The golden
JF-Expert Member
- Sep 11, 2018
- 1,383
- 2,586
Nadhani kuna mahali watu hawajafikiri vizuri. Hii ajenda ya maslahi kwa watumishi wa uma ,hasa ogezeko la mishahara na kupanda vyeo si ajenda ya kupuuza hata kidogo.
Kwa maoni yangu hakuna kitu hatari kama hiki ,kwa sababu hili linagusa maisha ya watu moja kwa moja. Huu ni mkate wa kula siku na binadamu akianza kukosa mkate ,ubinadamu huanza kumtoka na unyama huingia kwa kasi ya kutisha.
Nimezungumza na watumishi wa kada mbalimbali mioyo yao imevimba kwa hasira. Kichwani wamebeba furushi kubwa la manun'guniko.
Nataka nishauri ,tena natoa ushauri huu kwa moyo safi kabisa. Swala hili kama litaendelea kupuuzwa tutakuwa tunatengeneza hatari kubwa sana. Sitaki yatokee mabaya. Kama kuna watu wanawashauri vibaya viongozi ,watu hao waache Mara moja.
Kwa maoni yangu hakuna kitu hatari kama hiki ,kwa sababu hili linagusa maisha ya watu moja kwa moja. Huu ni mkate wa kula siku na binadamu akianza kukosa mkate ,ubinadamu huanza kumtoka na unyama huingia kwa kasi ya kutisha.
Nimezungumza na watumishi wa kada mbalimbali mioyo yao imevimba kwa hasira. Kichwani wamebeba furushi kubwa la manun'guniko.
Nataka nishauri ,tena natoa ushauri huu kwa moyo safi kabisa. Swala hili kama litaendelea kupuuzwa tutakuwa tunatengeneza hatari kubwa sana. Sitaki yatokee mabaya. Kama kuna watu wanawashauri vibaya viongozi ,watu hao waache Mara moja.