Albert Msando apotoka tena


Wakati ukiwa umenukuu, kipengele 6.3.4(c), kikiwa ni SABABU YA KUACHICHWA UONGOZI, LAKINI UMEKWEPA KUZUNGUMZIA NI MAMLAKA GANI YA UAJIBISHAJI, YENYE UWEZO WA KUIMPLEMENT KIPENGELE HICHO.

Nikukumbushe tu kuwa katiba inasema hivi


KWA MUJIBU WA VIPENGELE HAPO JUU NILIVYOVIQUOTE ZITTO KAMA KIONGOZI WA KITAIFA HAWEZI KUVULIWA NYADHIFA ZAKE NA KAMATI KUU, YEYE ANAWEZA KUWAJIBISHWA NA BARAZA KUU TU, TENA BAADA YA KURA YA SIRI KUPIGWA, NA HILO NDO LITACHAGUA MTU KUISHIKA HIYO NAFASI, NA HUYO MTU MWENYE KUISHIKILIA NAFASI HIYO ITABIDI ATHIBITISHWE NA MKUTANO MKUU.

SASA HII KAMATI KUU ITAJIPAJE MAMLAKA YA KUMVUA UONGOZI KIONGOZI MKUU WA KITAIFA KINYUME NA MADARAKA YAKE?
 
Haka ka BEN kanajikuta kenyewe ndio ka PLATO cha CHAGGADEMA,kweli hiki chama kimejawa mambululaaaaaaaaa
 
Hahaha ha.Hapana ....Let us call spade a spade!
Vijana mnauwa chama (CDM), ni wakati sasa kuunda taasisi ndani ya CDM kufundisha watu siasa mnafanya kama vile samba/yanga kwamba striker asipofungia timu siku ya derby eti kahongwa au msaliti...Khaa!Viongozi wa chama wanashutumiana JF inatufundisha nini, mwingine akitoa makala kwenye gazeti wengine wanaitafsiri watakavyo wao ili kuhalalisha walitakalo. Upande mmoja watuhumiwa wanajieleza dhidi ya shutuma, upande mwingine viongozi wapo majukwaani kuwaeleza wananchi yanayojiri wakihalalisha shutuma wakati watuhumiwa hawajatowa utetezi. Chama kinakuwa sasa suala la kambi haliepukiki na haya hujitokeza dhahiri miongoni mwa wanachama yanahitaji busara za hali ya juu kwenye chama kwa sababu hata kiongozi wa juu naye ana watu wake. Rejea UK Tony Blair alibanwa na chama chake kwa uamuzi wa kwenda Iraq na alijua hasimu wake ni Gordon Brown kabla ya uchaguzi aliachia ngazi lakini kwa utaratibu ndani ya chama ambao haukuleta mpasuko mkubwa chamani, vile vile conservative party ya UK Cameroon aliyachukuwa madaraka baada ya rafiki yake kushutumiwa kwamba hawezi kuongoza upinzani bungeni. Yote kwa yote ni siasa na kwa vyovyote lazima tukubali maamuzi ya vikao ila utetezi uheshimiwe, ila ni ngumu kuishinda CCM kwa hizi episode zinavyoendelea CDM........Kinana anazijua sana siasa za Tz na ukizingatia orodha ya wabunge wengi wa CDM walipata ubunge kwa makosa ya CCM (kwenye uteuzi wa wagombea) 2010 haswa kwenye majimbo yafuatayo, Arusha,Arumeru,Mbeya,Iringa,Tunduma,Ilemela,Musoma nk. inahitajika kazi kubwa kuliko ya katibu mkuu kwenda mikoani na kueza makosa ya zitto ambayo ni tuhuma badala ya kuibana serikali........na kuna jambo wewe kama ni mwanasiasa wa ukweli unahitaji kujiuliza, watuhumiwa wa ''usaliti'' wapo watatu lakini issue imekuwa Zitto, inawezekana kabisa ana ushawishi mkubwa kwa wananchi japo viongozi wanaaminisha wananchi kinyume. CDM ikiendelea na hili jambo naona kabisa upinzani unavyofifia........., kwa upande wa CDM kuna wabunge wanaoweza siasa za weledi mfano Mnyika,Slaa,Mdee,Zitto,Arfi hawa wanauwezo wa kuandika ripoti zenye ushawishi wa kitaifa ila kuna ambao yaani akiongea mara nyingi unaona anabishana na spika tu kujenga dhana kwamba wanaonewa.
 


