alistahili kuwa mama mtarajiwa wa watoto wangu wazuri kama tungejaaliwa
kuwa pamoja.

Mwenyezi Mungu hamfichi mja wake.
Mbali ya kuwa mtaratibu, mkimya na mwenye kuonyesha kunijaali katika
muda mfupi.
Binafsi, nilikuja kung'amua kuwa alikuwa yuko na kimuhemuhe cha kuingia
katika ndoa na pengine ndio sababu ya yeye kuwa mnyenyekevu wa aina ile
kwangu.

Tofauti na mie, Mimi mishale yangu ya uhusiano bado ilionyesha bado
niponipo kamili kwa kipindi kile.
Ilinibidi nimuweke wazi juu ya msimamo wangu, kwa sababu sina hulka ya
kucheza na muda wa wengine.

Basi bwana, binti kwa ujinga wake (nadhani) Kwakuwa pengine alikuwa
'desparate' na ndoa akaamua kujivisha Mabomu hivyohivyo.
Liwalo naliwe akiamini kuwa pengine nitabadilika mbele ya safari.
Akajiachia, Mguu-pande mguu sawa, Kanivulia 'Thong' yake.
Nifanyeje? Mzee mzima 'nikajilia' vyangu.

Maisha yakawa yanaenda.
Mimi niliamini muda muafaka ukifika hakika nitamvika Pete ya uchumba
kidoleni mwake na mchakato wa kuhamia kambi ya wala 'Tunda kwa idhini
rasmi' basi tutafanya hivyo (Nililenga kum-surprise baadae kidogo)

Baada ya miezi sita kupita katika uhusiano wetu, taratiiiiiibu binti
akaanza visa vya hapa na pale.
Kwakuwa nilimpenda nilijaribu kumsihi kuwa asiwe mapepe awe na subira
kwa kuwa siku zote mazuri hayahitaji pupa.
Hasa, Ukizingatia kuwa kuamua na kulikabili jambo ambalo tungedhamiria
kulienendea (Ndoa)
Si la kukurupuka,Tungehitajika kujipanga haswa.

Lakini binti aliona kama vile namchelewesha,
Akaongea mengi sana.
Na hapo ndipo nilipoanza kuyaona kwa kiasi makucha na rangi yake
halisi.

Nyodo zenye nakshi ya dharau kwa mbali vilitawala.
Nilijiaminisha kuwa kama hana Mtu anemtia kiburi (Kumshikia akili)
Basi atakuwa kapata bwana mtarajiwa aliemuahidi ndoa.

Mimi sikutaka wala kuhitaji sana marumbano, kwa roho safi niliachia
behewa likatike.
Moyoni Iliniuma, na nilisikitika sana lakini sikuwa na jinsi.

Yapata miaka minne sasa. Naweza sema kidonda na maumivu ya uhusiano
wangu na binti huyu vilishapona ingawa Naweza kukiri kuwa makovu bado
yapo na yananipa kumbukumbu mbaya juu ya uhusiano wangu na binti huyu.

Hata hivyo ni wikimbili tu zilizopita;
Huyu bi dada kaanza mawasiliano mfulizo na mimi mithili ya mvua za
masika.
Ni wazi yupo wanguwangu kama vile anataka kurudishia minyororo ya
behewa la uhusiano wetu ambalo alilikata yeye mwenyewe kwa mikono yake
mwenyewe.

Tumeongea mengi sana Lakini kikubwa kuliko yote.
Eti, Angefurahi kama tunge-spend weekend moja pamoja.
Nilipomuuliza ki-intelijensia kama hana mwanamme, akanijibu kifupi tu
eti, "I'm free like a bird and ready to mingle."
Hajui tu anazidi kunitia kichefuchefu.

Nakiri kuwa binti huyu aliniumiza, alinitesa na alinikera
Kwangu mimi anastahili adhabu na si ndogo.

Wakati bado naifikiria adhabu ya kumpa natoa nafasi kwa wanajopo.
Kama kuna mwenye adhabu ambayo anadhani ni stahiki kumpa huyu binti au
maoni ya nini nifanye pengine asisite.
kunipa.

NAWASILISHA.

remember am yr current. so usijishauwe na kupasha kiporo cha makande.
 
Hastahili adhabu yeyote. Acheni uzinzi sio kila siku kulia lia wakati matatizo mnayatafuta wenyewe. Mimi hata nikizini nikiachana na mwanamke siwezi kuanza kulia lia eti sijui kanitenda, sijui nimpe adhabu. Kwanza kakukosea kitu gani hasa??!!!
Kuelewa nako ni tatizo.
 
mkuu asikudanganye mtu,adhabu ya mwanamke kama huyo ni kutomjibu msg zake,kutopokea simu zake,kata mawasiliano aone hana thamani tena,huna haja ya kumdhuru ni kumpuuza tu,huwa inawauma sana
 
4 years away alikua ameweka plasta kwenye papuchi au ndo alikua anagawa kwa kila rika..?? angalia kijana asije akawa

ndo yeye anakuja kulipa kisasi kesho kutwa tukakuzika na kilo 5 narobo..halaf unachowaza sio ujanja!!!
Hili nalo neno, Ila sina lengo la kumuingia maungoni.
Kipau mbele changu kwa sasa ni kumpa funzo kutokana na maumivu aliyoyanibabisha awali.
 
adhabu kwa kipi sasa? mwambie hutaki baas...sasa kama aliona unamchelewesha afanyeje!!!
Okay, Nitafikiri na kuchambua ushauri wa wengine ukiwemo wa kwako kama itanifaa nitafanya usemacho.
lakini kumbuka si kila kosa lafaa kusamehewa, Nipe hata adhabu ndogo ya kumpa.
 
we mwenyewe wakati huo hukuwa tayari kuwa kwenye mahusiano serious na huyo binti, sasa alikuumiza kwa lipi? kama humtaki achana naye
 
Back
Top Bottom