UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 3,104
- 14,258
- Thread starter
- #61
Akinyi Must Die (Ni lazima Akinyi Afe) - 02
Sauti ya kiume "Bwana Yesu asifiwe kanisa?"
Ilikuwa ni sauti ya Muinjilisti ikisikika vema tokea kanisa la Kiinjili la kilutheri Tanzania,maeneo ya Nyamhongolo.
Waumini "Aminaaaa"
Ilikuwa ni jumapili nyingine tulivu ambayo ilikuwa ni utaratibu wa mama Deo kila ifikapo siku hiyo yeye na familia yake hujumuika pamoja na waumini wengine kwa ajili ya kumsifu na kumuabudu Mungu.
Muinjilisti "Kama ilivyokuwa imetangazwa na uongozi wa kanisa,leo itakuwa siku ya kipekee ya wageni ikiambatana na kuwaombea watoto wadogo na kuwakabidhi mikononi mwa Bwana"
Muinjilisti aliendelea "Nadhani mbele yenu kama mnavyoona kuna ugeni mkubwa,sisi kama kanisa mara zote wageni wanapotutembelea huwa tunakawakarimu kwa nyimbo na mambo mengi,lakini pia huwa tunawapa fursa ya kusalimia kanisa,pia Baba mchungaji atakuja kuwakaribisha vyema wageni wote waliopata nafasi kuabudu pamoja nasi siku ya leo"
Muinjilisti "Basi tusiendelee kupoteza muda nimuombe mzee wa kanisa aje amkaribishe Baba mchungaji"
Mzee wa Kanisa "Bwana wetu Yesu Kristo apewe sifa"
Waumini "Ameeen"
Aliendelea "Nisingependa kupoteza muda kwa maana mengi yamesha semwa na Muinjilisti wetu wa Kanisa,hivyo nichukue nafasi hii kumkaribisha Baba Mchungaji"
Aliendelea "Baba mchungaji karibu sasa kisemeo ni cha kwako"
Baba Mchungaji "Ahsante sana Mzee wetu wa kanisa lakini pia nimshukuru Muinjilisti Siphael Lelo kwa ukaribisho wa Utangulizi,Mungu awabariki sana"
Baba Mchungaji "Ndugu waumini wenzangu,leo ni siku ya pekee sana kusimama tena mbele yenu,napenda nimshukuru mwenyezi Mungu kwa kunipatia fursa hii ya pekee,kama mtakumbuka wiki iliyopita nilitangaza hapa ya kwamba,jumapili ya leo ambayo ni siku ya Bwana,tutapokea wageni ambao wataungana nasi katika kumuabudu Mungu,mbali na mambo mengine pia mlitangaziwa itakuwa ni siku maalumu kwa ajili ya kuwaombea watoto wetu wadogo na ambao hawajawahi kukabidhiwa mikononi mwa Bwana"
Aliendelea "Basi nisipoteze muda kwasababu muda nao umetuacha sana,nipende kuwakaribisha wageni wote waliotutembelea leo lakini kwa upekee nipende kumkaribisha Mchungaji Timotheo Owino kutoka kule Kisumu Kenya ambaye yeye na Mkewe leo wameona watubariki kama kanisa kwa kuabudu pamoja nao"
Aliendelea "Lakini pia nipende kukukaribisha Pastor kwa ajili ya kutuendeshea ibada pia utakuwa na jukumu la kuwaombea watoto wadogo na kuwakabidhi mikononi mwa Bwana"
Baada ya muda wa ibada kuisha,ilianza kazi rasmi ya kuwaombea watoto,kila mwanamke au familia ya baba na mama ambao walikuwa na mtoto mdogo walipaswa kusogea mbele ili kuwekwa mikononi mwa Bwana.Basi kwakuwa familia nzima ya mama Deo ilihudhuria ibada hiyo,hawakusita kwenda mbele na yule mtoto mdogo kwa ajili ya mibaraka ile ya maombezi.
Mchungaji Owino " Nilipomshika kichwa huyu mtoto ili nimuombee,nimehisi nguvu zinanitoka ghafla ndani yangu na najihisi roho wa Bwana amenishukia"
Aliendelea "Huyu mtoto anaitwa nani?"
Mama Deo "Mmh! ni stori ndefu Pastor"
Mchungaji Owino "Anaitwa ni stori ndefu!?"
Mama Deo "Hapana Pastor hana jina"
Mchungaji Owino "Oooh!, ok kaa pale nisubiri nifanye huduma hii nakurudia nikimaliza maana mwanao anakitu cha pekee sana mama"
Haikuchukua muda yule mchungaji Timotheo Owino kumaliza ile huduma,alipokamilisha alimuita mama Deo kwa ajili ya mahojiano zaidi na kutaka kufahamu upekee wa yule mtoto.Mama deo hakutaka kuficha kitu alimsimulia yule mchungaji kila kitu kuhusu yule mtoto.
Mchungaji Owino "Haleluya,nakushukuru sana Mungu wa Mbinguni kwa ajili ya kiumbe huyu"
Aliendelea "Sasa kama ndivyo nakuomba huyu mtoto kuanzia leo aitwe AKINYI,na pia mimi na mama mchungaji tutazungumza na nitashirikisha na uongozi wa kanisa pia na kama ikiwapendeza nyinyi nyote basi tunaomba tuondoke na huyu binti mzuri tukamtunze"
Mama Deo " Sawa baba mchungaji sisi hatuna tatizo ila ni vema serikali ya mtaa akiwemo Mwenyekiti na Mjumbe wakafahamu suala hili maana huyu mtoto nilikabidhiwa mimi nimuangalie"
Mchungaji Owino "Basi leo jioni tutakuwa wageni nyumbani mwenu nahitaji tushiriki maombi na familia yako"
Mama Deo "Karibu sana baba mchungaji"
Baada ya ibada mama Deo na familia yake hawakutaka kupoteza muda waliianza safari ya kurudi nyumbani ili kujiandaa kwa ugeni ule jioni ya siku hiyo.Mchungaji Timotheo Owino pamoja na mkewe waliongea na uongozi wa lile kanisa ikiwemo mchungaji ambaye alikuwa mwenyeji wake na wakapewa baraka zote za kuitembelea ile familia ya mama Deo kwa usiku ule.
Sasa ilipofika jioni mchungaji Timotheo Owino Okumu na mkewe waliongozana na muinjilisti Siphael Lelo aliyekuwa akiyafahamu makazi ya waumini wa kanisa lake mpaka kwa familia ya mama Deo.
Ilipofika usiku mama Deo alipokea Ugeni mzito ukiongozwa na Muinjilisti Siphael Lelo aliyekuwa Muinjilisti wa Kanisa alilokuwa akiabudu la Kilutheri Tanzania kwa Usharika wa Ilemela aliyeambatana na Mchungaji Timotheo Okumu Owino pamoja na Mkewe.
Mama Deo "Karibuni sana jamani"
Mchungaji Owino "Ahsante sana binti yangu"
Baada ya kupata chakula na kujumuika wote kwa pamoja katika maombi usiku ule,Mchungaji Timotheo Owino aliyekuwa ameambatana na mkewe pamoja na Muinjilisti Siphael Lelo,waliamua kuondoka kwa makubaliano kwamba,baada ya siku tatu kuwepo pale kanisani wangeomba kuondoka na kile kitoto kichanga kurejea kwao nchini Kenya endapo wangekubaliwa na Uongozi wa kanisa pamoja na mamlaka za kiserikali.
Uongozi wa kanisa ulichukua jukumu la kufuatilia lile suala la mtoto kwa mamlaka husika za nchi ikiwemo jeshi la polisi kwasababu upelelezi wa kesi ya msingi ulikuwa bado haujakamilika,hivyo mama Deo angechukua jukumu la kuwakabidhi yule mtoto pengine angekuwa mwenye atia kulingana na sheria za Jamhuri.
Mamlaka za nchi ikiwemo Ustawi wa jamii pamoja na Jeshi la polisi baada ya kujiridhisha kwamba taasisi ya kikanisa ndiyo ilikuwa ikimuhitaji yule mtoto ilitoa ruksa ya kwamba wamchukue wakamtunze na wahakikishe wanampatia mahitaji yote muhimu ya kibinadamu na wawe wanatoa taarifa muhimu kwa uongozi wa kanisa ili kuwezesha kufahamu maendeleo ya mtoto.
Kweli!,baada ya ziara ya kikanisa ya mchungaji Timotheo Okumu Owino kukamilika walimchukua yule mtoto mdogo ambaye walimpatia jina la Akinyi na kuondoka naye kuelekea nchini Kenya katika kaunti ya Kisumu.
AFTER 15 YEARS SOME WHERE IN TARIME (BAADA YA MIAKA 15 MAHALI FULANI TARIME)
Sauti ya kiume "Mama mseti"
Sauti iliendelea kuita "Mamaa mseetiii"
Mama Mseti "Abheeeee"
Sauti ya kiume "Tacho omahe(Hebu njoo)"
Aliendelea "Hivi ulishamueleza Bhoke lile suala?"
Mama Mseti "Nilimwambia lakini alikuwa analia anasema hataki"
Sauti ya kiume "Tarehe 16 ni wiki ijayo,hivyo hakikisha unapeleka jina lake kwa mzee Machera"
Mama Mseti "Sawa"
Katika kijiji cha Magoto wilayani Tarime,sherehe za tohara na ukeketaji zilipambana moto,ilikuwa ni ufahari kijana mwenye umri mdogo kupata tohara ya kimila na kiutamaduni isiyokuwa na ganzi ndani yake kwani ilionyesha ujasiri wa hali ya juu,pia kama ungeweza kuvumilia tohara ile iliyokuwa na maumivu makubwa,basi iliashiria kwamba ungeweza kupambana hata na Simba.Pamoja na tohara zile kwa vijana wa kiume,pia kulikuwa na ukeketaji kwa mabinti wadogo ambao walianza kuvunja ungo,suala la ukeketaji kwa mabinti wadogo licha ya kuacha maumivu na makovu kwa mabinti lakini lilileta heshima na ufahari kwenye familia aliyotekea binti husika.Hivyo kila ilipokuwa ikifika mwezi wa 11 wa kila mwaka kulikuwa kukifanyika sherehe kubwa za kimila na kiutamaduni,zilipishana tu tarehe kati ya tohara na ukeketaji lakini mwezi ulikuwa ni mmoja.
Mama Mseti "Juzi nimeongea na baba yako nimejaribu kumueleza lakini haelewi mwanangu"
Mama Mseti alikuwa akiongea na binti mrembo aliyekuwa na sifa za kila aina za kuitwa mwanamke mzuri,ingawa alikuwa na umri mdogo lakini alikuwa na akili ya kupambanua mambo kama mtu mzima.
Binti "Lakini mama kwa nini baba anataka kunifanyia hivi?"
Mama Mseti "Mwanangu baba yako unamfahamu namna alivyomkali,pia ukikataa kufanyiwa ukeketaji mimi atanipiga mpaka aniue maana nitakuwa nimevunja mila na desturi zetu"
Mama Mseti aliendelea "Nakuomba uvumilie tu mwanangu,mbona mwenzio Wesiko alifanyiwa na sasa yupo mzima tu"
Mama mseti aliendelea kumshawishi binti Bhoke ili akubali kufanyiwa ukeketaji ili kuiheshimisha ile familia.Bhoke aliingia ndani akaanza kulia sana akiamini ule ukeketaji ulikuwa unaondoa sifa ya usichana wake.
Hakupenda kusikia kitu kinaitwa ukeketaji na ilikuwa ikimuumiza sana kuona mama yake pamoja na baba yake wakilazimisha lile jambo,yeye aliamini wazazi wake ndio wangekuwa mstari wa mbele kulikataa lakini haikuwa hivyo.Ilikuwa kabla ya ukeketaji majina yote ya mabinti waliofikisha umri wa kukeketwa yalipelekwa kwa Ngariba,Ngariba aliyefahamika kwa wakati huo na asiyekuwa na huruma hata kidogo alifahamika kwa jina moja la Nyanchimweru aliyekuwa mke wa mzee maarufu hapo Kijijini Magoto aliyefahamika kama Mzee Machera Wanyonyi.
Sauti ya kiume "Hivi hela zangu nilizoweka chini ya mtungi zimeenda wapi?"
Alikuwa mzee Gisiri Mnanka au Baba Mseti akimuuliza mkewe.
Mama Mseti "Mi hata sijui"
Baba Mseti "Hujui!,tatigha kundetera Obhokangi(Acha kuniletea ujinga),nazitaka hizo hela"
Mzee Gisiri alikuwa akimuuliza mkewe Mama Mseti kuhusu hela zake huku akiwa mwenye Jazba asiyekuwa na mzaha hata kidogo.
Mama Mseti "Sasa jamani hizo hela nichukue nipeleke wapi!"
Mama Mseti aliendelea kujitetea kwa kutolea ufafanuzi kwa upole na sauti ya hamaki na mshangao.
Baba Mseti "Nikirudi jioni kutoka mnadani nizikute hizo hela"
Ilikuwa ni sauti ya Mzee Gisiri iliyojaa jazba na msisitozo huku akifungua mlango na kuondoka zake.Mama mseti aliwaza sana ni nani atakuwa amechukua hela za mumewe ambaye ni mkorofi kupita kiasi.
Alianza kuzitafuta zile hela ndani ya nyumba bila kuambulia chochote.
Jioni ile mama Mseti alimsubiri Bhoke binti yake atoke shule uenda akawa anafahamu kuhusu hela za Baba yake,mama Mseti aliendelea kusubiri bila mafanikio ya kuonekana Kwa Bhoke,aliamua kuondoka mpaka kwa rafiki yake Bhoke ambaye aliitwa Wesiko Gisunte ili kuona kama mwanae amepita kwa huyo rafiki yake.
Wesiko "Kwani hajarudi?"
Aliendelea "Aliponipitia twende shule alikuja akasema nimsindikize Senta akapande gari anaenda Nyabitocho kupeleka hela za ng'ombe baba yake kamtuma,akaniambia atawahi kurudi"
Mama Mseti "Huyu mtoto anataka kuniingiza kwenye matatizo"
Mama mseti aliendelea kujisemea huku machozi yakimtoka akimhofia zaidi mumewe.
Wesiko "Kwani hamkumtuma?"
Mama Mseti "Amechukua hela za baba yake katoroka"
Wesiko "Sasa itakuwaje bhamure"
Wesiko ambaye alikuwa rafiki yake kipenzi na Bhoke alionekana kushangaa sana.
Mama mseti alirudi nyumbani kwake huku akiwaza namna itakavyokuwa.Haukupita muda mzee Gisiri akawa amerudi nyumbani na mama Mseti kumueleza kila kitu.
Baba Mseti "Huyo atakuwa amekimbia Saro(ukeketaji)"
Mzee Gisiri Mnanka alieleza kwa jazba sana kiasi kwamba ungejichanganya mbele yake ilikuwa ni halali yake.
Aliendelea "Nilikwambia tangia mwanzo uwe makini na huyu mtoto lakini ukawa mbishi,ona sasa,hii aibu tutaiweka wapi mama Mseti?,hivi unadhani jamii itatuchuliaje?,huyu mtoto asipopatikana na wewe uondoke hapa la sivyo nitakuua!"
Muda huo mama Mseti alikuwa ametulia tuli kama maji ya mtungi maana alifahamu kabisa angenyanyua mdomo wake,basi ingekuwa mwisho wa maisha yake.Asubuhi na mapema mzee Gisiri alienda kumuamsha kijana wake mkubwa aliyeitwa Mseti ambaye hakuwa mbali na Boma la Baba yake na kumueleza namna hali ilivyokuwa,Mseti alichukua Baiskeli akambeba Baba yake wakaanza safari ya kuelekea kijiji cha Nyabitocho ili kumtafuta binti Bhoke.
Bhoke "Nauli ya kuelekea Musoma ni ngapi?"
Ilikuwa ni sauti ya Binti Bhoke akimuuliza mmoja wa Kondakta wa Hiace zilizokuwa zimepaki stendi ya Tarime mjini zikiwa na ruti ya kuelekea Musoma.
Kondakta "Kwa wewe mwanafunzi ni elfu moja miatano"
Bhoke alichomoa hela alizokuwa ameziweka kwenye mfuko wa sketi yake ya shule aliyokuwa amevaa mpaka wakati huo.
Bhoke "Hii hapa"
Kondakta "Matiko,hebu mkatie huyu mtoto tiketi acha kushangaa bhana"
Kondakta "Ingia ukae pale nyuma jirani na yule mama"
Baada ya kupewa tiketi yake Bhoke alipewa pia utaratibu wa kukaa ndani ya ile gari,binti Bhoke aliingia na kuelekea nyuma kabisa ya siti jirani na mama mmoja wa makamo.
Wakati huo mzee Gisiri na mwanaye Mseti walipofika pale kijijini Nyabitocho walianza kumsaka Bhoke bila mafanikio yoyote.Waliendelea kutafuta maeneo mbalimbali pale kijijini ikiwemo kuuliza watu aliyofahamiana nao lakini hakufanikiwa.
Baba Mseti "Sasa atakuwa ameenda wapi?"
Aliendelea "Nitampata tu,we subiri uone"
Mzee Gisiri alisema kwa jazba huku akiendelea kumtafuta Bhoke binti yake.