Mkuu asikupe taabu Ben huyo na mie hatujaanza leo humu kupishana hoja!!!!!
Ila hicho ndio chama chenu mkuu hakuna.jema isipokuwa ya kuoendeza upande fulani tu!!!!
Ukitoa wazo tofauti utaitwa gamba sijui mamluki,umetumwa na wewe sasa unaitwa masalia huk ndani kwenu!!!!!

Mimi si mwanachadema as well sina chama kabisa ila hatuwezi kukaa kimya sababu ni CDM,CCM na wengine ndio vyama vinavyoshikilia hatima yetu kwa matendo yao na sio kadi za mifukoni mwa wananchi!!!!!

Sikutakii mabaya brother ila kwa mawazo yako humo sijui kama utadumu!!!!!!
 
Kuna kipindi unatamani ulale tu na ushtukie imefika 2015 ukapige kura basi! Lakini haiwezekani inabidi ushuhudie tu hizi sarakasi.
 

Huna hata aibu kuandika usichokiamini.

Kwa hiyo kwenda Serena kukitukana chama na Kamati kuu huku ukilindwa na Vijana wa UVCCM kwako ni sawa na sahihi kabisa.

Loh..wewe ni wa kuonewa huruma!
 
Bora msukule unaweza tumwa sehemu kuliko chuma chakavu lisilofaa kwa matumizi zaidi ya kurejeshwa kiwandani kutengenezwa product nyingine"wewe ni chuma chakavu"

kachumbari haikamiliki bila kutia mbwembwe zote ulizizitaja hapo
Teh teh teh unamaana skrepa..
 
Watu kama Msando hawatakiwi Chadema kutokana na misimamo yao ya kusimamia haki, Msando ni jasiri sana amejikita kwenye katiba ya chama chake wanaompiga wenyewe hawataki kuangalia katiba wanamsikiliza Mbowe na Lema.
 
I have no intention of putting my fate on politicians whom their only proffesional is conning voters_ my godfather,vitto corleone
 
Huna hata aibu kuandika usichokiamini.

Kwa hiyo kwenda Serena kukitukana chama na Kamati kuu huku ukilindwa na Vijana wa UVCCM kwako ni sawa na sahihi kabisa.

Loh..wewe ni wa kuonewa huruma!

Mbona nyie mnapata kura nyingi za urais na.hamtaki kujua uanachama wa supportrs wenu!!!!
Anasema anachokiamani na yupo tayari kukisimamia ndio maana kataka ushahidi wa hadhara ya Tanzania kupitia press!!!!!

Unawezaje kusema huyu mtu hajiamni tena ukiwa na fake ID wewe na yeye nani wa kuonewa huruma????!!!!!!

Wewe ni mfano halisi wa tofauti ya mzalendo na mfuasi!!!!!
 
Kama mambo ya kiserikali/utawala yangekuwa yanajadiliwa kama kifamilia(on family basis) ,vita ya dunia isingetokea_don corleone.
 

Stop being over jubilant brother.Do you agree with him?Je wewe unakubaliana na hizo rhetorics kama Mwanachama wa CHADEMA?Be honest to ypurself!

Chadema ni chama cha kinafiki tu hakina maana. Leo hii MUNGI anamuita mawalla freemason? Ilikuwaje wakakubali kupokea kiwanja walichopewa nae ? Huu ni zaidi ya ushirikina.

Huna hata aibu kuandika usichokiamini.

Kwa hiyo kwenda Serena kukitukana chama na Kamati kuu huku ukilindwa na Vijana wa UVCCM kwako ni sawa na sahihi kabisa.

Loh..wewe ni wa kuonewa huruma!

Molemo, nitajie matusi yangu kwa Chama na Kamati Kuu. Nitaona aibu.

Ulinzi wa nini nahitaji? Unawapa sifa CCM wasizostahili hata kidogo. Katika maisha yangu CCM wangekuwa wameongea na mimi au wamenitumia kwa hata jambo moja wangejisifu sana. Hilo halitakaa litokee na wanajua hivyo.

Inawezekana kabisa wewe ni mwanaCCM unajidai Chadema kwa kusema uongo na uzushi ili ionekane kuna tatizo. Tunawashtukia na tutawakomesha. Ujanja wenu wa kuchonganisha kwa kutumia kivuli cha kutojulikana kimefika mwisho.

