Ajali nyingine mbaya Kahama!

Kassim Awadh

JF-Expert Member
Mar 12, 2012
884
187
P1590005[1].JPG P1580990[1].JPG P1580981[1].JPG P1580982[1].JPG P1590034[1].JPG DSC00022[1].JPG
Imetokea asbh leo. Basi la kampuni ya RS limegongana na lori la kampuni ya Dhandho. Basi ilikuwa linatokea Dar kwenda Bukoba ambapo Lori lilikuwa linatokea Ushirombo kwenda Dar. Chanzo ni dereva wa lori kumkwepa mwendesha baiskeli ambapo alihama upande wake na kumfuata mwenye basi. Watu watatu wamekufa palepale na wengine kujeruhiwa vibaya ikiwemo kukatika miguu. Picha mojawapo anaonekana askari polisi akiwa ameshika mguu uliokatika ukiwa ndani ya kiatu na nyingine ni majeruhi aliyekatika mguu akiwa hospitali.
 
poleni sana leo mbona ajali nyingi sana? Hawa madereva wanazuta bangi nini? Kuna uzembe hapa unafanyika
 
poleni sana leo mbona ajali nyingi sana? Hawa madereva wanazuta bangi nini? Kuna uzembe hapa unafanyika

Na sheria za barabarani ni mbovu, hazilindi abiria. Tutachinjwa mpaka tutakapo pata serikali inayojali maisha ya wananchi. Kwa sasa serikali dhaifu ya Vasco tusahau kuwajibishwa mtu
 
Aiseeee ni ajali mbaya sana. Nashani week hii imekuwa mbaya sana kutokana na ajali kuzidi.
 
Traffic wapo busy kuongoza misafara ya viongozi wa CCM waliokuwa kwenye chaguzi za nafasi mbalimbali za uongozi kichama!
 
poleni wote mliopatwa na matatizo!!!Tuchukue hatua gani kitaifa jamani kuzuia hili janga la ajali?
 
Umenistusha, kumbe ni ile ya asbh! Mungu awatie nguvu wafiwa wote, na awajaalie afya njema majeruhi wote na kuwalaza mahali pema peponi waliopoteza maisha. AMEEN!
 
Yaani baada tu ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani kupita tunachokishuhudia ni ajali kuzidi sijui maana yake nini hii makitu......................!!
 
Hizi accident nyingine tatizo ni uzito wa madereva kufanya uamuzi. Ukweli ni kwamba uwezo wa kufanya uamuzi wa binadamu (IQ) unatofautiana sana. Kuna madereva wengi sana barabarani ambao IQ zao ziko chini sana, na wana uwezo wa kuendesha gari ikiwa kila kitu kiko safi barabarani. Pale wanapopata challenge kidogo tu basi wanafanya uamuzi wa ajabu sana ambao mara nyingi husababisha madhara na vifo.

Kuna wakati nilipendekeza kwamba madereva wa mabasi wawe wanafanyiwa kitu inaitwa psychometric test. Kuendesha gari si suala tu la kujua jinsi ya kunyoosha usukani na kubadilisha gia. Kukwepa baiskeli wakati kuna basi upande wa pili ni mojawapo ya dalili kuonyesha uwezo mdogo wa kufikiri na kufanya uamuzi wa busara na haraka wa huyo dereva wa lori. Kuna madereva IQ zao ni sawa na mtu aliyekunywa chupa nzima ya whisky ndio aendeshe gari.
 
Back
Top Bottom