Masulupwete
JF-Expert Member
- Feb 15, 2012
- 2,366
- 2,438
Kuna baadhi ya akinababa wamekuwa na tabia ya kuwakataa na hatimaye kuwatelekeza watoto wao hasa wale wanaozaliwa nje ya ndoa zao (waliozaa na michepuko).
Kwa uchunguzi wangu, mara nyingi mungu huwa hawatupi watoto wa aina hii. Na mara nyingi watoto huja kuwa wakombozi wa familia baadaye.
Kuna mmoja huyu ni jamaa yangu kabisa. Yeye alipata watoto 5 ndani ya ndoa na wengine 3 nje ya ndoa. Huyu jamaa yangu aliwakataa na kuwatelekeza hawa watoto wa nje ya ndoa.
Kinachotokea sasa jamaa umri umesogea anahitaji msaada wa watoto. Wale watoto 5 wamekula kona hawana habari naye na badala yake sasa anatunzwa na wale watoto 3 aliowakataa huko nyuma.
Wababa tusikatae watoto.
Mtoto hausiki kwa namna yoyote na ugomvi wa wazazi.
Mtoto ni rasilimali ya baadae.
Kitanda hakizai haramu.
Kwa uchunguzi wangu, mara nyingi mungu huwa hawatupi watoto wa aina hii. Na mara nyingi watoto huja kuwa wakombozi wa familia baadaye.
Kuna mmoja huyu ni jamaa yangu kabisa. Yeye alipata watoto 5 ndani ya ndoa na wengine 3 nje ya ndoa. Huyu jamaa yangu aliwakataa na kuwatelekeza hawa watoto wa nje ya ndoa.
Kinachotokea sasa jamaa umri umesogea anahitaji msaada wa watoto. Wale watoto 5 wamekula kona hawana habari naye na badala yake sasa anatunzwa na wale watoto 3 aliowakataa huko nyuma.
Wababa tusikatae watoto.
Mtoto hausiki kwa namna yoyote na ugomvi wa wazazi.
Mtoto ni rasilimali ya baadae.
Kitanda hakizai haramu.