Ajali ya boti Bukoba, 28 waokolewa

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626
Inasemekana jana kwenye Kisiwa cha Kelebe, Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera boti iliyokuwa inatokea Ukerewe kuelekea Bukoba ilizama na kati yao 25 waliokolewa, huku mtu mmoja akiwa hajulikani alipo.

Ikiwa imepita siku tatu bila ya mtu huyo kupatikana katika uokozi huo itachukuliwa kama amefariki.

Kwa upande mwingine chanzo kingine kimedai kuwa boti ilikuwa na watu 50 na waliookolewa ni watano pekee.

boti.jpg


Taarifa zaidi zitakujia kadri zitakavyopatikana.


===============

UPDATES...
Alipoulizwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Blasius Chatanda amesema “Boti ilizama saa tatu asubuhi ya Julai 22, 2023, ilibeba watu 29, kati ya hao mmoja hajulikani alipo wengine wameokolewa, sababu ya kuzama ni upepo mkali na sio kweli kuwa ilibeba watu 50, Boti za huku hazina uwezo wa kubeba watu wote hao.”
 
Kuna haja hilo eneo na vyombo kufanyiwa utafiti.Tujue haya matukio ni uzembe au kuna sababu za kisayansi?Maana kunatia mashaka sasa.
 
Kuna haja hilo eneo na vyombo kufanyiwa utafiti.Tujue haya matukio ni uzembe au kuna sababu za kisayansi?Maana kunatia mashaka sasa.
Mkuu kipindi hiki kuna upepo wa kusi unatesa sana vyombo. Huko Kelebe ni kina kirefu na upepo ukikufamania na chombo ikazima na kupelekea kupelekwa na wimbi, kuzama hakuepukiki. Maji yasikie tu ndugu.
 
Ziwa Victoria upande wa Bukoba itakuwa Kuna nguvu za uvutano (gravitational force) kubwa kuliko kawaida ndiyo maana ndege huanguka na boti huzama mara kwa mara.

Serikali legevu huwa zinasubiri majanga badala ya kufanya utafiti na kutafuta suluhu ya kudumu.
 
Movement ya continental plates,ocean currents na gravitational forces mnaotafuta PhD na masters za geography kwanini msifanyie research hii kitu?
 
Mkuu kipindi hiki kuna upepo wa kusi unatesa sana vyombo. Huko Kelebe ni kina kirefu na upepo ukikufamania na chombo ikazima na kupelekea kupelekwa na wimbi, kuzama hakuepukiki. Maji yasikie tu ndugu.
Kuna jambo linatakiwa kufanyika lakini. Hiyo ndo maana ya kuwa na nchi inayoongozwa na raisi na kuna wataalamu. Huenda aina za vyombo huchangia. Yote haya yanahitaji tafiti. Sema hapa Afrika hili si la msingi sana maana haligusi maslahi ya wakubwa kiviile.
 
Back
Top Bottom