Madai ya mwanzo kabisa ilikuwa kutaka muundo wa Muungano wetu uwe wa Shirikisho (Federal Union) Serikali 3, badala ya huu uliopo wa NCHI moja (Unitary State) Serikali2 na walijenga hoja zao kwa kufuata mfumo wa Shirikisho iilihali huo sio mfumo wetu. Inawezekana hawakujua kwamba Muungano wetu wa mwaka 1964 haukuwa wa Shirikisho kama walivyo aminishwa.
Mkuu
Mkandara , kwanza niendelee kukushukuru kwa rejeo lako humu jf, japo kwa sasa jf imekuwa sana, lakini idadi ya watu sensible ukilinganisha na ile jf ya zamani, watu sensible wamepungua sana, na kwa vile mwaka huu wa 2026, kwanza nimependekeza nyie wana jf wote waanzilishi wa ile jf ya 2006, mtambuliwe as jf pioneers, mpewe a token of appreciation, michango yenu ina thamani kubwa sana kwa taifa letu hili, asante
Mwaka 2026 JF Inatimiza Miaka 20! Tuwakumbuke Wana JF wa Zamani, Tuwaenzi, Tuwarudishe, na Wale ma GT wa Enzi Zile Waurejeshe Moto Kama Ule au ..?
Pili tangu kuasisiwa kwa huu muungano wetu adhimu na adimu, hakuna any public information program kuwaelimisha Watanzania kuhusu huu muungano wetu, hivyo wengi hawaujui, na hoja nyingi tuu za kupinga muungano zinatokana na ignorance!. Dawa ni serikali ikubali kugharimia public education and information program kuwaelimisha Watanzania kuhusu muungano wetu, Watanzania watauelewa. Mfano Watanzania bara wengi wanakereketwa na Wazanzibari kumiliki ardhi Bara, lakini wabara hatuwezi kumiliki ardhi Zanzibar, au ajira za Wazanzibari kwenye serikali ya JMT wakati hakuna mbara kuajiriwa SMZ!, hivyo kwa vile kuna vitu ni special na exclusive kwa Wazanzibari, wao nao wanataka Wabara pia na vitu exclusive na kuwaona Wazanzibari kama ni wageni. Hawajui kuwa baada baada ya muungano, wazanzibari wana haki sawa sawa na Mtanzania mwingine yeyote, zile haki zao za Zanzibar ni over and above!.
Tena baadhi viongozi wanasema wazi wazi kuwa Muungano ule Baraza la Malinduzi walilazimishwa kuukubali lakini haukupata ridhaa yao. Sijui hawa pia walikuwa katika Baraza lile Mpinduzi la kwanza lenhe wajumbe 29 ama nao walihadithiwa.
Hoja hii ni hoja ya kweli kabisa, muungano uliridhiwa na upande mmoja tuu wa muungano, Tanganyika, BLM liliarifiwa tuu na Karume kwa kuwaita mabalozi na kuwaarifu tumeungana na tumeridhia.
Hati za muungano zilizosainiwa tarehe 22 April pale Zanzibar na Nyerere na Karume, zilitaka ziridhiwe na mabunge ya nchi zote mbili, BLM liridhie Hati zile za Muungano ambazo ni international treaty kwa Zanzibar kufanya ratification na BLM litunge sheria ya muungano Zanzibar na Tanganyika we did, hati zile zililetwa Bunge la Tanganyika likaridhia, Tanganyika tukatunga sheria ya muungano, ile tarehe 23 April, na tarehe 25, Karume akatua kwenye Bunge la Tanganyika kubadilisha hati, kilichofanyika ni hakuna ratification yoyote iliyofanyika Zanzibar, wala Zanzibar haikutunga sheria yoyote ya muungano, bali sheria ya muungano ni moja tuu, iliyotungwa na Bunge la Tanganyika.
