Akina Butiku wapo wapi?

Akina Butiku wapo wapi?

Mzito Kabwela

Platinum Member
Joined
Nov 28, 2009
Posts
18,908
Reaction score
7,751
Kwa jinsi walivyoongea kwenye kongamano lao sikutegemea kama hawa jamaa wangekuwa kimya hivi.
Mbaya zaidi walikuwa wanaongea fact, Mzee Makamba akawaita WEHU!
Nilitegemea wangeshaonyesha msimamo wao wa kutoiunga CCM mkono waziwazi ili kubadilisha timu ya wezi na kuiweka timu ya waadilifu serikalini.

Hapa ndipo ninapoamini kuwa SIASA haiendeshwi bila unafiki!
 
Tanzania ni zaidi ya uijuavyo!!!! Umeshawahi kula ndimu mbele ya mpuliza tarumbeta??? basi ndicho CCM walichofanya kwa hawa wakuu,
 
Wapo hao viongozi si unajua siku hizi CCM wamejifanya nasi kujifanya ni wanviburi sasa sijui kile kipindi cha mwalimu walikuwa ni bendera fuata upepo au leo hao wazee wakiwaambia sio hivi oooh mbona nyie enzi zenu hamkusahihisha hivi au vile sasa imekuwa malipizano au nyie mlioko madarakani kama mliona wao walikosea na sasa si mlekebishe tuwaone mkikosolewa kubalini. tatizo viongozi wa sasa hawaambilikiki kabisa ukiwambia neno linatoke sikio la pili tena kwa speed ya ajabu kweli kweli, ati wao ndio wao jamani mmmh.

Me nadhani ni vyema tu hao wazee wakae kimya kabisa tuli na wajionee kandanda la hao CCM viongozi wa sasa maaana hawa viongozi hawataki kabisa kuingiliwa wala kushaurika kabisa ng'oooo
 
Kwa jinsi walivyoongea kwenye kongamano lao sikutegemea kama hawa jamaa wangekuwa kimya hivi.
Mbaya zaidi walikuwa wanaongea fact, Mzee Makamba akawaita WEHU!
Nilitegemea wangeshaonyesha msimamo wao wa kutoiunga CCM mkono waziwazi ili kubadilisha timu ya wezi na kuiweka timu ya waadilifu serikalini.

Hapa ndipo ninapoamini kuwa SIASA haiendeshwi bila unafiki!

Labda hawajaiona hiyo "timu ya waadilifu" na zaidi sana "iliyo tayari kutawala nchi".
 
Butiku yupo. Afya yake haijawa nzuri siku za hivi karibuni. Kafanyiwa operesheni lakini nasikia anaendelea vizuri. Tusiwe wepesi kuhukumu.
 
Kwa jinsi walivyoongea kwenye kongamano lao sikutegemea kama hawa jamaa wangekuwa kimya hivi.
Mbaya zaidi walikuwa wanaongea fact, Mzee Makamba akawaita WEHU!
Nilitegemea wangeshaonyesha msimamo wao wa kutoiunga CCM mkono waziwazi ili kubadilisha timu ya wezi na kuiweka timu ya waadilifu serikalini.

Hapa ndipo ninapoamini kuwa SIASA haiendeshwi bila unafiki!
Wafanye nini wazee wa watu? Walishajisemeaga wakamaliza, mawazoni mwao nadhani walitegemea labda ile move inge-spark reaction from the crowd (public) lakini wapi bwana.
Nani hata alitishia (kutishia tu) kufanya maandamano ya kuwaunga mkono?
Wabongo (wasomi na kinyume chake) woote kimyaaa.
Nchi hii tunahitaji Rawlings (au hata Kagame) wetu ili tunyooke na kuanza kuwa na mitizamo ambayo ni tangible.
Slaa anaweza kujaribu (na nitampigia kura kwa vile hakuna aliye bora mwingine kwa sasa), lakini sina uhakika he is as steely as those two I have mentioned.
 
Wafanye nini wazee wa watu? Walishajisemeaga wakamaliza, mawazoni mwao nadhani walitegemea labda ile move inge-spark reaction from the crowd (public) lakini wapi bwana.
Nani hata alitishia (kutishia tu) kufanya maandamano ya kuwaunga mkono?
Wabongo (wasomi na kinyume chake) woote kimyaaa.
Nchi hii tunahitaji Rawlings (au hata Kagame) wetu ili tunyooke na kuanza kuwa na mitizamo ambayo ni tangible.
Slaa anaweza kujaribu (na nitampigia kura kwa vile hakuna aliye bora mwingine kwa sasa), lakini sina uhakika he is as steely as those two I have mentioned.

Na viongozi wenzake watakuwa akina nani?
 
Na viongozi wenzake watakuwa akina nani?

Kiongozi anakuwa moja, wengine ni wasaidizi tu. Uraisi hauna ubia bali una washauri tu ambao si lazima uwasikilize - The buck stops with the President, upo ? Kiongozi anapovurunda anatakiwa awajibike na si kuwatafuta wa kuwatupia lawama kama akina Lowassa au Karamagi, hapana.
 
Butiku yupo. Afya yake haijawa nzuri siku za hivi karibuni. Kafanyiwa operesheni lakini nasikia anaendelea vizuri. Tusiwe wepesi kuhukumu.


Isije ikawa ndio mambo ya Sheikh Yahya kuwa yeyote atakayekwenda kinyume na mkwere ataadhibika; maana baada ya lile kongamano pia tulisikia Sinde warioba nae akawa mahututi akapelekwa South!! Si mlisikia kuwa mara baada ya DR. Slaa kuchukua fomu jamaa alikimbilia Msoga na baada ya siku mbili Dr. akavunjika mkono eti bafuni; lakini safari hii hata mchinje kondoo ngapi hamuachiwi mpaka kieleweke!!
 
Isije ikawa ndio mambo ya Sheikh Yahya kuwa yeyote atakayekwenda kinyume na mkwere ataadhibika; maana baada ya lile kongamano pia tulisikia Sinde warioba nae akawa mahututi akapelekwa South!! Si mlisikia kuwa mara baada ya DR. Slaa kuchukua fomu jamaa alikimbilia Msoga na baada ya siku mbili Dr. akavunjika mkono eti bafuni; lakini safari hii hata mchinje kondoo ngapi hamuachiwi mpaka kieleweke!!
Sijui ni lini wadanganyika tutaacha kuwa washirikina au kuamini ushirikina! Ni aibu
 
Wapo chadema kupitia gazeti la Raia Mwema!
Wapo sana na wanaona ila watasemea wapi wakati wapo nje ya pango??hawapewi hata nafasi yakujihusisha na shughuli zozote za chama wamekuwa kama mimi nawewe!!!wamebanwa unacheza na hicho chama???:eyeroll2:
 
wacha wakae kimya, nasikia JK kawapiga stop kujenga kikwangua anga pale haribu na ikulu, sasa unategemea watakuwa upande gani, tusubili wakati wa campain
 
Isije ikawa ndio mambo ya Sheikh Yahya kuwa yeyote atakayekwenda kinyume na mkwere ataadhibika; maana baada ya lile kongamano pia tulisikia Sinde warioba nae akawa mahututi akapelekwa South!! Si mlisikia kuwa mara baada ya DR. Slaa kuchukua fomu jamaa alikimbilia Msoga na baada ya siku mbili Dr. akavunjika mkono eti bafuni; lakini safari hii hata mchinje kondoo ngapi hamuachiwi mpaka kieleweke!!

Sh. Yahya hana lolote anatisha tu, alishindwa hata na pweza kutabiri mshindi wa World cup.
 
Sijui ni lini wadanganyika tutaacha kuwa washirikina au kuamini ushirikina! Ni aibu

Mara hapo viongozi washirikina watakapoondolewa kwenye madaraka!! Uliona wapi mkuu wa nchi anapata ushauri wa waganga wa kienyeji a' la Sangomas jinsi ya kutawala nchi na nchi ikaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom