DELETED ACCOUNT
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 9,805
- 15,470
Tunaojua Sanaa ya Vita tunajua kamwe usiruhusu adui yako akakuchagulia silaha. Daudi alipoingia uwanja wa vita kumkabili Goliath alikataa kuvaa na kubeba silaha alizopewa, akalazimisha kwenda na vikokoto vyake alivyovizoea kila siku. Watu wakamshangaa huyu vipi, ana akili kweli? Mwisho wa siku wote tunajua nani alilazwa chini.
Bado hatujajua hatma ya mechi ya pili ya fainali kati ya Simba na Berkane na inawezekana kabisa kwamba mechi inaweza kuchezwa Zanzibar na Simba kibishibishi ikachukua ubingwa ila narudi kule kule, kamwe usikubali adui yako akakuchagulia silaha ya kupambana naye.
Kama ile barua ya kuongea na Algeria watupe uwanja ni kweli, ni sahihi kabisa kwenda huko. Hapo tunaongea na serikali ya Algeria wasiruhusu mdudu yoyote shabiki wa Belkane kuingia kwenda kuangalia mechi, sisi tunajivua lawama zote za kitakachotokea huko. Na jezi zao zile zenye bendera ya Morocco hawataruhusiwa kuzivaa ndani ya Algeria. Fainali ichezwe bila mashabiki tuone kama hao CAF watafurahi.
Mwisho wa siku ni lazima tuheshimiane.
Bado hatujajua hatma ya mechi ya pili ya fainali kati ya Simba na Berkane na inawezekana kabisa kwamba mechi inaweza kuchezwa Zanzibar na Simba kibishibishi ikachukua ubingwa ila narudi kule kule, kamwe usikubali adui yako akakuchagulia silaha ya kupambana naye.
Kama ile barua ya kuongea na Algeria watupe uwanja ni kweli, ni sahihi kabisa kwenda huko. Hapo tunaongea na serikali ya Algeria wasiruhusu mdudu yoyote shabiki wa Belkane kuingia kwenda kuangalia mechi, sisi tunajivua lawama zote za kitakachotokea huko. Na jezi zao zile zenye bendera ya Morocco hawataruhusiwa kuzivaa ndani ya Algeria. Fainali ichezwe bila mashabiki tuone kama hao CAF watafurahi.
Mwisho wa siku ni lazima tuheshimiane.