Anga linaongea uwepo la turubai lingine kubwa

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,916
Siasa majnuni zimetufundisha unafiki, uzandiki na rohombaya. Kuna turubai lingine laja
EL kaumwa na kuugua sana! Je, ni wangapi tulimwombea yeye na wagonjwa wengine wote? Watu wako busy na nyama choma na bia na zipu. Leo kila mmoja anakuja na machozi yake ya mamba! Wanafique wakubwa nyie

Zamani bibi yetu alifariki. Kifo chake kulikuwa sherehe kwakuwa hatimaye alipumzika tabu za dunia.. Alitwaliwa toka maisha haya akiwa na umri wa takribani miaka 121 hivi.

Miaka yake ya mwishoni alikuwa kama mtoto ni wa kubebwa muda Wote hawezi kusimama hawezi kutembea hawezi kula mwenyewe nk bila usaidizi

Mwanzoni hali hiyo ilimuumiza sana.. Mtu aliyezoea kufanya shughuli zake mwenyewe leo hawezi mpaka asadiwe.

Maisha yake yaligeuka ghafla na kuwa na kuwa mageni kwake, ndugu na marafiki wa kukumbushana mambo ya zamani, utoto wao, ujana wao nk! Wote hawakuwepo walishatangulia mbele za haki miaka mingi nyuma

Alitawaliwa na upweke mkubwa hakuna na watu wa kuongea naye, wa kuwa karibu naye. Kusimuliana mengi. Waliokuwepo walimfanyia kila kitu kwa upendo mkubwa lakini hawakuwa sehemu ya past yake!

Siku anaondoka duniani ilikuwa furaha badala ya huzuni. Kayaishi maisha yake.. Kaolewa na kujaaliwa watoto wengi wa kike na wa kiume! Wakasoma na kupata Kazi kisha wakapata na familia.

Akajaaliwa kuwaona wana wa wanawe.. Wajukuu vitukuu na vining'ina.. Mungu akupe nini tena.. Siku anafumba macho milele uso wake ulijawa na amani na tabasamu la ujanani.. Huku akiwa kazungukwa na wanafamilia waliokuwepo! Ni baraka kubwa!

Hakuna kitu chema kama afya na hakuna kitu kibaya kama ugonjwa hasa wa muda mrefu. Ugonjwa huharibu bajeti zote na ratiba zote! Ugonjwa hupangiwa bajeti yake mpya na wahudumu.. Ugonjwa huleta simanzi na majonzi ndani ya familia.

Siku MOJA ya mgonjwa aliyelala kitandani hajiwezi ni ngumu na ni ndefu kuliko hata ya wanaomhudumia

Mtu aliyeishi maisha yake kwa mafanikio makubwa kijamii, kifamilia, kitaifa, kimataifa, kifedha, kiimani nknk kama EL na mwishoni kupata udhaifu wa kimwili kwa muda mrefu. Siku akitwaliwa toka maisha haya inapaswa kuwa siku ya furaha kuu na si unafiki mkubwa wa wanasiasa kwamba.

. Wamepokea kifo chake kwa nshtuko mkubwa
. Taifa limepoteza mtu muhimu sana
. Pengo lake hakuna wa kuliziba nknk

Wengine wanaandika haya wakiwa kwenye dhambi za dunia na divai mkononi. Kama ratiba za maturubai hazitaingiliana basi tujifunze kuacha unafiki na machozi ya mamba.


Sanaa ya kifo
 
UMENIACHA NJIA PANDA

Mgonjwa mmoja alimgeukia daktari wake alipokuwa akijiandaa kutoka katika chumba cha uchunguzi na kusema, "Daktari, naogopa kufa. Niambie kuna nini upande wa pili."
Kwa utulivu sana, daktari alisema, "Sijui...."... "Hujui? Wewe ni mshika dini, na hujui ni nini upande mwingine?" Daktari alikuwa ameshika kitasa cha mlango, mara upande wa pili ikasikika sauti ya kukwaruza na kunung'unika, na alipofungua mlango, mbwa akaruka ndani ya chumba hicho na kumrukia huku akionyesha furaha ya shauku.

Daktari akamgeukia mgonjwa, akasema, "Je, umemwona mbwa wangu? Hajawahi kuingia kwenye chumba hiki hapo awali. Hakujua kilichomo ndani. Hakujua chochote isipokuwa bwana wake alikuwa hapa, na mlango ulipofunguliwa, aliingia ndani bila woga. Sijui sana kilichoko upande wa pili wa kifo, lakini najua kitu kimoja... najua Mungu wangu yupo na hiyo inatosha."


Sanaa ya kifo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa unafiki tuliouona kwenye msiba wa EL tusubiri tutasikia mengi.
Watakuja watu watasema marehemu ndiye aliyenisaidia kuondoa bikra ya mke wangu.
Wait and see. Time is a tireless teacher.
Kwa sisi wakristo unafiki haukutajwa kwenye amri kumi. Je kwenu ninyi waislamu UNAFIKI Ni dhambi ?
marehemu ndiye aliyenisaidia kuondoa bikra ya mke wangu.
bd82e7100b9670a5bbfd1edd358ddda3.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania wengi Wana tabia kama za Herode.
Nina fuatilia kwa makini sifa/wema unaotolewa na viongozi waandamizi wa CCM juu ya Mzee Lowasa.Kwa wema unaotajwa na vinywa vyao, swali moja la msingi utajiuliza ni kwanini walimuibia kura ?

Hata wale walio mzuia ndani ya chama chao nao wanatuambia Mzee Lowasa alikuwa na sifa za malaika lakini wakamsulubisha kama shetani.Hii Nchi kama unafiki ungekuwa unazalisha umeme,bila shaka Tanzania ingekuwa na umeme mwingi kuliko Uingereza, Sweden, Denmark na Canada ukizijumlisha kwa pamoja.
20240213_080813.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanzia

Balozi Dkt. Diodorus Buberwa Kamala (26 November 1968 - 12 Feb 2024)

--
Balozi Mstaafu na Waziri wa zamani wa Afrika Mashariki, Dkt. Deodorus Buberwa Kamala amefariki dunia akiwa anapatiwa matibabu hospitali ya Mzena Jijini Dar es Salaam

Dkt. Buberwa amewahi kuwa Mbunge wa jimbo la Nkenge wilaya ya Missenyi mkoa wa Kagera kuanzia mwaka 2000 hadi 2010, mwaka 2006 aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Afrika Mashariki na baadaye Waziri Kamili mwaka 2008 hadi 2010

Mwaka 2011 aliteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji na Uholanzi ambako alitumikia nafasi hiyo hadi mwaka 2015 aliporejea kuwa Mbunge hadi mwaka 2020.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom