Albert Msando, Mwanasheria wa Zitto, Kitila na Mwigamba Kuunguruma kesho Serena 4.30 asbh

mkuu Earthmover ni kweli kabisa. Hawakutegemea kabisa hawa jamaa, dk slaa kawakata ngebe ktk safari yake hii ya kigoma


viva chadema

...Huu ni ushindi mkubwa sana katika medani za siasa....Chadema hatuongozwi kwa majina ...kama ingekuwa majina basi Chadema ingejiita Mesi!!!

..Kesho Chadema Msingi inaunguruma Kigoma mjini...stay tuned hapa hapa!!!
 
Muda mwingine kupitia misukosuko ndipo utaujua ufahamu wa mtu. Sikutegemea ZZK anaweza kutumia njia hii kutatua jaribu alilonalo. Anyway kama wapo waliomshauri kutumia vyombo vya habari katika utatuzi wa jambo dogo kama hili wana nia ya kumpoteza kisiasa. Vyombo vya habari havina urafiki na mtu ila kujipeleka ni kuwatengenezea biashara tu kwa headings nzito zenye utafiti kiduchu.

Tutarajia matusi mengine kesho kwa chama na viongozi wake wakuu.
 
Wakuu, nimetumiwa mwaliko huu wa uwepo wa mkutano na waandishi na wahariri kesho saa nne na nusu pale serena. ningependa nasi sote tuitikie wito huu kwa kuarifiana juu ya tukio hilo.

zaidi soma Taarifa za mwaliko


Mwaliko wa Mkutano na Waandishi wa habari: Ndugu Albert Msando



MWANASHERIA wa Mhe Zitto Zuberi Kabwe (Mb), Dr. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba, Ndugu Albert Msando, atazungumza na wahariri wa vyombo vya habari katika Hoteli ya Serena kuanzia saa nne na nusu asubuhi (saa 4.30 asubuhi).

Dhima ya mkutano huu itakuwa kutoa ufafafunuzi juu ya mashitaka 11 na majibu yake ambayo Mhe. Zitto Kabwe na washitakiwa wenzake walipewa na Kamati Kuu ya CHADEMA. Aidha, katika kikao hiki Ndugu Msando, kwa niaba ya wateja wake, ataeleza hatua ambazo wateja wake wanazichukua ndani ya chama katika kuhakikisha kwamba mgogoro uliopo unakwisha kwa amani na haraka iwezekanavyo bila kuleta athari zaidi kwa chama.

Tunatanguliza shukrani na tunaomba waalikwa wazingatie muda.

Imetolewa na Ofisi ya Mbunge Zitto Kabwe,
Jumanne, 10 Desemba 2013
Dar es Salaam
Mnyalu Msemakweli
===>Kweli nchi hii kuna ombwe la uongozi TeamZitto sisi hatutaki matamko ya kila siku,tunataka tuone nini kimefanyika kuhusu suala lenu,na ni vizuri tamko likatolewa na CDM Kurugenzi ya Habari,
===>Mnatukera na kutuchosha kwa kufanya mambo kama watoto,haya mambo ndio ambayo yamesababisha wew Zitto uchukiwe na wenzako,kwa nini huna uvumilivi na hupendi kufuata taratibu?
 
Last edited by a moderator:
Tutarajia matusi mengine kesho kwa chama na viongozi wake wakuu.

Uzuri jamii ishamjua ni mtu wa namna gani. Asubiri ubunge wa mahakama au wa viti maalum kama mama Rwakatare. Si wa kumuacha huyu ni kumfanya kama Malema wa ANC.
 
Anataka kueleza jinsi Babu alivyochemsha,alisema Mjadala umefungwa lakini anaenda mitaani akifanya Mikutano huku akisema ZZK ni mtovu wa nidhamu,iwapi busara ya akina ZZK kujieleza wakati Babu Slaa anaeleza hukumu ya ZZK na waenzake kuwa ni halali

BURIANI CHAMA CHA DOMOKRASIA NA MAOMBOLEZO
 
Ningewashauri hawa jamaa wakae kimya tu baada ya kupeleka utetezi wao Kamati kuu, wasubiri uamuzi!!!!!
 
Uzuri jamii ishamjua ni mtu wa namna gani. Asubiri ubunge wa mahakama au wa viti maalum kama mama Rwakatare. Si wa kumuacha huyu ni kumfanya kama Malema wa ANC.

Ni ujinga na utovu mkubwa wa Nidhamu kuijibu Kamati Kuu kupitia Vyombo vya Habari.

Udhalilishaji huu wa Kamati Kuu ufike mwisho sasa.Ni lazima Mbowe na Dr Slaa wakihami chama na uwe mwisho wa kuidharau Kamati Kuu.
 
Ningewashauri hawa jamaa wakae kimya tu baada ya kupeleka utetezi wao Kamati kuu, wasubiri uamuzi!!!!!

Taarifa za uhakika ni kwamba ukumbi wa Serena umelipiwa na CCM na watakaosimamia waandishi wa habari hapo kesho ni Vijana wa UVCCM.
 
Zitto ashasahaulika .kwenye TZ politics gatz,aanzishe chama chake cha dini yake na kanda yake amchukue kafulila,habib,hamad rashid,kisandu na wasaliti wenzie.msando majibu si lazima kwenye media na hatuna interest nayo,tunasubiri maamuzi ya kamati a.k.a CC.u guys try to learn in politics being quite is also an answer.tushawachoka you too wabinafsi.


wale wale wanaojiita wanademokrasia,tusubiri kesho tuone tatizo nini?
 
Mnyalu Msemakweli Hapa ndipo tunaposema kusoma sana na kuwa na vyeti kibao haisaidii kama hautakuwa na busara au hekima ,kwa nini Zitto na Kitila wanatoa majibu yao kwa tuhuma zinazowakabili kwa waandishi w habari badala ya kamati kuu?Ni kwa nini wanakimbilia siasa za kwenye vyombo vya habari?Au wanataka huruma ya wananchi ?.Msaliti siku zote huwa anahangaika sana kama kuku aliekatwa kichwa ,ni kurukaruka tu ndicho wanachokifanya Zitto na mwenzie Kitila.
 
Last edited by a moderator:
Mnyalu Msemakweli
===>Kweli nchi hii kuna ombwe la uongozi TeamZitto sisi hatutaki matamko ya kila siku,tunataka tuone nini kimefanyika kuhusu suala lenu,na ni vizuri tamko likatolewa na CDM Kurugenzi ya Habari,
===>Mnatukera na kutuchosha kwa kufanya mambo kama watoto,haya mambo ndio ambayo yamesababisha wew Zitto uchukiwe na wenzako,kwa nini huna uvumilivi na hupendi kufuata taratibu?

Wamejiandaa kumtukana Mbowe,Dr Slaa na Kamati Kuu hapo kesho.

Ni lazima chama kifuatilie nyendo za huyu Albert Msando anayejifanya CDM kumbe ni mwanachama wa CCM aliyeko CDM kukivuruga.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom