Albert Chalamila hajafanya kosa la uasi?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,305
12,600
Asichukuliwe poa kwani kitendo alichofanya ndugu Chalamila kina kila dalili zote kuwa sio cha bahati mbaya na hayuko peke yake.

Maongezi yake ukiyasikikiza vizuri yana kila dalili kuwa anawachochea watu wa kanda ile dhidi ya kifo cha mpendwa wetu. Bado haamini kuwa Mungu anaweza kufanya vile kwa mtu ambae ni Rais.

Chalamila anafahamu kuwa Tanzania ina kanda nyingi zikiwemo kanda za Mashariki, Kaskazini, Kati, Kuzini, Nyanda za juu Kusini, Magharibi na Kanda ya Ziwa. Alikuwa akifahamu kuwa kanda ya ziwa ilikuwa miongoni mwa kanda nchini ambazo zimerundikiwa kwa makusudi miradi mingi ya maendeleo ya matwilioni ya pesa kulinganisha na kanda nyingine nchini. Chalamila anataka kwenye miradi hiyo mama Samia asiondoe hata coma wala nukta kwenye ujenzi na utekelezwaji wake.

Chalamila inawezekana ana hasira iliyopitiliza juu ya awamu ya sita. Aliyoyasema hayakuwa kwa bahati mbaya, lazima ahojiwe zaidi ili kujua alimaanisha nini kusema pamoja na kwamba JPM amekufa lakini miradi ya kanda itatekelezwa kama ilivyo na mama Samia, huko ni kuwachonganisha wananchi wa kule na mama, maana hata JPM kuna miradi ya watangulizi wake aliifanyia tathmini ili kuona ipi aendelee nayo na ipi aicheleweshe na ipi aiache kabisa. Kwanini Chalamila anataka kuwaaminisha watu wake kuwa miradi na ahadi za JPM zitabaki palepale na vilevile kwa spidi ileile?
 
Chalamila ni mhuni kama wahuni wengine tu, mwacheni aje huku kwa mabeach boy tubembee naye......let them experience the difficulties for sometimes, they might learn somethin.....lazima naye ajue Bia inanunuliwaje....
 
Kule alikotokea:
1.Kama aliwabambikia watu tuhuma,basi itakuwa ni laana ya familia zilizonyanyaswa na maagizo yake.

2.Kama kuna watu aliowadhulumu haki yao,itakuwa ameombewa kila aina ya sala ili apate malipo yake hapa hapa duniani.

3.Kama jamii ilikuwa inasononeka,yawezekana "kamati za ufundi" ziliendelea kumshughulikia mpaka kieleweke!!!,Rejea yule mteule aliyetokea jimbo fulani ,ushindi wake ulitiliwa shaka,alipopata nafasi ya uteuzi "alishindwa kusoma kiapò",mambo ya kamati za ufundi sio mchezo mchezo!

HATA HUYU MKUU ALIYETENGULIWA NAFASI YA MKUU WA MKOA,AKIRUDI NYUMBANI ATAJISHANGAA NI NINI KIMEMTOKEA!!
 
Chalamila ni mhuni kama wahuni wengine tu, mwacheni aje huku kwa mabeach boy tubembee naye......let them experience the difficulties for sometimes, they might learn somethin.....lazima naye ajue Bia inanunuliwaje....
Ina maana yeye hakuwa na taarifa kuwa mama alikataza mabango?
 
Simkubali Chalamila ila kwa hili "MITANDAO IMEMSAGIA KUNGUNI".
Mdomo wake uliponza kichwa chake, mbuzi wa bwana heri na shamba la bwana heri. Cha msingi tu alikuwa akiimaanisha nini? Ujumbe wake unarandana kwa namna hii au ile na ule wa veronica france.

Tunachosema hatua isiishie kwenye kumsimamisha u RC tu bali ahojiwe na achunguzwe ili kujiridhisha na maneno yake yalilenga kitu gani. Kama aliponyokwa tu basi ijulikane vinginevyo aunganishwe na Jonas Mkude kwenye safari ya kwenda hospitali.
 
Nimesoma kichwa cha habari tu jibu ni ndio kafanya gross misconducts. Angekua the common mwananchi kwa zile kauli zake mbili zile angekua ananyea ndoo for the time being akichachafywa chafashwa. Hivo inatakiwa akamatwe ahojiwe akiwa ndani
 
Nimesoma kichwa cha habari tu jibu ni ndio kafanya gross misconducts. Angekua the common mwananchi kwa zile kauli zake mbili zile angekua ananyea ndoo for the time being akichachafywa chafashwa. Hivo inatakiwa akamatwe ahojiwe akiwa ndani

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
Kuna waziri aliyejaribu kutumia taaluma yake kuelezea hatari za kupiga nyungu kiafya akakiona cha mtema kuni sembuse huyu aliyepingana waziwazi na kiti.
 
