Akili . . . . . !!!!

Mental age na kalendar age weka sawa tupige mahesabu, zifafanue tujiculculate
 
Mkuu hili swali la Akili ni nini linakanganya sana.
Naomba nijibu kwa uelewa wangu finyu au uelewa wenyewe ndio Akili? Wataaramu wengi wanasema akili tunazaliwa nazo ila tunachoongeza ni ufahamu na kutofautiana ni huo Huo ufahamu ndio maana kuna levo tofauti kwenye taaruma moja.
Akili ni jinsi unavyochanganua mambo kwa uelewa mpana ndio maana kuna watu hawajasoma lakini mahakama inawaita kushauri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani,mimi naamini kujifunza hakukuishia darasani,na sipendi kufanya mambo kimazoea.Kuna hii kitu nimekua nikisikia tangu mdogo,AKILI.Je ni nini?Je ni ufahamu?Inapimwaje?Shule kwa mfano,yule anaefaulu masomo huonekana ana "akili" lakini ukija mtaani unamkuta ni mlevi,mnyanyasaji,mkatili,mpenda fujo n.k,je huyu kweli ana akili?Au ubongo ni akili?Nijuavyo mimi ubongo ni kifaa anachotumia mtu kufikiri.Sasa akili iko wapi?Inakaa mwilini?Je ni eneo lipi inakaa?Au ufahamu ndio akili,Kama ni ndio ufaham ni akili?Hebu fungukeni mtusaidie sisi wenye kutanzwa na hii kitu!
1. Ukiweza kubuni jambo liwe ni biashara,afya na chochote kile kitakachoweza kutatua shida za jamii wewe= una akili

2. Ukiweza jikuta uko kwenye misukosuko ya kimaisha isiyo na ufumbuzi wa mtu mmoja peke yake lakini wewe ukaweza kujitatulia shida hiyo bila msaada wa mtu mwingine wewe= una akili

3. Kitendo cha kuandika vitabu vikatumika kufundishia watu mashuleni au mitaani na wakabadilisha maisha yao kupitia uwezo wako wewe= una akili

4. Ukipiga kitabu kama CP na ukawa mkaguzi wa mahesabu magumu,au ukapasua Sayansi mpaka tukastukia tukija hospital unatupasua kichwa na kutuludishia tena uhai na jinsi tulivyokua awali wewe= una akili

Kiufupi ni kama hivyo kwa uelewa wangu

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 
Mjadala ni mzito kweli kweli.
Naona tunachangia matokeo ya kazi ya akili hatujafikia lengo la swali.

Akili ni nini?????
 
mkuu eiyer,
akili ni ule uelewa,ufahamu na uwezo wa mtu kutafakari na kutumia maarifa aliyonayo kutoa suluhu ya matatizo mbalimbali(solution to different problems) hapa ieleweke kuwa tatizo si (negative thing) ila kama kitu kihitajicho kutatuliwa.
mfano mwanafunzi anapokuwa kwenye mtihani anakumbana na things which need solution. atatumia uelewa ufahamu na uwezo wake wa tafakuri kutoa suluhu kwa kadri inavyompasa.
akili ni imaginary kama ilivyo thought,yani huwezi ukapasua ubongo ukapima au kuona akili. akili hupimwa kwa kadri mtu anavyoweza kuleta suluhu ya mambo mbalimbali,mfano anaulwiza kitu ama anapaswa kufanya jambo analifanya kwa ufanisi na uhakiki.kwa wakati stahiki, akili hutofautiana baina ya watu.
sasa tunapokuja katika katika mtu mwenye akili kufanya matendo mabaya ni hivi huyu anaweza akawa ana ufahamu mkubwa ama uelewa mkubwa katika kitu fulani lakini sio katika kitu kingine kwa maana nyingine hakuna mwenye akili katika kila kitu. na tabia maadili na akili vyaweza visiende sambamba.
Jibu lako tosha kabisaaa mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akili ni "zao" la ubongo. Ubongo ukiwa na uwezo wa kutafakari na kupambanua changamoto zinazojitokeza na kupata ufumbuzi safi/chanya (na huenda hata ufumbuzi chanya wewe kwa maksudi ukatenda hasi) wewe bado utaitwa mwenye AKILI. Mtu anaweza kuwa bingwa wa Accounts, kwa mfano, akatumia akili hiyo KUIBIA umma. Mtu huyu atakuwa ametumia akili yake iliyotukuka kwa mtazamo hasi. Dhana hii ni tofauti na ule msemo wa wahenga kuwa AKILI NYINGI HUONDOA MAARIFA!
Huu ni mtazamo wangu tu.....

Nawakilisha
 
Jamani nami naomba nichangie kama ifuatavyo, mnataka kusema wanyama hawana akili? sidhani akili wanazo ila tumewazidi ufahamu, akili imetokana na ubongo, ubongo unaonekana akili haionekani ila akili tunaitafsiri kwa sababu tuna ufahamu, kwenye ufahamu ndipo tulipowazidi wanyama

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom