kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
MSICHANA Jacklin [24] mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam amejitokeza na kutoa ushuhuda mbele ya wanawake kwa kujisifia kuvunja ndoa ya bosi wake kwa kujiita ni mwanamke wa kuigwa katika jamii.
Hayo aliyasema katika hafla fupi ya kumfunda mwali wa kike maarufu kama Kitchen Party iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita huko maeneo ya Kibaha mkoani Pwani.
Msichana huyo alitoa ushuhuda huo kwa kuwafundisha wanawake waliokuwa na tabia ya kuwaachia kila kitu wasichana wao wa kazi na hivyo kujenga tabia ya kutozishughulikia nyumba zao.
Akitoa mada aliyoiita "mwanamke bora" alifafanua neno hilo na kujipa mfano yeye mwenyewe alivyokuwa bora katika familia ya mume wake wakati alipokuwa akifanya kazi za ndani kabla hajaweza kuolewa na mwanaume huyo.
Alisema kuwa jamani wanawake wenzangu tujitahidi kuangalia nyumba zetu sio tunawaachia wasichana wa kazi kila kitu hiyo ni hasara jamani, unaweza ukahatarisha ndoa yako
Mimi nilikuwa msichana wa kazi za ndani miaka miwili iliyopita bosi wangu wa kike alikuwa hashughuliki na nyumba yake kabisa na kuniachia kila kitu mimi na yeye ilikuwa kila kukicha anakwenda kwenye shughuli zake na akitoka anaranda na huwa anarudi usiku na wala alikuwa hana hata muda wa kumungalia mume wake na hata mtoto wake alikuwa hamshuhulikii".
Aliendelea kwa kusema kuwa tabia hiyo ilimchosha mume wa mwanamke huyo ambaye alikuwa sio msemaji na kila anapomkanya alikuwa hamsikii kabisa.
Mume wa mwanamke huyo alichoshwa na vitendo vya mke wake vya kutokumjali hata hajui mke wake kama anajua kupika ama la kwa kuwa alikuwa hashughuliki na mapishi.
"Hivyo mume huyo alinitaka mimi niondoke kwa muda kwa kuwa mke wake alikuwa hajishughulishi kwa kuona alikuwa na msaidizi".
Katika hali hiyo mwanamke huyo hakukubaliana na kitendo cha kumuondoa msichana huyo na kumwambia mtoto angepata shida na kumtaka msichana huyo asiondoke
Hali hiyo iliendelea na baadae baba huyo alidai alimtaka kumuoa msichana huyo kwa kuona kuvutia na utendaji wake kazi lakini msichana huyo alidai hakuafiki kabisa kwa kumlindia heshima bosi wake wa kike.
Hata hivyo mwanaume alimlazimisha amuoe na alituma washenga nyumbani kwa msichana huyo kwa lengo la kumuoa bila ya mke wake kujua na hatimaye alipomaliza hatua za awali alimtaka msichana huyo amuage mke wake kuwa anahitajika nyumbani kwao mkoani Morogoro kwa muda wa siku mbili ili akamuoe.
Hata hivyo bosi wake hakufahamu hilo alimruhusu na kumsihi asizidishe siku tatu arudi na alipoenda kwao alienda kuolewa na mume wa mwanamke huyo na aliporudi alimtambulisha mke wake kuwa kuanzia sasa msichana huyo ni mke mwenzake.
Ndipo mwanamke huyo alianza vurugu za hapa na pale akimtaka mume wake ampe talaka ili ampishe aweze kuishi na msichana huyo.
Na hatimaye mwanamke huyo alidai talaka kinguvu na aliweza kuondoka nyumbani hapo.
Jamani tutunze nyumba zetu, tuwatunze waume zetu, tutunze watoto wetu na si kuwaachia wasichana wa kazi kila kitu mtavunja nyumba zetu alimalizia msichana huyo
Hata hivyo baadhi ya wanawake ukumbini hapo walivutiwa na msichana huyo huku wengine wakiwa wanamlaani kwa kitendo chake cha kuvunja ndoa ya mwanamke mwenzake bila hata huruma.
Hayo aliyasema katika hafla fupi ya kumfunda mwali wa kike maarufu kama Kitchen Party iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita huko maeneo ya Kibaha mkoani Pwani.
Msichana huyo alitoa ushuhuda huo kwa kuwafundisha wanawake waliokuwa na tabia ya kuwaachia kila kitu wasichana wao wa kazi na hivyo kujenga tabia ya kutozishughulikia nyumba zao.
Akitoa mada aliyoiita "mwanamke bora" alifafanua neno hilo na kujipa mfano yeye mwenyewe alivyokuwa bora katika familia ya mume wake wakati alipokuwa akifanya kazi za ndani kabla hajaweza kuolewa na mwanaume huyo.
Alisema kuwa jamani wanawake wenzangu tujitahidi kuangalia nyumba zetu sio tunawaachia wasichana wa kazi kila kitu hiyo ni hasara jamani, unaweza ukahatarisha ndoa yako
Mimi nilikuwa msichana wa kazi za ndani miaka miwili iliyopita bosi wangu wa kike alikuwa hashughuliki na nyumba yake kabisa na kuniachia kila kitu mimi na yeye ilikuwa kila kukicha anakwenda kwenye shughuli zake na akitoka anaranda na huwa anarudi usiku na wala alikuwa hana hata muda wa kumungalia mume wake na hata mtoto wake alikuwa hamshuhulikii".
Aliendelea kwa kusema kuwa tabia hiyo ilimchosha mume wa mwanamke huyo ambaye alikuwa sio msemaji na kila anapomkanya alikuwa hamsikii kabisa.
Mume wa mwanamke huyo alichoshwa na vitendo vya mke wake vya kutokumjali hata hajui mke wake kama anajua kupika ama la kwa kuwa alikuwa hashughuliki na mapishi.
"Hivyo mume huyo alinitaka mimi niondoke kwa muda kwa kuwa mke wake alikuwa hajishughulishi kwa kuona alikuwa na msaidizi".
Katika hali hiyo mwanamke huyo hakukubaliana na kitendo cha kumuondoa msichana huyo na kumwambia mtoto angepata shida na kumtaka msichana huyo asiondoke
Hali hiyo iliendelea na baadae baba huyo alidai alimtaka kumuoa msichana huyo kwa kuona kuvutia na utendaji wake kazi lakini msichana huyo alidai hakuafiki kabisa kwa kumlindia heshima bosi wake wa kike.
Hata hivyo mwanaume alimlazimisha amuoe na alituma washenga nyumbani kwa msichana huyo kwa lengo la kumuoa bila ya mke wake kujua na hatimaye alipomaliza hatua za awali alimtaka msichana huyo amuage mke wake kuwa anahitajika nyumbani kwao mkoani Morogoro kwa muda wa siku mbili ili akamuoe.
Hata hivyo bosi wake hakufahamu hilo alimruhusu na kumsihi asizidishe siku tatu arudi na alipoenda kwao alienda kuolewa na mume wa mwanamke huyo na aliporudi alimtambulisha mke wake kuwa kuanzia sasa msichana huyo ni mke mwenzake.
Ndipo mwanamke huyo alianza vurugu za hapa na pale akimtaka mume wake ampe talaka ili ampishe aweze kuishi na msichana huyo.
Na hatimaye mwanamke huyo alidai talaka kinguvu na aliweza kuondoka nyumbani hapo.
Jamani tutunze nyumba zetu, tuwatunze waume zetu, tutunze watoto wetu na si kuwaachia wasichana wa kazi kila kitu mtavunja nyumba zetu alimalizia msichana huyo
Hata hivyo baadhi ya wanawake ukumbini hapo walivutiwa na msichana huyo huku wengine wakiwa wanamlaani kwa kitendo chake cha kuvunja ndoa ya mwanamke mwenzake bila hata huruma.