TANZIA Ajali Mbeya: Watu wanne akiwemo Mkurugenzi wa Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora wamefariki dunia

Watu kadhaa wanahofiwa kufariki dunia huku wengine wakijeruhiwa baada ya Lori kufeli breki na kugonga Magari madogo mawili, katika mteremko wa Inyala mkoani Mbeya.


Endelea kutufuatilia kwa taarifa zaidi.

ITV

==============================

Watu wanne akiwemo Mkurugenzi wa Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora, wadaiwa kufariki dunia hii leo huku wengine kadhaa wakijeruhiwa baada ya Lori kufeli breki na kugonga magari madogo mawili, katika mteremko wa Inyala Mkoani Mbeya.

Sasa viongozi wameanza kufa naeneo haya ya Inyala.
Kwa mwezi wanakufa watu 5 hadi 20.
Mwezi wa July maeneo hayo lori lililofeli breki liliua watu 20 pale Inyala crissing ya TAZARA.
Mimi niliona kwa macho.

Tumelia watu wa Mbeya juu ya barabara hii hadi tumechoka wenyewe.
Sasa viongzi wanakufa, pengine serikali itafumbua macho.
 
Lori limefeli breki mteremko wa Inyara likaparamia hizo gari ndogo. Dereva hausiki hata kidogo

Pengine hujafatilia vizuri hii taarifa! Huyu DED na dereva wake waliambiwa wasimame wsiendelee na safari kwakuwa ulikuwa ni muda wa magari makubwa kupita lakini wao wakasema wana haraka sana! Kufika mbele wakasimama kununua mahitaji! Walipotaka kurndelea nasafari tena waliambiwa tena na askari kuwa muda wa kupita magari madogo umepita ni zamu ya magari makubwa!

Baada ya kuwasha gari na DeD kupanda nakuanzq safari ndipo lori lilikuwa kwenye speed likafeli break na kuvamia magari mengine pamoja na gari la DED!

Ubishi umewauwa!
 
Wakuu kuna klipu nimesikiliza alikuwa anaongea mkuu wa mkoa wa mbeya anadai kuwa ile sehemu gari uwa zinapishana yaani yanaanza malori zeni yanafuata magari madogo sasa uyu marehemu alikaidi zamu ya gali ndogo kupita ilikuwa imeisha na malori yalikuwa yameanza kuruusiwa kupita kwa iyo marehemu alidai anawai basi ikabid apite umauti ukampita. Shida niliyoiona viongozi wetu wakaidi sana ndio wavunja Sheria wakubwa
 
Madereva wa serikali na viongozi wao ni wabishi sana hata wakisimamishwa na askari wanajiona wako juu ya sheria , wanapitaga kwenye barabara za mwendokasi na spidi zaidi ya 240 utadhani wako selous huko, nchi ngumu sana hiyo, mtu akielezwa ukweli anakua mkali
 
Pengine hujafatilia vizuri hii taarifa! Huyu DED na dereva wake waliambiwa wasimame wsiendelee na safari kwakuwa ulikuwa ni muda wa magari makubwa kupita lakini wao wakasema wana haraka sana! Kufika mbele wakasimama kununua mahitaji! Walipotaka kurndelea nasafari tena waliambiwa tena na askari kuwa muda wa kupita magari madogo umepita ni zamu ya magari makubwa!

Baada ya kuwasha gari na DeD kupanda nakuanzq safari ndipo lori lilikuwa kwenye speed likafeli break na kuvamia magari mengine pamoja na gari la DED!

Ubishi umewauwa!
Mkuu sio kwamba sijafuatilia, baada ya ajali sisi wakazi wa Mbeya tulimsikia Mkuu wa Mkoa akitoa maelezo ambayo ndiyo yalikuwa msingi wa mimi kukubishia. Baadaye RPC anatoa maelezo kama haya uliyotoa wewe. Naamini RPC yuko sawa, hawa wanasiasa hawaaminiki kabisa. Huyu Mh Omera ni longolongo sana, aliongea as if wahanga wa jali hawakuvunja sheria yoyote. Na aliwahi kutusingizia kuwa tumemtuma kuwa tunapenda na tunaikubali sana tozo.

Mkuu uko sawa nilimuona na kumsikia RPC akiongea.
 
Back
Top Bottom