Ajira nihurumie nifurahi na mimi pia

Ajira nihurumie nifurahi na mimi pia

JOESKY

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2015
Posts
823
Reaction score
2,044
Maisha ni kitendawili kigumu ambacho kwa sisi wanadamu kukitegua tunashindwa kabisa kutokana na ugumu wake.

Ama kwa hakika mambo hayajawa mepesi mpaka ugumu ukukumbatie.

Ni mwaka mwingine bado namaliza soli ya kiatu kusaka fursa ya ajira au kibarua nipate kuweka mkono kinywani ila still mambo yananipiga makofi ya uso naona nyota nyota tu.

Sijui ugumu huu nakutana nao mimi tu?

Kama kutafuta ajira nimezunguka shule zote za sekondari na medium naishia kuacha barua tu na kufanya interview nimepita kwenye taasisi na mashirika bado bahati si yangu.

Nakuomba mpenzi wa hili jukwaa nikutanishe na ajira nami nifurahie maisha kama wengine ajira yoyote ya kunipatia kipato nitafurahi sana niweze angalau kunywa chai na mhogo badala ya slace mbili za mkate na maji yenye glucose.

Nipo mbeya PM for details
 
SGR na Nyerere dam ndiyo nyimbo zinazotrend.
 
Usisahau kutinga ofisi za CCM ukiwa na kadi ya Chama Kuna ajira zimejaa pomoni.
 
Usisahau kutinga ofisi za CCM ukiwa na kadi ya Chama Kuna ajira zimejaa pomoni.
Nashukuru kwa kejeli mkuu ila kwa kifupi mimi sio mwanaccm by the way nimekuelewa asante kwa ushauri
 
Back
Top Bottom