Itaendelea............................
Sauti ya kiume "Bwana Yesu asifiwe kanisa?"
Ilikuwa ni sauti ya Muinjilisti ikisikika vema tokea kanisa la Kiinjili la kilutheri Tanzania,maeneo ya Nyamhongolo.
Waumini "Aminaaaa"
Ilikuwa ni jumapili nyingine tulivu ambayo ilikuwa ni utaratibu wa mama Deo kila ifikapo siku hiyo yeye na familia yake hujumuika pamoja na waumini wengine kwa ajili ya kumsifu na kumuabudu Mungu.
Muinjilisti "Kama ilivyokuwa imetangazwa na uongozi wa kanisa,leo itakuwa siku ya kipekee ya wageni ikiambatana na kuwaombea watoto wadogo na kuwakabidhi mikononi mwa Bwana"
Muinjilisti aliendelea "Nadhani mbele yenu kama mnavyoona kuna ugeni mkubwa,sisi kama kanisa mara zote wageni wanapotutembelea huwa tunakawakarimu kwa nyimbo na mambo mengi,lakini pia huwa tunawapa fursa ya kusalimia kanisa,pia Baba mchungaji atakuja kuwakaribisha vyema wageni wote waliopata nafasi kuabudu pamoja nasi siku ya leo"
Muinjilisti "Basi tusiendelee kupoteza muda nimuombe mzee wa kanisa aje amkaribishe Baba mchungaji"
Mzee wa Kanisa "Bwana wetu Yesu Kristo apewe sifa"
Waumini "Ameeen"
Aliendelea "Nisingependa kupoteza muda kwa maana mengi yamesha semwa na Muinjilisti wetu wa Kanisa,hivyo nichukue nafasi hii kumkaribisha Baba Mchungaji"
Aliendelea "Baba mchungaji karibu sasa kisemeo ni cha kwako"
Baba Mchungaji "Ahsante sana Mzee wetu wa kanisa lakini pia nimshukuru Muinjilisti Siphael Lelo kwa ukaribisho wa Utangulizi,Mungu awabariki sana"
Baba Mchungaji "Ndugu waumini wenzangu,leo ni siku ya pekee sana kusimama tena mbele yenu,napenda nimshukuru mwenyezi Mungu kwa kunipatia fursa hii ya pekee,kama mtakumbuka wiki iliyopita nilitangaza hapa ya kwamba,jumapili ya leo ambayo ni siku ya Bwana,tutapokea wageni ambao wataungana nasi katika kumuabudu Mungu,mbali na mambo mengine pia mlitangaziwa itakuwa ni siku maalumu kwa ajili ya kuwaombea watoto wetu wadogo na ambao hawajawahi kukabidhiwa mikononi mwa Bwana"
Aliendelea "Basi nisipoteze muda kwasababu muda nao umetuacha sana,nipende kuwakaribisha wageni wote waliotutembelea leo lakini kwa upekee nipende kumkaribisha Mchungaji Timotheo Owino kutoka kule Kisumu Kenya ambaye yeye na Mkewe leo wameona watubariki kama kanisa kwa kuabudu pamoja nao"
Aliendelea "Lakini pia nipende kukukaribisha Pastor kwa ajili ya kutuendeshea ibada pia utakuwa na jukumu la kuwaombea watoto wadogo na kuwakabidhi mikononi mwa Bwana"
Baada ya muda wa ibada kuisha,ilianza kazi rasmi ya kuwaombea watoto,kila mwanamke au familia ya baba na mama ambao walikuwa na mtoto mdogo walipaswa kusogea mbele ili kuwekwa mikononi mwa Bwana.Basi kwakuwa familia nzima ya mama Deo ilihudhuria ibada hiyo,hawakusita kwenda mbele na yule mtoto mdogo kwa ajili ya mibaraka ile ya maombezi.
Mchungaji Owino " Nilipomshika kichwa huyu mtoto ili nimuombee,nimehisi nguvu zinanitoka ghafla ndani yangu na najihisi roho wa Bwana amenishukia"
Aliendelea "Huyu mtoto anaitwa nani?"
Mama Deo "Mmh! ni stori ndefu Pastor"
Mchungaji Owino "Anaitwa ni stori ndefu!?"
Mama Deo "Hapana Pastor hana jina"
Mchungaji Owino "Oooh!, ok kaa pale nisubiri nifanye huduma hii nakurudia nikimaliza maana mwanao anakitu cha pekee sana mama"
Haikuchukua muda yule mchungaji Timotheo Owino kumaliza ile huduma,alipokamilisha alimuita mama Deo kwa ajili ya mahojiano zaidi na kutaka kufahamu upekee wa yule mtoto.Mama deo hakutaka kuficha kitu alimsimulia yule mchungaji kila kitu kuhusu yule mtoto.
Mchungaji Owino "Haleluya,nakushukuru sana Mungu wa Mbinguni kwa ajili ya kiumbe huyu"
Aliendelea "Sasa kama ndivyo nakuomba huyu mtoto kuanzia leo aitwe AKINYI,na pia mimi na mama mchungaji tutazungumza na nitashirikisha na uongozi wa kanisa pia na kama ikiwapendeza nyinyi nyote basi tunaomba tuondoke na huyu binti mzuri tukamtunze"
Mama Deo " Sawa baba mchungaji sisi hatuna tatizo ila ni vema serikali ya mtaa akiwemo Mwenyekiti na Mjumbe wakafahamu suala hili maana huyu mtoto nilikabidhiwa mimi nimuangalie"
Mchungaji Owino "Basi leo jioni tutakuwa wageni nyumbani mwenu nahitaji tushiriki maombi na familia yako"
Mama Deo "Karibu sana baba mchungaji"
Baada ya ibada mama Deo na familia yake hawakutaka kupoteza muda waliianza safari ya kurudi nyumbani ili kujiandaa kwa ugeni ule jioni ya siku hiyo.Mchungaji Timotheo Owino pamoja na mkewe waliongea na uongozi wa lile kanisa ikiwemo mchungaji ambaye alikuwa mwenyeji wake na wakapewa baraka zote za kuitembelea ile familia ya mama Deo kwa usiku ule.
Sasa ilipofika jioni mchungaji Timotheo Owino Okumu na mkewe waliongozana na muinjilisti Siphael Lelo aliyekuwa akiyafahamu makazi ya waumini wa kanisa lake mpaka kwa familia ya mama Deo.
Ilipofika usiku mama Deo alipokea Ugeni mzito ukiongozwa na Muinjilisti Siphael Lelo aliyekuwa Muinjilisti wa Kanisa alilokuwa akiabudu la Kilutheri Tanzania kwa Usharika wa Ilemela aliyeambatana na Mchungaji Timotheo Okumu Owino pamoja na Mkewe.
Mama Deo "Karibuni sana jamani"
Mchungaji Owino "Ahsante sana binti yangu"
Baada ya kupata chakula na kujumuika wote kwa pamoja katika maombi usiku ule,Mchungaji Timotheo Owino aliyekuwa ameambatana na mkewe pamoja na Muinjilisti Siphael Lelo,waliamua kuondoka kwa makubaliano kwamba,baada ya siku tatu kuwepo pale kanisani wangeomba kuondoka na kile kitoto kichanga kurejea kwao nchini Kenya endapo wangekubaliwa na Uongozi wa kanisa pamoja na mamlaka za kiserikali.
Uongozi wa kanisa ulichukua jukumu la kufuatilia lile suala la mtoto kwa mamlaka husika za nchi ikiwemo jeshi la polisi kwasababu upelelezi wa kesi ya msingi ulikuwa bado haujakamilika,hivyo mama Deo angechukua jukumu la kuwakabidhi yule mtoto pengine angekuwa mwenye atia kulingana na sheria za Jamhuri.
Mamlaka za nchi ikiwemo Ustawi wa jamii pamoja na Jeshi la polisi baada ya kujiridhisha kwamba taasisi ya kikanisa ndiyo ilikuwa ikimuhitaji yule mtoto ilitoa ruksa ya kwamba wamchukue wakamtunze na wahakikishe wanampatia mahitaji yote muhimu ya kibinadamu na wawe wanatoa taarifa muhimu kwa uongozi wa kanisa ili kuwezesha kufahamu maendeleo ya mtoto.
Kweli!,baada ya ziara ya kikanisa ya mchungaji Timotheo Okumu Owino kukamilika walimchukua yule mtoto mdogo ambaye walimpatia jina la Akinyi na kuondoka naye kuelekea nchini Kenya katika kaunti ya Kisumu.
AFTER 15 YEARS SOME WHERE IN TARIME (BAADA YA MIAKA 15 MAHALI FULANI TARIME)
Sauti ya kiume "Mama mseti"
Sauti iliendelea kuita "Mamaa mseetiii"
Mama Mseti "Abheeeee"
Sauti ya kiume "Tacho omahe(Hebu njoo)"
Aliendelea "Hivi ulishamueleza Bhoke lile suala?"
Mama Mseti "Nilimwambia lakini alikuwa analia anasema hataki"
Sauti ya kiume "Tarehe 16 ni wiki ijayo,hivyo hakikisha unapeleka jina lake kwa mzee Machera"
Mama Mseti "Sawa"
Katika kijiji cha Magoto wilayani Tarime,sherehe za tohara na ukeketaji zilipambana moto,ilikuwa ni ufahari kijana mwenye umri mdogo kupata tohara ya kimila na kiutamaduni isiyokuwa na ganzi ndani yake kwani ilionyesha ujasiri wa hali ya juu,pia kama ungeweza kuvumilia tohara ile iliyokuwa na maumivu makubwa,basi iliashiria kwamba ungeweza kupambana hata na Simba.Pamoja na tohara zile kwa vijana wa kiume,pia kulikuwa na ukeketaji kwa mabinti wadogo ambao walianza kuvunja ungo,suala la ukeketaji kwa mabinti wadogo licha ya kuacha maumivu na makovu kwa mabinti lakini lilileta heshima na ufahari kwenye familia aliyotekea binti husika.Hivyo kila ilipokuwa ikifika mwezi wa 11 wa kila mwaka kulikuwa kukifanyika sherehe kubwa za kimila na kiutamaduni,zilipishana tu tarehe kati ya tohara na ukeketaji lakini mwezi ulikuwa ni mmoja.
Mama Mseti "Juzi nimeongea na baba yako nimejaribu kumueleza lakini haelewi mwanangu"
Mama Mseti alikuwa akiongea na binti mrembo aliyekuwa na sifa za kila aina za kuitwa mwanamke mzuri,ingawa alikuwa na umri mdogo lakini alikuwa na akili ya kupambanua mambo kama mtu mzima.
Binti "Lakini mama kwa nini baba anataka kunifanyia hivi?"
Mama Mseti "Mwanangu baba yako unamfahamu namna alivyomkali,pia ukikataa kufanyiwa ukeketaji mimi atanipiga mpaka aniue maana nitakuwa nimevunja mila na desturi zetu"
Mama Mseti aliendelea "Nakuomba uvumilie tu mwanangu,mbona mwenzio Wesiko alifanyiwa na sasa yupo mzima tu"
Mama mseti aliendelea kumshawishi binti Bhoke ili akubali kufanyiwa ukeketaji ili kuiheshimisha ile familia.Bhoke aliingia ndani akaanza kulia sana akiamini ule ukeketaji ulikuwa unaondoa sifa ya usichana wake.
Hakupenda kusikia kitu kinaitwa ukeketaji na ilikuwa ikimuumiza sana kuona mama yake pamoja na baba yake wakilazimisha lile jambo,yeye aliamini wazazi wake ndio wangekuwa mstari wa mbele kulikataa lakini haikuwa hivyo.Ilikuwa kabla ya ukeketaji majina yote ya mabinti waliofikisha umri wa kukeketwa yalipelekwa kwa Ngariba,Ngariba aliyefahamika kwa wakati huo na asiyekuwa na huruma hata kidogo alifahamika kwa jina moja la Nyanchimweru aliyekuwa mke wa mzee maarufu hapo Kijijini Magoto aliyefahamika kama Mzee Machera Wanyonyi.
Sauti ya kiume "Hivi hela zangu nilizoweka chini ya mtungi zimeenda wapi?"
Alikuwa mzee Gisiri Mnanka au Baba Mseti akimuuliza mkewe.
Mama Mseti "Mi hata sijui"
Baba Mseti "Hujui!,tatigha kundetera Obhokangi(Acha kuniletea ujinga),nazitaka hizo hela"
Mzee Gisiri alikuwa akimuuliza mkewe Mama Mseti kuhusu hela zake huku akiwa mwenye Jazba asiyekuwa na mzaha hata kidogo.
Mama Mseti "Sasa jamani hizo hela nichukue nipeleke wapi!"
Mama Mseti aliendelea kujitetea kwa kutolea ufafanuzi kwa upole na sauti ya hamaki na mshangao.
