Alinisaliti, nilichomfanyia hatokaa anisahau daima

Alinisaliti, nilichomfanyia hatokaa anisahau daima

Wakuu mimi ni member humu jamvini ila imenibidi kufungua account mpya ili niweze kuleta huu Uzi hapa,hii ni kutokana na kufahamiana na watu wengi kupitia account yangu ya siku zote. Nimeona hii ndio njia nzuri ya kueleza yangu ya moyoni bila kua na wasiwasi wa ku expose identity yangu...Nahisi uzi utakua mrefu ila mnisamehe maana mimi sio mwandishi mzuri.

Jumamosi iliyopita nikiwa katika matembezi ya hapa na pale katika fukwe moja hapa jijini,nimekaa na co worker napata juice ya baridi huku yeye akiisindikiza siku na castle light.wanaingia wanawake wawili mmoja mnene sana kimaumbile.wanaketi meza jirani kidogo na tulipo sisi,Ghafla nakosa amani,mapigo ya moyo yanaongezeka.. Nakua nawatazama sana hawa wanawake,ila wao naona hawa ja pay attention kwetu hivyo hawajatuona..baada ya muda huyu co worker ananiuliza kama kuna tatizo,najishtukia kidogo najikaza namwambia hamna tatizo lolote.ila kiukweli macho na akili yote imehamia kwa huyu mwanamke mnene,kila nikimtizama nahisi kumfahamu licha ya kutoonana nae kwa muda mrefu sana, ni jioni tulivu,anakuja muhudumu wanatoa oda,baada ya muda mhudumu anarudi na Smirnoff (vodka) club soda,glass mbili na vipande vya limao. Wanafungua wanaanza kunywa taratibu, muda unaenda nakosa uvumilivu namfuata huyu mwanamke, nafika walipokaa namshika begani,


"Habari yako???"
Ghafla anashtuka sana,Ananiangalia kwa muda kisha anainuka na kunikumbatia humu akitaja jina langu. Ananiachia na kunitizama tena kwa Mara nyingine,kisha anaanza kuniuliza
"Za masiku? Upo kweli? Mbona unazidi kua kijana?unafanya sana mazoezi eh?nimekutafuta sana mbona, blah blah blah + maswali mengi yasiyo na mwisho.
Mara ya mwisho namuona alikua binti mwenye umbo lililojengeka ipasavyo,nashindwa kuvumilia namuuliza " ndugu huu unene ni wa uzazi nini???anacheka anajibu hapana ni maisha tu.anaangalia mezani kwetu na kuhoji kulikoni mbona unakunywa juice unatumia dawa nini??natabasamu namwambia nipo kwenye dozi kweli(japokua si kweli)Tunaongea mawili matatu narudi mezani kwangu huku tukiwa tumeahidiana tutaongea zaidi maana bado tupo sana.


Huyu mwanamke ni nani????

August 2008, nafamiana na huyu msichana mrembo,baada ya urafiki wa muda tunaanza mahusiano ya kimapenzi. Mimi nafanya kazi katika shirika la kiserikali yeye akiwa mwaka wa pili chuo, baada ya muda mapenzi yananawiri sana ikafika hatua nikawa nimemtambulisha kwa baadhi ya ndugu jamaa na marafiki,katika kipindi cha mwaka na nusu hivi mpaka ilipofikia hatua anahitimu chuo kwa kweli kwangu alikua 'perfect woman'. Akaniteka haswa nikasahau habari za wanawake wengine kabisa, anahitimu chuo natumia influence yangu namtafutia kazi kwenye kampuni flani hapa hapa jijini, anaanza kazi na tunaanza kuishi wote.(japo kwao aliwaambia kua anaishi kwa rafiki wake wa kike)...muda unaenda huku mapenzi yakishamiri, asubuhi nampeleka kazini na mimi naenda ofisini,akitoka anakuja kunisubiri(ye anawahi kutoka) tunarudi wote nyumbani.


Baada ya mwaka tunaanza process za ndoa,hakutaka kuzaa kabla hatujaoana. Utaratibu wa kutambulishana unafanyika,ndoa inapangwa baada ya miezi nane kutokana na majukumu ya kikazi,kila mmoja ana furaha moyoni mwake. Nampa full power kwenye baadhi ya miradi yangu asimamie yeye..simfatilii huko kwenye hio miradi wala kuhoji financial status zaidi ya kumwambia awe makini maana nataraji kuanza ujenzi mwingine inaweza kufika mahali nikahitaji msaada wake..namuonea huruma anavyotoka kazini mapema na kuja kunisubiri mimi kila siku ya kazi, namfundisha kuendesha gari,anapata kauzoefu hatimaye siku yake ya kuzaliwa namfanyia surprise namnunulia gari.. Mipango ya harusi inaendelea pande zote mbili


Usaliti unaanza
Nikiwa sijui hili wa lile akaanzisha tabia mpya ya kuchelewa kurudi nyumbani, nikawa natoka kazini nampigia hapokei(hili halikunipa shida sana maana alikua si mzoefu sana barabarani hivyo akiwa anaendesha hapokei simu) nafika nyumbani simkuti,akirudi kila siku sababu mpya, muda si muda akaanza tabia anaondoka na gari asubuhi akirudi jioni anakuja kachelewa na gari haji nalo,analiacha kazini,sababu anazotoa yani nilikua hata sijielewi,Mara naona uvivu kuendesha,jioni sioni vizuri blah blah blah, alikua na mdogo wake kaanza 1st year udsm pale akamfanya kama cover story yake, kila akichelewa anadai alikua nae anampa company.simu zangu akawa mgumu sana kupokea,akabadilika ghafla. Kuna siku kachelewa kurudi,nimekaa sebleni nakunywa whisky na kujisomea kitabu Fulani,alivyofika akaniambia Ana akshi sana twende chumbani, baada ya mambo mambo ile nataka kuingia ikulu nikahisi kabisa hii ikulu imedukuliwa na wajanja,the thing is am old enough na huyu mwanamke namjua sana so nika notice something haipo sawa hapa.nikakaza moyo konde nikaingia mchezoni japokua akili haikuwa sawa kabisa. Bado kama miezi minne ndoa inakuja,maisha yamebadilika, ye anawahi kutoka kazini ila kufika nyumbani kila siku ananikuta mimi, nyumbani hapiki kuna mahali akawa anapitia chakula karibu kila siku(napajua)

Nikaanza upelelezi, sina tabia ya kugusa simu yake na sikuona sababu ya kuanza kufanya hivyo,kuna siku nampigia,after kama missed call 5 anapokea,ni SAA 3 usiku hajarudi nyumbani,namuuliza alipo ananiambia bado bado kuna foleni,basi namwambia ptia chakula anasema haya,nawasha gari naenda hii sehemu anapochukulia chakula napaki kwa mbali kidogo najibana mahali nakunywa bia yangu taratibu,muda si muda anaingia my wife to be na kijana mmoja,wanafungiwa chakula wanaenda parking,jamaa anamtolea mkoba kwenye gari kisha wana French kiss jamaa anaondoka wife anachukua bajaji anaondoka pia. Hapa ndo nikaelewa kwanini gari analiacha kazini,after work kuna MTU anakuja kumchukua.

Naamini humu tu watu wazima na kila mmoja wetu anafahamu hisia za usaliti zilivyo hivyo sihitaji kuelezea.. Narudi baanyumbani SAA 9 usiku nikiwa nimelewa sana,nafika nalala sebleni huku wife to be akijifanya analalamika sana,najitahidi kumpuuza,kesho yake nashindwa kwenda kazini.simuulizi chochote,, baada ya siku mbili anarudi kachelewa,baada ya kumkiss nagundua amekunywa, ndugu nlikua sijawahi kumpiga mwanamke maishani mwangu ila hio siku nilimpa kichapo vijana wa sasa hivi wana msemo wao kua 'sio cha nchi hii' yani pombe ikakatika akanieleza anavyogawa uroda a-z!!! Nikasaidiana na mlinzi tukampeleka hospitali maana alipasuka ikabidi wamshone bila ganzi maana alikua amekunywa pia.kesho yake baada ya kujadiliana tukawasiliana na pande zote mbili harusi isogezwe miezi minne mbele kutokana na sababu mbalimbali.p


Time for revenge
Nlijitahidi sana kumsamehe lakini sikuweza,akawa mnyenyekevu kupita kiasi lakini moyo wangu ukakataa kabisa,sikumwambia MTU yoyote na mipango ya harusi inaendelea, nikawa chapombe,si kazini si nyumbani pombe akawa ndo rafiki yangu.. Sina hisia na huyu mwanamke tena,kilichobaki na kumfanyia kisasi kisha nimuache(sina moyo wa kusamehe,I tried but it didn't work).kila aina ya kisasi naona kama hakitoshi,I went crazy kuna muda nlitamani ata kumuua yanii... Nakaa naye namwambia achukue likizo ya bila malipo twende vacation ya kimya kimya kabla ya harusi tuone ni jinsi gani tunaweza rejesha penzi..naongea na bosi wangu(long time friend) namwambia a-z bila kumficha, kuna nafasi zilitoka kwenda kuongeza ujuzi nje pale kazini sikufatlia maana ziliingiliana na ratiba ya harusi,tuka force na bosi pale akanichomeka. Nikatumia ka ushawishi kidogo kwenye hii kampuni ya bidada wakampa ka likizo japokua kishingo upande sana


