A lot of sense;
ITAKAVYOKUWA
Ikiwa watu wataendelea KUGOMA kupeleka USHAHIDI kwa TUME; basi TUME itakuja na RIPOTI kwamba; “HAKUNA USHAHIDI WA WATU KUULIWA 29 OKTOBA 2025”. Watu wakimwaga UGALI, Tume itamwaga MBOGA na MAJI YA KUNAWA
Itatatua tatizo/mgogoro wa serikali na wananchi uliopo au ndio tu itauchochea moto zaidi?
The big problem here, nionavyo mimi, ni kama vile wananchi wanashindana na serikali yao kwa jambo ambalo liko very clear. Na kwamba kuna upande UTASHINDA na mwingine KUPOTEZA wakati nchi na taifa na watu wake wote tumeathirika
UKweli ni kuwa:
Watu wameuwawa na vyombo vya dola; Polisi & TISS na mali kuharibiwa. Huu ndio ukweli usioweza kupakwa rangi ya uongo wowote kuubadilisha hata kama tume hii itakuja na manipulations zake kujaribu kuwapa nafuu ya lawama na adhabu tunaowajua kabisa ndio wahusika yaani
CCM, Serikali yao (Polisi, TISS, vyombo vingine vya dola ikiwemo mahakama na bunge na zaidi Samia Suluhu Hassan aliyekuwa Rais wakati uhalifu unatokea!!)
Ikija na mawazo kama asemavyo Peter Madeleka kwa macho ya "kisheria" yaweza kuwa YES lakini kiuhalisia sio kwa sbb mgogoro uliopo (SERIKALI vs WANANCHI/UMMA) katika hatua hii hautatuliki kisheria. Na kwa maana hiyo, Tume ikija na conclusion hiyo, basi watakuwa wamefuja pesa zetu tu kwa miezi mitatu kwa sbb it won't help anything!
At this juncture, kila mtu anataka majibu ya maswali haya toka kwa Tume hiyo pamoja na kuwa ilishapingwa hata kabla haijaanza kazi kwa sbb ya kukosa "
moral authority" kufanya kazi hiyo;
1. Chanzo cha mauaji haya na uharibifu wa mali ni nini?
👉Je, ni kweli ni Mange Kimambi na Maria Sarungi na wanaoitwa "wanaharakati?" How?
👉Je ni vijana wetu maarufu kama
Generation "Z" kifupi
GenZ? How?
👉Je, ni Tundu Lissu au John Heche au CHADEMA kama Habib Mchange wapiga propaganda wengine wasemavyo? How?
👉Je, ni CCM, Rais Samia Suluhu Hassan, Polisi, TISS au JWTZ? How?
👉Je, ni mahakama na Bunge kushindwa kusimama ktk nafasi zao? How?
👉Je, ni Tume ya Uchaguzi kuharibu uchaguzi kwa kutengeneza matokeo feki kuipendelea CCM na kupora mamlaka ya umma kuchagua viongozi wawatakao? How this happened?
👉Je, Utekaji na mauaji ya raia yaliyoanza tangu mwaka 2017 kwa jaribio la kumuua Tundu Lissu na kutekwa kwa Ben Sanane? How?
👉Au Je, ni Askofu Josephat Gwajima na kanisa lake lililofutiwa usajili na ghafla from nowhere likarudishiwa lakini baada ya tendo la mauaji kufanyika? How?
#Tume ijibu swali hili muhimu genuinely bila ulaghai linalozaa maswali yote hayo hapo juu👆
#Kwamba:
NI NINI CHANZO NA KWA NAMNA GANI EXACTLY? Wasijaribu kutufanya wananchi mabwege hata kidogo. We want the truth of this matter that will linger our ears without doubt 🧐
2. Nani alipanga na kutekeleza mauaji haya?
3. Kwanini waliua watu maelfu? What were the motivating factors for this massacre/genocide?
4. Hatua gani za
kisheria na
kisiasa zichukuliwe kwa waliotenda uhalifu huu dhidi ya binadamu?
5. Hatua gani zichukuliwe kuzuia hii kitu isitokee tena huko mbeleni?
#Kama Tume itakuja na ripoti yoyote isiyo na majibu ya maswali haya, itakuwa imepoteza muda na fedha za umma bure kwa miezi mitatu na wao watakuwa ni tatizo jingine pia litakalohitaji kutatuliwa!!