Anasahau kuwa kule Kigoma hata umeme wa uhakika hawana watati kanda ile ikiwa na miradi mikubwa ya madaraja makubwa, maji, meli, viwanja vya ndege, hospitali ya kimataifa, barabara, benki kuuu, benki za biashara CRDB, mbuga ya wanyama, nk.
 
Kwa kweli alichokifanya Braza ni Insubordination ya wazi wazi. Kama rais alishaelekeza kuwa, Viongozi watatue matatizo ya wananchi huko huko kwenye maeneo yao. 'Hataki kuona bango lolote kwenye mikutano yake ati yeye akienda ndio aelezwe atatue wakati kuna utitiri wa viongozi kwenye ngazi mbalimbali. Alienda mbali akasema, bango 1 tu linatosha kumuondoa Mkuu wa Wilaya na wengine'.

Sasa ukizingatia tu maneno ya Mh. Rais, kiongozi mwenye busara angejitahidi kujua kero kuu ya wananchi ni ipi ili ikibidi itafutiwe suluhu na majibu mazuri, kabla ya ziara ya rais ili kuondoa uwezekano wa wananchi kuandika hayo mabango.

Ajabu, Mh. RC ndiye anakuwa mstari wa mbele kuhasisha wanachi kuandika Mabango. Tena anasema wewe andika hata matusi tu haina shida. Kwa kweli, kitendo hicho ni kupingana kabisa na maelekeo ya rais na ni dharau ya wazi. Hadi sasa wengi wanajiuliza, Chala alikusudia nini hasa? Alitaka matusi hayo atukanwe nani hasa? Je yeye wajibu wake kama M/kiti wa ulinzi na usalama mkoa ulikuwa wapi? Je hakuona kweli kuwa maagizo yake hayni kinyume na maelekezo ya Rais? Je hakufikili kuwa endapo wananchi wangeandika hayo mabango na matusi kama alivyowataka angeleta taharuki?

Kwa kweli, tunampongeza Mh. Rais kwa kuliona hilo kwa haraka sana kabla ya ziara yake huko. Maana huenda huyu bwana angeweza siku moja kuhamasisha jambo kubwa zaidi ya hili. Kuchunga kauli kwake imekuwa ni tatizo sana. Kiongozi amekuwa muda mwingi anahamasisha wananchi mambo yenye ukakasi, mfano "Hamasa ya kutaka wananchi Kunywa Pombe, ameshawahi pia kusema kuws vibaka nao wana umuhimu wake, bila vibaka kuwepo polisi watakuwa hawana kazi.." N.k. Sasa jamani, hao wananchi wakihamasika muda wote wanywe pombe, kutafanyika kweli kazi za maendeleo?

Kuna ambao wameshauri, ashikiliwe, achunguzwe n.k; hilo tunawaachia wenye mamlaka zao. Nisingependa kushauri maana sio eneo langu ila kiufupi nimeangalia kauli ya ndugu yetu huyu Vs. Maelekezo ya rais.

Anyway, tuwaombe viongozi wetu wawe serious na majukumu yao. Huku mtaani kuna watu wengi wenye elimu kubwa na uwezo mkubwa sn wa kuongoza lakini hawajapata fursa. Nyie kupata fursa msijisahau. Nchi ni yetu sote na sisi wananchi tunahitaji watu sahihi wa kuongoza njia kwenda kwenye maendeleo.
 
Kwa kweli alichokifanya Braza ni Insubordination ya wazi wazi. Kama rais alishaelekeza kuwa, Viongozi watatue matatizo ya wananchi huko huko kwenye maeneo yao. 'Hataki kuona bango lolote kwenye mikutano yake ati yeye akienda ndio aelezwe atatue wakati kuna utitiri wa viongozi kwenye ngazi mbalimbali. Alienda mbali akasema, bango 1 tu linatosha kumuondoa Mkuu wa Wilaya na wengine'...
Hata kwa kutumia jf unaweza kupata watu wazuri wanaoweza kulisaidia taifa hili kizalendo kabisa kuliko akina chalamila na kasesela
 
Asichukuliwe poa kwani kitendo alichofanya ndugu Chalamila kina kila dalili zote kuwa sio cha bahati mbaya na hayuko peke yake.

Maongezi yake ukiyasikikiza vizuri yana kila dalili kuwa anawachochea watu wa kanda ile dhidi ya kifo cha mpendwa wetu. Bado haamini kuwa Mungu anaweza kufanya vile kwa mtu ambae ni Rais.

Chalamila anafahamu kuwa Tanzania ina kanda nyingi zikiwemo kanda za Mashariki, Kaskazini, Kati, Kuzini, Nyanda za juu Kusini, Magharibi na Kanda ya Ziwa. Alikuwa akifahamu kuwa kanda ya ziwa ilikuwa miongoni mwa kanda nchini ambazo zimerundikiwa kwa makusudi miradi mingi ya maendeleo ya matwilioni ya pesa kulinganisha na kanda nyingine nchini. Chalamila anataka kwenye miradi hiyo mama Samia asiondoe hata coma wala nukta kwenye ujenzi na utekelezwaji wake.

Chalamila inawezekana ana hasira iliyopitiliza juu ya awamu ya sita. Aliyoyasema hayakuwa kwa bahati mbaya, lazima ahojiwe zaidi ili kujua alimaanisha nini kusema pamoja na kwamba JPM amekufa lakini miradi ya kanda itatekelezwa kama ilivyo na mama Samia, huko ni kuwachonganisha wananchi wa kule na mama, maana hata JPM kuna miradi ya watangulizi wake aliifanyia tathmini ili kuona ipi aendelee nayo na ipi aicheleweshe na ipi aiache kabisa. Kwanini Chalamila anataka kuwaaminisha watu wake kuwa miradi na ahadi za JPM zitabaki palepale na vilevile kwa spidi ileile?
Kawachonganisha nini hebu muache kulalama. Sisi tunachotaka maendeleo na si malalamiko. Muda uanenda hivyo unakaa kuanalyse. Je unajua wewe hali aliyoikuta? Eti uasi, chapeni kazi!
 
Kawachonganisha nini hebu muache kulalama. Sisi tunachotaka maendeleo na si malalamiko. Muda uanenda hivyo unakaa kuanalyse. Je unajua wewe hali aliyoikuta? Eti uasi, chapeni kazi!
Wacheni ujinga hali aliyoikuta ina nini? Barabara xilikuwepo, umeme ulikuwepo, magorofa yalijengwa, gesi iligunduliwa na kuwashwa, ajira zilikuwepo, timu ya taifa ilikuwa inacheza, uwanja wa mpira ulijengwa, udini na ukabila ulikuwa hakuna, mabasi ya kwenda haraka yalikuwepo, shule zilikuwepo, nyumba za askari zilijengwa kila kambi, airport ilikuwa inakarabatitiwa, barabara zilijengwa, daraja la kigamboni lilijengwa, nk. Tuache kudanganya watu.
 
Asichukuliwe poa kwani kitendo alichofanya ndugu Chalamila kina kila dalili zote kuwa sio cha bahati mbaya na hayuko peke yake.

Maongezi yake ukiyasikikiza vizuri yana kila dalili kuwa anawachochea watu wa kanda ile dhidi ya kifo cha mpendwa wetu. Bado haamini kuwa Mungu anaweza kufanya vile kwa mtu ambae ni Rais.

Chalamila anafahamu kuwa Tanzania ina kanda nyingi zikiwemo kanda za Mashariki, Kaskazini, Kati, Kuzini, Nyanda za juu Kusini, Magharibi na Kanda ya Ziwa. Alikuwa akifahamu kuwa kanda ya ziwa ilikuwa miongoni mwa kanda nchini ambazo zimerundikiwa kwa makusudi miradi mingi ya maendeleo ya matwilioni ya pesa kulinganisha na kanda nyingine nchini. Chalamila anataka kwenye miradi hiyo mama Samia asiondoe hata coma wala nukta kwenye ujenzi na utekelezwaji wake.

Chalamila inawezekana ana hasira iliyopitiliza juu ya awamu ya sita. Aliyoyasema hayakuwa kwa bahati mbaya, lazima ahojiwe zaidi ili kujua alimaanisha nini kusema pamoja na kwamba JPM amekufa lakini miradi ya kanda itatekelezwa kama ilivyo na mama Samia, huko ni kuwachonganisha wananchi wa kule na mama, maana hata JPM kuna miradi ya watangulizi wake aliifanyia tathmini ili kuona ipi aendelee nayo na ipi aicheleweshe na ipi aiache kabisa. Kwanini Chalamila anataka kuwaaminisha watu wake kuwa miradi na ahadi za JPM zitabaki palepale na vilevile kwa spidi ileile?
Naona katoa na singo ya kuhamasisha...


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chalamila ni mhuni kama wahuni wengine tu, mwacheni aje huku kwa mabeach boy tubembee naye......let them experience the difficulties for sometimes, they might learn somethin.....lazima naye ajue Bia inanunuliwaje....

Wewe unawaza bia na pombe wakati wenzio mlo wa siku tu ni shida!!! 😨
 
Back
Top Bottom