Ajali Ubungo Riverside

Ajali hadi mjini?? Duh, haya wapumzike kwa amani na MUNGU atusaidie tuepukeane na ujinga huu wa kuendesha magari yasiyofanyiwa service
 
Nasikia ni watu kama 5 na lori tanker liacha njia na kulali magari mengine na wamachinga wapita njia ajali mbaya sana
 
Speeding na yenyewe ni shida sana kwetu huku. Malori yakitoka ubungo kwenda Buguruni huwa nayakuwa katik mwendo mkali sana, mpaka inakera. Poleni mliopata ajali, Mungu awape tulizo
 
Sawa mkuu ila tupe idadi kamili maana tuna ndugu wengi maeneo hayo na especially hiyo barabara
 
Ajali Mbaya (Ubungo Riverside): Lori laacha njia na kuua watu, maiti 20 zishapatikana
 
Sijaipata vema, ila ni ajali mbaya, watu watatu wamekufamo na wengine bado wamekwama mu-gari.
Source: East Africa Radio


katikati ni gari ndogo nyekundu iliyokandamizwa chini ya gari kubwa jeupe la mafuta. kuna mtu yuko hai bado hajatolewa. habari zinasema watu watatu wamekufa kati yao mama mjamzito ambaye kichwa na kiwiliwili vimetengana



Baadhi ya watu katika eneo la ajali
Na Mjengwablog
 
mimi nilikuwepo tanker lilkuwa linatoka ubungom kuelekea buguruni kufika kituo cha daladala cha riverside likakuta daladala limepaki njiani na kwa kuwa lilikuwa mwendo kasi likashindwa kufunga breki likapanda ukuta na kugonga gari zilizo kuwa kwenye foleni zinatoka buguruni kuja ubungo,yule mwenye daladala mwenye makosa kakimbia,ajali ni mbaya sana kuna mama kakatika kichwa hapohapo,lecturer mmoja wa chuo kikuuu namfahamu kwa sura amepona pia ila amenusurika na gari yake.
 
RIP waliopoteza maisha.

Nina amini kabisa kuwa mtu angefanya kazi yake ipasavyo tusingekuwa na madereva walio chini ya kiwango, kusingekuwa na scrap vehicles on roads. Ila kwa kuwa tunapenda cheap solution hatukawii kusingizia kazi ya mungu, au hata ya Al shabaab tusivyokuwa na soni.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom