Alichojitabiria Zitto kimemtokea haraka

Alichojitabiria Zitto kimemtokea haraka

Kitila Mkumbo ametupotezea kijana wetu kwenye ramani.
 
Imeshakula kwake mwache ajutie maamuzi yake
 
Imeshakula kwake mwache ajutie maamuzi yake

Haya maelezo ya Tabby kumhusu Zitto yamenikuna sana. Nimeona niyakopi tena hapa. Kkwa wale ambao mlikuwa hamjui, tatizo la Zitto ndio hili hakuna kingine! Anapenda KUABUDIWA, KUPIGIWA MAGOTI. Bila shaka ndio maana ACT wakijua hilo wakampa uspreme leader ili asiwe chini ya mtu mwigine. Tabby kamcharacterise Zitto ifuatavyo:

Zitto yuko talented lakini hayuko organized, hajielewi na ametawaliwa zaidi na ubinafsi, kiburi na show!. Zitto unaweza kumhamisha kwenye mission yake kwa kumsifia na kumpamba. Ameonyesha kukosa sifa za uongozi kwa sababu haonyeshi nia ya dhati ya kufikia malengo wala uchungu wa kutokufikiwa malengo.

Hayuko tayari ku sacrifice personal interests kwa maslahi ya public ambayo baadaye ingemlipa satisfactions mara mia na historia ya nchi siku zote ingemtaja kuliko kiburi, maringo na kujaribu kuharibu maslahi ya umma bila chembe ya hisia. Anaamua kusaliti mission kwa sababu tu amekosa kuabudiwa kwa kiwango anachotaka ama amepata recognition kubwa hata kama ni flattering upande pinzania, na hivyo kuwa tayari kuwageuka na kuwaua Watanzania wote ili mradi atumikie kundi haram linalomsifia hata kama ni kwa njia haram.

Baada ya matusi kwa ukawa, anataka kujiunga nao ama kwa kuwa anahitaji kuendelea kuwa ndani ya adui ili aweze kummaliza vizuri, ama anajisikia kusalitiwa na waliokuwa wanamwabudu kwa kuwa hawezi kufanya madhara zaidi kwa CHADEMA na sasa UKAWA na hivyo anaamua kuwageuka, au anarudi baada ya kuona anakuwa mpweke kwa kutengwa na hivyo anatafuta peers, au inaweza kuwa sababu yoyote.

Lakini katika mazingira ya vita vya ukombozi, watu kama Zitto hakuna mtu generali mwenye akili timamu anaweza kuwaamini kwa lolote kwa sababu hawaaminiki. Zitto amejidhirisha ni namna gani hawezi kuthamini wala kujali commitments. Ni mtu irresponsible na hawezi kuwaza mara mbili kabla hajaamua kusaliti haki kwa sababu kwake KUSIFIWA NA KUABUDIWA ndivyo vya kwanza, mengine hayana thamani.

NINAOMBA UKAWA, KAMA KUNA SABABU YA KUMJIBU, NINASHAURI MU ACKNOWLEDGE RECEIPT YA MAOMBI YAKE, LAKINI MWAMBIENI MTAJIBU MWAKANI KWA SASA MNA TIGHT SCHEDULES KIASI CHA KUKOSA UWEZEKANO WA KUINGIZA mchakato wa USAJILI WA WANACHAMA WAPYA WA UKAWA
 
tumpe muda wadau! yaan mwezi mmoja tu mumesha pata hitimisho lake!
 
wabunge hamsini kutoka cdm na ccm watajiunga act wazalendo dah!!
 
Mrema hakujenga chama bali alikuwa na ufuasi, kujenga chama ni kuwa na mtandao kuanzia kitongoji cha mwisho nchi hii hadi Dar
Namaanisha Mrema alipata umaarufu mkubwa uliodumu kitambo
 
ACT haifanyi siasa ya show tulikitaa kuwapandisha watu majukwaani siasa hizo tunawaachia wao

Na yule mvuta bangi wa moro mliezunguka nae mikoani alikuwa anafanya nini majukwaani!! nasikia ndio mgombea wenu pekee wa ubunge moro mjini....aisee mnakazi kweli!!!!
 
Mwaka jana mwishoni Zitto alifanya mahojiano na gazeti la mwananchi na alihojiwa mambo mbali mbali likiwemo la mstakabari wake kisiasa. Mwandishi pamoja na mambo mengine alitaka kujua Zitto kwa nini asihame toka Chadema na kuhamia vyama vingine. Zitto alisema kuhama chama siyo jambo rahisi, akasema ukihama chama utapata headlines za magazeti kwa wiki mbili mpaka mwezi mmoja alafu unakufa kisiasa.

Kiukweli alichotabiri Zitto ndicho kilichomtokea, baada ya kufanya ziara ambayo haikuwa na mafanikio makubwa pamoja na kuhudhuriwa na watu wengi. Zitto alipata headlines kweli kwenye magazeti na mitandao ya kijamii, lakini baada ya mikutano hiyo Zitto hasikiki tena. Mikutano yake mikubwa sijui kama ilikuwa na faida maana alishindwa kumchukua hata mwenyekiti wa mtaa awe wa Chadema hata CCM.

Nashawishika kukubaliana naye kwamba alichokuwa anaogopa 'kupata headlines za wiki mbili na kufa kisiasa' alikuwa sahihi kabisa. Kujenga chama si mchezo, hata angepewa miaka mitano kujenga chama chake Kigoma tu bado ni kazi ngumu sana. Zitto ni kijana ninayemwamini kwamba ana akili na uwezo mkubwa, ilikuwaje akaingia mkenge wa wapiga dili kwamba wanaazisha chama ambacho 'eti' wabunge wengi watajiunga nacho baada ya bunge kuvunjwa? Si amuulize Mpendazoe alivyoingizwa mkenge na CCJ 2010?

Zitto ni mfano wa kuigwa kwa kuthubutu kwake hivyoo vijana tusiogope kukataa ukandamizaji kwa misingi ya kupoteza tonge!! na hata ilichofanya na ilipofikia huwezi kunishawishi kwamba hakuna mafanikio kabisa!!! hizo ni poroja za mchana kweupe ambazo mwisho wake hazidumu zaidi ya week moja.
 
Red: Ndilo jambo ambalo mnalikwepa kulikubali ila litabaki hivo koz ndio ukweli.
Kwa mtu makini anayemjua Zitto hakai akianzisha thread utumbo kama hizi bali ni kusubiria his next move pamoja na ACT katika kuirudisha nchi katika misingi.Karibu ACT-Wazalendo.

Ndoto zitaendelea kuitwa ndoto hata kama zitaotwa mchana wa SAA 8.
 
Zitto ni mfano wa kuigwa kwa kuthubutu kwake hivyoo vijana tusiogope kukataa ukandamizaji kwa misingi ya kupoteza tonge!! na hata ilichofanya na ilipofikia huwezi kunishawishi kwamba hakuna mafanikio kabisa!!! hizo ni poroja za mchana kweupe ambazo mwisho wake hazidumu zaidi ya week moja.

Labda utusaidie ZZK na ACT wamefanya nini? mikutano siyo kujenga chama ni kuhamasisha tu.
 
Back
Top Bottom