Kitendo cha Zanzibar kutoridhia muungano, hakuufanyi muungano kuwa halali, kwasababu muungano ni mkataba hivyo hata kama mkataba haukusainiwa, expressly, lakini ukatekelezwa , unahesabika umeridhiwa impliedly by performance, yaani Zanzibar japo haukuridhia muungano expressly by ratification, imeridhia impliedly by perfomance.
Kanuni hii pia inatumika kwenye forced mariages, ndoa ni mahusiano ya consensus, wanandoa wote wawili wanatakiwa kuridhia. Ndoa ambayo mwanandoa hakuridhia ni voidable marriage. Kuna ndoa nyingi mwanamke analazimishwa kuolewa bila ridhaa yake, forced mariages, akiishafika kwa mumewe, anaingiliwa kwa nguvu bila ridhaa yake, yaani anabakwa!, akishika ujauzito na kuamua kusalia kwenye ndoa hiyo huku akitimiza majukumu ya lile tendo, hata kama alilazimishwa, kisheria anahesabiwa ame consent hiyo ndoa, na inakuwa ni ndoa halali by performance, lakini mwanamke yule baada ya kufika kwa mume, akigomea tendo la ndoa kata kata, ndop hiyo inakuwa ni ndoa batili.
Hivyo ndivyo muungano ulivyo kwa Zanzibar, Wazanzibari japo hawakuridhia, lakini wameihudumia hii ndoa ya muungano, by perfomance, wanahesabika wameridhia na muungano ni halali!
Kifupi, Haya ni matusi mazito sana kwa Taifa letu nanhasa katika jamii ambayo tumeishi zaidi ya miaka 60 tukiamini sisi wote ni Watanzania.
Hoja kuwa Zanzibar haukuridhia muungano, sio matusi, it is a fact!.
Ukisikia Wazanzibar wanadai NCHI yao na Watanganyika wanadai NCHI yao. Muungano haramu hauwezi kuunda Serikali ya Shirikisho kwenye Muungano Haramu.
Muungano sio haramu, ni muungano halali hata kama umeingiwa ki haramu, kama ilivyo kwa mwana haramu, ni mtoto aliyetungwa nje ya ndoa na aliyezaliwa nje ya ndoa. Uharamu wa mtoto ni alipotungwa kama hakuna ndoa, tendo hilo ni zinaa, lakini baada ya kutunga mimba haramu, ukaamua kumuoa huyo mwanamke, siku mtoto anazaliwa, anakuwa ni mtoto halali. Muungano uliingiwa kiharamu Zanzibar, hivyo ni momba haramu, lakini baada ya April 26, Tannganika na Zanzibar kuwa ni nchi moja, sheria ile ile moja ya muungano ya Tanganyika, imetosha kuuhalalisha muungano Zanzibar kwasababu sasa ni nchi moja ya Tanzania.
Kama hutuutambui Muungano, tunawezaje kuunda Serikali zozote ndani ya Muungano usotambuliwa? Kama hutuutambui Muungano wetu wala hauna ridhaa yetu, tunataka Serikali 3 za kitu gani?
Kama kuna mtu yoyote anadiriki kusema hautambui muungano!, huyo ni kichaa!, ni mwendawazimu!, na vichaa hao na wendawazimu hao wako wengi tuu. Mimi niliwahi kumshauri Dr Shein
Dkt. Shein Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Kabla Hajamwaga Sumu Hii na pia Dr. Mwinyi
Ushauri wa Bure kwa Dkt. Hussein Mwinyi: Mfute Kazi Haraka Othman Masoud Kabla Hajaendelea Kueneza Sumu
Namshukuru Mungu wachawi wameanza kutua juu ya paa mchana kweupe. Na kibaya zaidi zile sifa za KiongoI tumtakae, alizosema Mwalimu mwaka 1995 kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Chama chake zimebakia kuwa hadithi nyingine ndani ya Kitabu.
Tuliombee taifa letu, aidha maneno ya Mwalimu yametimia, tunasubiri Utabiri wa Sheikh Yahya Hussein.
Masalaam
Utatimia!
Huu Muungano wetu Adhimu, tutaulinda kwa gharama yoyote!
Mungu Ibariki Tanzania
P