Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Kundi la wanaharakati vijana nchini Misri wamemtaka mkuu wa Shirika la Kimataifa la nguvu za Atomiki, Mohamed Al- Baradei kugombea urais katika nchi aliyozaliwa ya Misri.
Vijana hao kutoka chama cha upinzani cha Wafd, wamesema wameanza kampeni kumuunga mkono Bwa Al Baradei, anayetazamiwa kung'atuka katika nafasi yake ya sasa baadae mwakani.
Rais Mubarak ambaye sasa ana umri wa miaka 80, ameitawala nchi hiyo kwa miaka 28 na bado hajatamka iwapo atagombea tena urais mwaka 2011.
Kuna mjadala mkubwa unaoendelea nchini Misri wa mtu gani atakayechukua nafasi ya Mubarak, huku kukiwa na uvumi mwanawe mdogo, Gamal anaandaliwa kuchukua nafasi yake.
BBC KISWAHILI.
Vijana hao kutoka chama cha upinzani cha Wafd, wamesema wameanza kampeni kumuunga mkono Bwa Al Baradei, anayetazamiwa kung'atuka katika nafasi yake ya sasa baadae mwakani.
Rais Mubarak ambaye sasa ana umri wa miaka 80, ameitawala nchi hiyo kwa miaka 28 na bado hajatamka iwapo atagombea tena urais mwaka 2011.
Kuna mjadala mkubwa unaoendelea nchini Misri wa mtu gani atakayechukua nafasi ya Mubarak, huku kukiwa na uvumi mwanawe mdogo, Gamal anaandaliwa kuchukua nafasi yake.
BBC KISWAHILI.