Vacation inaanzia unguja na huyu mwanamke,mi napanga kisasi tu,ye anajua tunaenda tafuta muafaka,nshakua pombe MTU hapo... Kwa kifupi Mwezi mzima tulitembea mikoa kadhaa hapa nchini,katika kipindi hiko chote sikuwahi kupata hisia nae tena,nlimpa tabasamu la kinafiki muda wote. Tulipokua znz mwanzo wa vacation nikamshawishi sana nianze 'kuruka ukuta'(samahani kama ntamkwaza MTU hapa) anakua mgumu ila baada ya ushawishi na influence ya pombe anakubali. Yani nlikua simjali hata kidogo,akawa Analia kila siku kua namuumiza lakini nikawa nampoza kinafiki,mwezi mzima nikamfanyia uchafu bila huruma.

Tunarudi jijini,naenda kwa mama namwambia kua Hamna mke pale wala ndoa,naanza maandalizi kimya kimya ya kwenda nje,narudisha usamamizi wa miradi yangu yote,siku si siku bidada yupo kazini nabadilisha lock za milango,natoa kila chake nampa mlinzi na kinote ampe kikiwa na maneno machache tu. Nakaa kwa boss kwangu siku mbili naenda nje

Nakutana na binti wa kitanzania(RIP) nje,nae kachoshwa na mahusiano,tunasaidiana 'kupambana na baridi la ulaya' katangulia mbele ya haki Ila kaniachia zawadi ya mapacha(boy and a girl). Ni mwaka wa pili tangu tumzike na ilikua ndio siku yangu ya mwisho kunywa pombe!!!!!

Maisha yanasonga,sitaki kusikia habari za kuoa maana najua sina moyo wa kusamehe na maisha ya sasa ndo mwendokasi kwelikweli. Sasa hivi watoto wangu ndo dunia yangu, +work and gym.
Eway huyu mwanamke jumamosi alinipa namba ila nikazifuta,maisha safari ndefu wakuu. Poleni kwa Uzi mrefu

The best revenge is forgiveness, don't follow my path
Nimejifunza somo fulani kupitia story yako mkuu, RIP mama wawili.
 
Karanja I am no way glorifying or agreeing with what mchumba wake put him through but...........umemsikia mwenyewe kuwa pamoja kumharibia dada wa watu utu wake na michezo ya ajabu, he left her high and dry katikati ya maandalizi ya harusi, with no closure and a homeless! Sasa kweli ni nani wakutakiwa kumuogopa mungu hapa!!!
Karanja I am no way glorifying or agreeing with what mchumba wake put him through but...........umemsikia mwenyewe kuwa pamoja kumharibia dada wa watu utu wake na michezo ya ajabu, he left her high and dry katikati ya maandalizi ya harusi, with no closure and a homeless! Sasa kweli ni nani wakutakiwa kumuogopa mungu hapa!!!
Mkuu nemo,here we go Again!! There is no way I can justify what i did,, but at least had to get even!!! Kumuharibia utu??? Cmon cut Me some slack, sleeping around miezi miwili pre marriage yani Huyo MTU ana utu kweli??? Eway I had two options
a)ruin myself and become a drunkass destroying my career all along as I continue trying make her happy
b)do what I did


Sadly I'd go with option b) anytime of the day
 
Sir, I beg to respectfully differ ! Please know, this is not true. Ke na Me wote ni binadamu. Kwenye maswala ya moyo we feel the same as you guys,if not more. Ni kuwa labda tolerance level yetu ni kubwa kuliko nyie.
Naweza kubaliana na wewe kwenye tolerance,upande mungine mwanamke anapata nafuu zaidi akipozwa na kuaahidiwa kosa halitarudiwa,sababu mwanaume anaweza akaoa wanawake wengi,lakini mwanamke hawezi kuolewa na wanaume wengi.
 
fresh tuu...ulivyomfanyia.... ...yaani wewe umnunulie gari yeye akampe bwana ake... ??..shenziiiii kabisaa.....
 
Sir, I beg to respectfully differ ! Please know, this is not true. Ke na Me wote ni binadamu. Kwenye maswala ya moyo we feel the same as you guys,if not more. Ni kuwa labda tolerance level yetu ni kubwa kuliko nyie.
Am with you in this one
 
fresh tuu...ulivyomfanyia.... ...yaani wewe umnunulie gari yeye akampe bwana ake... ??..shenziiiii kabisaa.....
Mkuu gari hakua anampa bwana wake bali alikua analiacha kazini wanatumia la bwana wake!! Haha
 
Story yako ni nzuri ila kwangu imeingia dosari the way ulivyofanya kulipiza kisasi. Kuhusu kuamua kukaa pweke ni maamuzi ila katika maamuzi hayo usichanganye na tamaa ya kuchukuwa na kubadilisha wanawake. Inawezekana na nakuunga mkono wengine tunaenda mvua ya tano sasa. Faraja pekee imebakia watoto.
 
Hawaridhiki kwa kuwa wanaume wasioridhika wanahangaika usiku kucha kuwasumbua.
E.g. mimi nina jamaa anataka kumnyang'anya mke wake Rav 4 anipe mimi. Mimi na yeye nani hajaridhika?
ktk akili ya kawaida na wewe unashabikia hilo...??...
 
I am so sorry for what happened to the mother of your children. May God rest her soul in eternal peace, and thanks for sharing this info.

The most open-minded woman I ever met,nimejifunza mengi kutoka kwake. Nilikutana nae nje akiwa anafanya masters yake,baada ya kuzoeana I told her my story!!! She'd usually say 'gym is the best therapy' tukawa tunafanya sana mazoezi at free days!!! Baada ya mwaka tukaanza intimate relationships(no string attached)...alikua nae kashapitia mengi hakutaka mahusiano

Well we had our twins, huku tukawa tunafanya kazi mikoa tofauti, I would spend every weekend with my family until she passed away,had a horrible car accident. We never took it further as she always considered me as a beloved friend and her kids dad(hii kitu ni ngumu kuelewa but we had the strangest relationship)

Deep down I knew that she loved me,maybe would have been married by now(who knows??) She means a lot in my life and making this twins happy is what I can do to repay her
 
mkuu pole sana..
hata mimi kuna kitu huwa kinanisumbua kichwa

>huwa napenda niwe na
familia baadae
>lakini naogopa sana
kuoa

maana visa vya ndoa au mahusiano kwa ujumla huwa ni tishio kwa kweli maana kila nikijaribu kugeuza visa vya wenzangu viwe vyangu huwa napata uwoga sana wa kuthubu hata kujaribu.
ishi kiseja....maana ukiwaza hivyo...useja ndio suluhisho....
otherwise...u' must be in.....broh.......ili neno familia litimie.....
 
Pole sana wanawake kuna muda hatueleweki tunataka nini, mtu kakupa kila kitu anakuonyesha mapenzi yote lakini unamsaliti sijui huwa ni pepo gani aisee
mmeumbwa hivyoo... ...sasa wacha twende hivyohivyo kindavandava....mlichonacho tunakihitaji sana....lazima tuwatumie...
 
Kweli,the lady was left outside alone,but the guy was sick and tired of her because of her betrayal,unajua mwanamke akisalitiwa ni less painful kuliko mwanaume akisalitiwa,sisi wanaume ndio providers since stone age,na pia sisi ni kings in our own castles,sasa jiulize,mimi mwanaume muoaji na kiongozi wa familia,nagundua mwanamke wangu ana bwana mungine? daah ni bora mauti yanikute nife nisipate huo uchungu,mwanamke kwenda na bwana mungine ni donda kwa mwnaume kuliko misiba yote duniani.

Unasema mwanamke akisalitiwa ni less painful kwake? Kwa kuwa yeye ana moyo wa jiwe ama hana hisia? Ila nyie mkisalitiwa ndo panauma kwa kuwa mna mioyo ya nyama sio? Endeleeni kusaliti, wanawake nao siku hz wameamka, wamechoka kufanywa wajinga. Ukimsaliti huku na yeye anakusaliti kule. Sasa ukijua unasalitiwa kunywa maji ushushie... Usaliti unauma pande zote. Usijidanganye eti kwa mwanamke ni less painful
 
I am so sorry of what happened to the mother of your children. May God rest her soul in eternal peace, and thanks for sharing this info.
Mkuu BAK this is the best only being am missing in my life, kila nikiwa gym hua namkumbuka, she use to tell me tukiwa gym.... "Man, u don't stop when you are tired,u stop when you finish all your reps"
Let her rest in peace
 
safi sana mkuu,namna ulivoandika inaonyosha ukomavu uliotukuka na upeo wa hali ya juu uliokuwa nao wakati wa kukabiliana na dhoruba iliyokukumba sio kama wajinga wengine ati wanakimbiliaga kuua. na zaidi hapo ulivoifuta namba yake duh tungekuwa tuko watu 5 kati ya mia kama ww(na mimi nimoo) hii nchi ingekuwa mbali sana hii sio kulialia tuu na kulepa upopoma wa kukumbushia!
 
Aisee.! Pole sana Mkuu..

And una moyo sana mkuu! Ingawa ulimshushia kipigo lakini walau ulikumbuka kumpeleka hospitali, maana sitaki hata kuimagine kile kitu ambacho ningefanya kwenye situation kama hiyo..

Mungu atuepushe na hili lisitukute..
utaalamu waliojaliwa wa kuchanganya ukatili na huruma kwa wakati mmoja....ndio inawacost mkuu....
 
Back
Top Bottom