Hatuendekezi upuuzi. Na kama ni mwanachadema na unaamini unachosema nipigie simu unieleweshe na mimi nitakuelewesha. Hakuna sababu ya kujificha. Nitumie PM na nitajadiliana na wewe vizuri tu.
 

Naona hata wewe umeendeshwa na mihemko.Kwa nini unatumia kesi ya Lwaks kama ref;CDM waliposema ni ya kugushi wana ushahidi wao,ambapo pindi ukihitajika watautoa.Halikadhalika wanaposema MM ni muhusika pia nategemea wana ushahidi vilevile.Ila kutumia Kesi ya Lwaks kutaka kumtetea Zitto,huo ni upuuzi.

sikutegemea Zitto kama ni mdhaifu kiasi hiki.Kwa akili yangu ndogo, ningetumia muda huu kuandaa utetezi wangu wa kutosha,nikaukabidhi kwa hiyo CC.then nikasubiri maamuzi yao.Kama nimeonewa taratibu nyingine zingefuata baada ya maamuzi yao yote.Kwa hili analolifanya ameishaonyesha, anatafuta huruma ya wananchi ili akipigwa chini,atafute watu wa kumuunga mkono.
Kwa mtizamo wangu ,huyu ni mtu wa kufukuzwa tu,anaonyesha ana matatizo sana.Anaonyesha pia ni mtu asiyependa kuongozwa kwa kufuata taratibu.
 
Watu kama Msando hawatakiwi Chadema kutokana na misimamo yao ya kusimamia haki, Msando ni jasiri sana amejikita kwenye katiba ya chama chake wanaompiga wenyewe hawataki kuangalia katiba wanamsikiliza Mbowe na Lema.

Jasiri ni Chenge tu aliyewaambia kwamba Gamba lake limefika kiunoni na halivuki, wote mmefyata mkia mpaka Alhaji Mkwele naye kimyaa!
 
Ben saa tisa alasiri,jiandae kuficha uso wako kipindi ZZK atarejeshewa madaraka

Kwa hiyo Lumumba mmejiandaa kumrudisha madarakani?

Kukusaidia zaidi soma MAWIO la leo Uk wa 4
 

Msando Albert,

Ikithibitika kuwa taratibu hazikufuatwa, je hiyo itafuta tuhuma walizopewa Zitto na wenzake? Na hivyo kufuta nia (intention) ya Kamati Kuu kuwaadhibu Zitto na wenzake? Hata wakimrejeshea Zitto nafasi yake ya Naibu Katibu Mkuu, atafanyaje kazi na timu ambayo inaamini kuwa Zitto ni msaliti? How will he fit in? Katika hali hiyo, chama kitaimarika vipi?

Na ukiacha taratibu, hizo tuhuma 11 ni zipi na majibu yake ni yapi? Sina hakika kama kwenye taarifa yako ya jana ulijibu tuhuma 11. Did you? If not, I am inclined to believe it was strategic. Kwa nini hizi tuhuma 11 zisiwekwe wazi ili wote tupime uzito wake? Mwenye kuzifahamu hizi tuhuma, tafadhali.
 


Mkuu, hata kama humpendi Lissu mpe haki yake. Kwenye RED (1) yeye hakutoa hukumu-cc ya chama ndio imetoa hukumu, yeye alitakiwa kuwasilisha tu. Kumbuka msemo wa wahenga- Mjumbe hauwawi. CC haikuwa kikao cha mtu mmoja wala wawili, na kwa kawaida kuna kuafikiana na kutoafikiana katika mjadala. Hivyo kupelekea kupigwa kura, hivyo watakaoshindwa lazima waunge mkono upande ulioshinda. Hivyo unamkosea Lissu unavomshambulia kuwa kahukumu.

Kwenye RED (2) ni ule ule upofu au mahaba uliyonayo kwa Zitto unakufanya uwapakazie REDBRIGADE. Nani Katekwa na kuporwa?? unaweza kuthibitisha hilo?? Kumbuka mdomo ni mali ya mtu na halipii kodi, hivo anaweza sema lolote muda wowote. Kimbembe kinakuja kwako wewe utakayepokea maneno usioyajua na kuanza kushabikia.

 
Hivi hizi pesa anazomwaga bwana zitto kwa watu kama hawa si angejiwekea hifadhi zikamsaidia baadae? au ndo sikio la kufa halisikii dawa?

Kwani anatoa mfukoni au zinatoka mfuko mkuu wa Serikali kwa kazi za TISS?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…