Alfajiri ya furaha kubwa! RIP DR. FUPI

Kuna jamaa nahisi ni mtu wa kitengo, tulikiwa tunapiga hii stor akaniambia sasa hivi mitandao ya ya kijamii inasababisha habari kusambaa kwa kasi sana, ila akasema hiyo haiwezi kuwazuia kufanya kazi.

Nikamwambia ila hili tukio selikali imefeli kwa jinsi lilivyoenda,

Akaniambia selikali haijwahi kufeli, kwa maneno mengine kitengo hakijawahi kufeli.
Ni maneno ya kujifariji tuu, imefeli maranyingi tu ila inatumika PLATFORM maalum ku rescue mambo... Ipo platform maalum kwa ajili ya kuokoa jahazi pale mambo yanapoenda mrama.... Na hii ndio inapaswa kushukuriwa daima
 
Ni maneno ya kujifariji tuu, imefeli maranyingi tu ila inatumika PLATFORM maalum ku rescue mambo... Ipo platform maalum kwa ajili ya kuokoa jahazi pale mambo yanapoenda mrama.... Na hii ndio inapaswa kushukuriwa daima
Duh.. Basi kazi ipo,
Q
 
Mkuu Mshana Jr hebu weka wazi kidogo..
Kwann umeandika maada hii Leo baada ya kupatkana kwa Mo?

Je hyo kampuni iliyokuwa imeagiza Michele ni kampuni gani?
Mmiliki wake ni nani?
Nakumbuka hilo tukio kampuni iliitwa M.E.T.L wakati ule haikuwa na kirefu.
 
Alfajiri ya leo tarehe 20.10.2018 imepokelewa na watu wengi kwa furaha kubwa baada ya kuenea taarifa za kupatikana salama mfanyabiashara kijana bilionea Mohammed Dewji... Ni furaha kwa familia, ndugu jamaa na marafiki na wale wote wasioamini katika udhalimu.....

Mwishoni mwa utawala wa rais Ali Hassan Mwinyi (CCM) mwaka 1992--->93... Lilitokea jambo baya sana lililoitia nchi yetu DOA kubwa sana... Mauaji ya kutisha ya Dr. Fupi aliyekuwa mkemia mkuu wa serikali kipindi hicho... Uzalendo wa nchi yake... Utu wema wake, uamunifu na chuki dhidi ya rushwa vilisababisha maisha yake yakatishwe... Akiacha mjane na watoto wawili
Udhalimu, uchoyo, ubinafsi kukosa huruma, hamu kubwa ya kupata kuliwafanya watu wanaojifanya watu Mungu sana kusahau utu wao na kufanya ukatili mkubwa kwa mtu aso hatia! Wakaichukua roho yake mchana kweupe, na kuiachia familia yake majonzi makubwa na machozi ya milele!

Nini kilitokea!?
Kulikuwa na kampuni moja iliyokuwa inajishughulisha na uuzaji wa nafaka... Kampuni hii ilikuwa na mabohari makubwa hapa DSM... Basi kukawa na uhitaji mkubwa wa mchele na ngano kipindi hicho, na kampuni husika ikaingiza tani za kutosha ili wananchi wapate chakula na kampuni ipate pesa
Mchele ule uliingizwa toka uarabuni kupitia Zanzibar nadhani.. Habari zikavuja kwamba mchele ule haukufaa kwa matumizi ya binadamu, ulikuwa umeshaharibika... Kuthibitisha tuhuma hizi ikabidi mkemia mkuu wa serikali aitwe kuupima...!
Mkemia akafanya kazi yake kwa uaminifu na weledi mkubwa akishirikiana na senior lab technician mmoja... Hawa wawili wakaheshimu kiapo chao cha kazi.. KUTENDA KWA WELEDI NA UAMINIFU... Dr Fupi akatoa majibu yake kuwa mchele ule haufai kwa matumizi ya binadamu, yoyote ayakayeutia atapata madhara makubwa ya kiafya yajayo taratibu....
Wenye mali wakapingana na majibu ya mkemia mkuu wa serikali... Malumbano yakaanzia hapo, vitisho nk... Lakini Dr Fupi akashikilia msimamo wake!
Mwishoni mwa wiki ile ya malumbano Dr Fupi akiwa nyumbani kwake akapata ugeni.. Kuchungulia getini akaona hawa si watu wema kwakuwa walikuwa wanaparamia ukuta... Dr kwa haraka akaomba msaada wa polisi wa vituo mbalimbali (alikuwa anaishi Oysterbay)
. Kituo no moja simu ilikuwa busy
. Kituo no mbili gari haikuwa na mafuta
. Kituo no tatu kilipokea wito lakini wakafika kwa kuchelewa kidogo...
Watu wale wabaya waliingia ndani kwake kwa kuvunja mageti na milango na wakamkuta Dr akiendelea kuomba msaada.. Walimkatakata mpaka akakata roho.... Wakaondoka bila kuchukua kitu chochote...
Wiki iliyofuata msaidizi wake akakaimu nafasi yake na kutoa haraka cheti cha ubora wa mchele husika na bidhaa husika ikaingizwa sokoni, huku familia ya Dr Fupi ndugu na jamaa wakiwa kwenye majonzi makubwa ya kumpoteza baba yao... Yule senior lab technician pia alikufa inasemekana kwa sumu....
Kampuni husika ilituhumiwa sana kwenye hili lakini wakati huo Mzee Malecela akiwa mwenye nguvu kubwa akalimaliza ajuavyo yeye....

Maneno ya Mungu yanasema ni rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuurithi ufalme wa mbinguni.. (Ngamia sio mnyama ni lile kamba kubwa la kushikilia chombo kinapoweka nanga ufukweni ama baharini)
Mbele ya nuru ya mafanikio ya matajiri nyuma yake kuna giza lililojaa udhalimu tupu.....
Ngazi za kuwafikisha watu wengi kwenye kilele cha mafanikio ya kibiashara zimeshikiliwa na mafuvu na mifupa ya wahanga wengi sana!

Ni weekend ya furaha MO kapatikana.... Ni weekend nyingine ya huzuni kubwa kwa familia ile ya Dr Fupi iliyopokwa mpendwa wao hali wakiwa bado wanamhitaji sana... Nitamlilia daima shujaa huyu wa uzalendo asiyekumbukwa popote!
mshana mungu unayemuamini akubariki sana sana sana
 
Kuna jamaa nahisi ni mtu wa kitengo, tulikiwa tunapiga hii stor akaniambia sasa hivi mitandao ya ya kijamii inasababisha habari kusambaa kwa kasi sana, ila akasema hiyo haiwezi kuwazuia kufanya kazi.

Nikamwambia ila hili tukio selikali imefeli kwa jinsi lilivyoenda,

Akaniambia selikali haijwahi kufeli, kwa maneno mengine kitengo hakijawahi kufeli.
Watu wa kitengo ilikua enzi za Mwalimu na Mwinyi kidogo. Siku hizi ma dogo wanatamka LIVE mbele ya watu kuwa wako usalama. Enzi zile mtu wa kitengo anajifanya fundi magari au fundi ujenzi au anauza bar. na huyo barmaid ni simple hata ukiomba mzigo unapewa tu. sema siku zile ule ujinga wa mtandao wa tigo ulikua hakuna
 
Back
Top Bottom