Baba Mseti "Nikirudi jioni kutoka mnadani nizikute hizo hela"
Ilikuwa ni sauti ya Mzee Gisiri iliyojaa jazba na msisitozo huku akifungua mlango na kuondoka zake.Mama mseti aliwaza sana ni nani atakuwa amechukua hela za mumewe ambaye ni mkorofi kupita kiasi.
Alianza kuzitafuta zile hela ndani ya nyumba bila kuambulia chochote.
Jioni ile mama Mseti alimsubiri Bhoke binti yake atoke shule uenda akawa anafahamu kuhusu hela za Baba yake,mama Mseti aliendelea kusubiri bila mafanikio ya kuonekana Kwa Bhoke,aliamua kuondoka mpaka kwa rafiki yake Bhoke ambaye aliitwa Wesiko Gisunte ili kuona kama mwanae amepita kwa huyo rafiki yake.
Wesiko "Kwani hajarudi?"
Aliendelea "Aliponipitia twende shule alikuja akasema nimsindikize Senta akapande gari anaenda Nyabitocho kupeleka hela za ng'ombe baba yake kamtuma,akaniambia atawahi kurudi"
Mama Mseti "Huyu mtoto anataka kuniingiza kwenye matatizo"
Mama mseti aliendelea kujisemea huku machozi yakimtoka akimhofia zaidi mumewe.
Wesiko "Kwani hamkumtuma?"
Mama Mseti "Amechukua hela za baba yake katoroka"
Wesiko "Sasa itakuwaje bhamure"
Wesiko ambaye alikuwa rafiki yake kipenzi na Bhoke alionekana kushangaa sana.
Mama mseti alirudi nyumbani kwake huku akiwaza namna itakavyokuwa.Haukupita muda mzee Gisiri akawa amerudi nyumbani na mama Mseti kumueleza kila kitu.
Baba Mseti "Huyo atakuwa amekimbia Saro(ukeketaji)"
Mzee Gisiri Mnanka alieleza kwa jazba sana kiasi kwamba ungejichanganya mbele yake ilikuwa ni halali yake.
Aliendelea "Nilikwambia tangia mwanzo uwe makini na huyu mtoto lakini ukawa mbishi,ona sasa,hii aibu tutaiweka wapi mama Mseti?,hivi unadhani jamii itatuchuliaje?,huyu mtoto asipopatikana na wewe uondoke hapa la sivyo nitakuua!"
Muda huo mama Mseti alikuwa ametulia tuli kama maji ya mtungi maana alifahamu kabisa angenyanyua mdomo wake,basi ingekuwa mwisho wa maisha yake.Asubuhi na mapema mzee Gisiri alienda kumuamsha kijana wake mkubwa aliyeitwa Mseti ambaye hakuwa mbali na Boma la Baba yake na kumueleza namna hali ilivyokuwa,Mseti alichukua Baiskeli akambeba Baba yake wakaanza safari ya kuelekea kijiji cha Nyabitocho ili kumtafuta binti Bhoke.
Bhoke "Nauli ya kuelekea Musoma ni ngapi?"
Ilikuwa ni sauti ya Binti Bhoke akimuuliza mmoja wa Kondakta wa Hiace zilizokuwa zimepaki stendi ya Tarime mjini zikiwa na ruti ya kuelekea Musoma.
Kondakta "Kwa wewe mwanafunzi ni elfu moja miatano"
Bhoke alichomoa hela alizokuwa ameziweka kwenye mfuko wa sketi yake ya shule aliyokuwa amevaa mpaka wakati huo.
Bhoke "Hii hapa"
Kondakta "Matiko,hebu mkatie huyu mtoto tiketi acha kushangaa bhana"
Kondakta "Ingia ukae pale nyuma jirani na yule mama"
Baada ya kupewa tiketi yake Bhoke alipewa pia utaratibu wa kukaa ndani ya ile gari,binti Bhoke aliingia na kuelekea nyuma kabisa ya siti jirani na mama mmoja wa makamo.
Wakati huo mzee Gisiri na mwanaye Mseti walipofika pale kijijini Nyabitocho walianza kumsaka Bhoke bila mafanikio yoyote.Waliendelea kutafuta maeneo mbalimbali pale kijijini ikiwemo kuuliza watu aliyofahamiana nao lakini hakufanikiwa.
Baba Mseti "Sasa atakuwa ameenda wapi?"
Aliendelea "Nitampata tu,we subiri uone"
Mzee Gisiri alisema kwa jazba huku akiendelea kumtafuta Bhoke binti yake.
Itaendelea............................
