GY
JF-Expert Member
- Nov 2, 2009
- 1,279
- 126
Ndugu yangu klorokwini, ndege ulojipatia,
Usimtupe shimoni, ndege asije kulia,
Ahsante kwa shukurani, sisi ni ndugu sawia,
Ila usije sahau, zuri kula na nduguyo.
Ndege huyo maridadi, kama ulivomsifu,
Asipigwe na baridi, wala kung'atwa siafu,
Kumtuna huna budi, Asije kupata ufu,
Msiba wake mkubwa, kufiwa na ndege wako.
Kaa naye kwa makini, haja kumtimizia,
Asijeshinda bandani, njaa kumuumizia,
Chakula alie ndani, siyo chini kumwekea,
Ndege akinona nona, ndo utamu utapata.
Hii ndo JF bwana!